Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Tabitha Chagulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA aliuliza:- Hospitali ya Mkoa wa Geita inakabiliwa na kero mbalimbali kama vile ukosefu wa Madaktari Bingwa wa akinamama na watoto, dawa, vifaa tiba pamoja na uhaba wa majengo ya wodi za wazazi:- Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kutatua kero hizo katika Hospitali ya Mkoa wa Geita?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza niishukuru sana Serikali kwa mkakati huo, pia nimshukuru sana Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri na ya kutia moyo. Nina swali moja tu la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Mkoa wa Geita imekuwa ikihudumia wagonjwa wengi sana kiasi kwamba inaelemewa kabisa. Hii ni kutokana na mapungufu makubwa yaliyopo katika Hospitali zetu za Wilaya. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuweza kuboresha hospitali zetu hizi za Wilaya ili kupunguza msongamano wa wagonjwa uliopo katika Hospitali yetu ya Mkoa wa Geita? Ahsante.
(Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi Serikali ina nia njema ya kuhakikisha kwamba, kwanza si kuimarisha Hospitali za Wilaya, tunaanzia kwanza kuimarisha vituo vya afya ndiyo maana pesa nyingi sana imepelekwa ili kupunguza ule msongamano ambao wananchi watalazimika kwenda hospitali ya Wilaya. Kama hilo halitoshi tunajua kabisa, ili kuweza kupunguza mlundikano kwa wananchi ambao wangependa kwenda hospitali za mikoa ni kuwa na uhakika wa kutibiwa katika hospitali za wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwatake wananchi na Halmashauri zetu zote nchini, wahakikishe kwamba, maeneo kwa ajili ya kujenga hospitali za Wilaya yanatengwa kwa kufuata viwango ambavyo vinatakiwa na Halmashauri kwa kutumia own source waanzishe na Serikali itaweka mkono wake. (Makofi)

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA aliuliza:- Hospitali ya Mkoa wa Geita inakabiliwa na kero mbalimbali kama vile ukosefu wa Madaktari Bingwa wa akinamama na watoto, dawa, vifaa tiba pamoja na uhaba wa majengo ya wodi za wazazi:- Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kutatua kero hizo katika Hospitali ya Mkoa wa Geita?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Matatizo ya upungufu wa Madaktari, watumishi wengine wa afya na vifaa tiba yaliyoko hospitali ya Mkoa wa Geita ni sawa kabisa na yale yaliyoko kwenye Hospitali ya Wilaya ya Ukerewe, Hospitali ya Nansio. Serikali iko tayari sasa kuangalia visiwa vya Ukerewe kwa upendeleo maalum na kutusaidia kuondoa tatizo hili ili kupunguza vifo vya akinamama na watoto visiwa vya Ukerewe?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli. Mheshimiwa Mbunge anakiri kwamba, nilipata fursa ya kwenda na tuliweza kufika mpaka kule Ukerewe na ni kweli changamoto ya afya katika visiwa vile imekuwa ni kubwa zaidi. Ndiyo maana katika vipaumbele vyetu sasa hivi hata ukiangalia idadi ya Madaktari ambao juzi tu tumewaajiri, tumeajiri Madaktari takribani 2,058, tumepeleka vijana kule kwa ajili ya kusaidia suala la changamoto inazozipata.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, kuna fedha vilevile tunaenda kuboresha kile kituo cha afya kama alivyopendekeza Mheshimiwa Mbunge na hatutasita kuendelea. Tunafanya juhudi ya kutosha hasa kwa sababu tunajua kwamba eneo la Ukerewe lazima tuboreshe miundombinu ili hata watumishi tunaowapeleka kule wawe na hamasa ya kufanya kazi baada ya kuboresha mazingira yao. Kwa hiyo, jukumu hili tumelichukua sisi Serikali kwa ajili ya maslahi mapana ya wananchi wa Ukerewe.

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA aliuliza:- Hospitali ya Mkoa wa Geita inakabiliwa na kero mbalimbali kama vile ukosefu wa Madaktari Bingwa wa akinamama na watoto, dawa, vifaa tiba pamoja na uhaba wa majengo ya wodi za wazazi:- Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kutatua kero hizo katika Hospitali ya Mkoa wa Geita?

Supplementary Question 3

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Hospitali ya Geita ambayo sasa hivi ni Hospitali Teule ya Mkoa ilikuwa Hospitali ya Wilaya. Hata baada ya kuipandisha hadhi na kuwa hospitali ya mkoa imeendelea kupata huduma kutoka Serikali Kuu kama hospitali ya wilaya. Je, ni lini Serikali itaipatia huduma kama hospitali ya mkoa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba, kwa sababu imepandishwa, tunalifanyia kazi. Hata hivyo juhudi tuliyofanya kubwa kama Serikali ni kuhakikisha tunaanza hospitali ile kubwa ya Rufaa ya Mkoa, juzi Naibu Waziri wangu nimemtuma kuna kazi kubwa imeshaanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwahakikishie wananchi wa Geita kwamba Serikali tumejipanga kuboresha sekta ya afya katika Mkoa wa Geita kwa ujumla wake ili kuimarisha hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa na hospitali ya Mkoa na hali kadhalika vituo vya afya, tukijua kutokana na uchimbaji wa madini population imekuwa kubwa katika maeneo hayo. Kwa hiyo, kama Serikali tumelichukua, tutalifanyia kazi kuhakikisha tunapata idadi ya dawa zinazohitajika katika hospitali. (Makofi)