Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNAB M. VULLU (K.n.y MHE. MARIAM N. KISANGI) aliuliza:- Ongezeko la watoto wenye matatizo ya afya ya akili na ubongo limekuwa kubwa kwa sasa katika nchi yetu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha vitengo vya elimu kwa watoto wenye mahitaji maalum (walemavu) wa viungo na ubongo?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYNAB M. VULLU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Swali la kwanza, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, bado inaonekana kuna tatizo la uhaba wa Walimu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inatoa Walimu wa kutosha ili waweze kufika kwenye Halmashauri zetu. Pia kuwa uwezo wa kupata Walimu wengi kwa sasa hivi haupo, je, hakuna haja ya kwamba wachukue Maafisa Afya kwenye Kata zetu waweze kusaidia watu ambao wana watoto wenye matatizo ya akili? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa, tatizo la ugonjwa wa akili au usonji linaongezeka nchini. Je, chanzo cha tatizo hilo ni nini, ni lishe duni, uhaba wa madini wakati mama anapokuwa mjamzito au ni nini kinachopelekea mpaka kuwa na idadi kubwa ya watu wenye ugonjwa wa akili? (Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama alivyosema kwamba kwa kiasi fulani kuna changamoto ya kuwa na Walimu wa kutosha kwa ajili ya kuwafundisha watoto wenye matatizo ya akili na usonji. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba pamoja na changamoto hiyo Wizara imejipanga kuhakikisha kwamba katika siku za huko mbele tatizo hilo linaondoka.
Mheshimiwa Naibu Spika, mikakati hiyo imeanza kwa kujenga chuo cha kisasa cha kufundishia Walimu cha Patandi. Tunajenga The State of Art College kwa ajili ya kufundisha Walimu watakaotoa huduma kwa wanafunzi wenye mahitaji hayo. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba siyo kwamba Serikali haijajipanga. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile wazo lake alilopendekeza kwamba tuwatumie Maafisa Maendeleo ya Jamii tutalifikiria kuangalia namna tutakavyoweza kufanya kazi pamoja na kwamba tunafahamu kwamba unahitaji watu maalum ambao wanajua saikolojia na namna nzuri ya kuwafundisha watoto hao.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na chanzo, kuna vyanzo mbalimbali vinavyosababisha watoto wazaliwe wakiwa na hayo matatizo. Mojawapo ni suala la alcoholic disorders hasa kwa akinamama wajawazito. Ni muhimu sana kujua kwamba tayari kuna tafiti zinaonesha kwamba kama mzazi akiwa mjamzito atakuwa mlevi sana inasababisha mara nyingi mtoto kuzaliwa akiwa na haya matatizo. Sababu ya pili ni kwamba magonjwa mengine ni ya kurithi, kwamba watoto wanazaliwa kwa sababu wamerithi kutoka kwa wazazi na kuna sababu nyingine, kwa vyovyote vile nina uhakika wenzetu wa afya wanaweza wakawa na taarifa sahihi zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kama wameongezeka au hawajaongezeka, kama Wizara ya Elimu tunachofahamu na tunachofanya ni kwamba, tunajua tumeendelea kuongeza uwezo wetu wa kuwapokea wengi zaidi. Ndiyo maana kama ninavyosema, tumeendelea kutenga fedha kila mwaka; mwaka huu tumetenga shilingi bilioni 3.5 kuhakikisha kwamba wanafunzi wale katika shule za msingi na sekondari wanapata vifaa vya kuwafundishia. Vilevile hata katika ujenzi wa majengo wa sasa ukienda kwenye shule za msingi yanajengwa ili yaweze kukidhi mazingira maalum ya wanafunzi wa aina hii. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII,
JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, nataka kuongeza maelezo mafupi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali sasa hivi ina mkakati, imeonekana kwamba siku 1,000 za mwanzo za mtoto baada ya kuzaliwa iwapo atapata tatizo la utapiamlo zinamuathiri sana katika kukua vilevile kiakili. Kwa hiyo, sasa hivi Serikali kupitia Taasisi yake ya Lishe, imeweka mkakati wa kuhakikisha kwamba siku 1,000 za mwanzo mtoto anapata lishe nzuri ili kuhakikisha kuwa anakua vizuri na anapata uwezo mzuri wa kuweza kuwa na akili sawasawa.

Name

Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNAB M. VULLU (K.n.y MHE. MARIAM N. KISANGI) aliuliza:- Ongezeko la watoto wenye matatizo ya afya ya akili na ubongo limekuwa kubwa kwa sasa katika nchi yetu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha vitengo vya elimu kwa watoto wenye mahitaji maalum (walemavu) wa viungo na ubongo?

Supplementary Question 2

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweza kuwapatia wanafunzi hususan wa shule za msingi angalau mlo mmoja kwa siku?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ni lini Serikali itahakikisha kwamba wanafunzi watapata angalau mlo mmoja kwa siku, naomba nimfahamishe Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari kuna utaratibu unaoendelea kwenye shule nyingi nchini kuhakikisha kwamba wanafunzi wanapata uji wakiwa shuleni. Hata hivyo, katika Mpango wetu wa elimu bila malipo, tayari tunafikiria kufanya maboresho ili masuala kama haya ya mlo vilevile yaweze kuchukuliwa

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. ZAYNAB M. VULLU (K.n.y MHE. MARIAM N. KISANGI) aliuliza:- Ongezeko la watoto wenye matatizo ya afya ya akili na ubongo limekuwa kubwa kwa sasa katika nchi yetu:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha vitengo vya elimu kwa watoto wenye mahitaji maalum (walemavu) wa viungo na ubongo?

Supplementary Question 3

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Jimbo la Lupembe katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, tuna shule moja ya Matembwe ambapo watoto wenye ulemavu tofauti tofauti wanasoma pale na tuliomba vifaa vya kufundishia na kujifunzia wanafunzi kutoka Wizarani au Serikali lakini mpaka sasa bado hatujapata. Nataka kujua ni lini Serikali italeta vifaa kwa ajili ya kuwawezesha watoto wale waweze kupata elimu vizuri, kwa kuwa vifaa sasa hivi hawana? Ahsante.(Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka uliopita 2016/2017, tulitoa vifaa kwa shule 213 za msingi na shule 22 za sekondari. Mwaka huu tumetenga shilingi bilioni 3.5 kwa ajili ya kununua vifaa. Naomba Mheshimiwa Mbunge aongozane nami nikitoka leo Bungeni ili anieleze mazingira ya shule yake tuweze kuweka kwenye utaratibu wa kugawa vifaa katika bajeti ya mwaka huu.