Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa vifaa tiba kwenye Hospitali ya Wilaya ya Singida Mjini au kituo cha afya Sokoine?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru sana. Namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, pamoja na kazi nzuri sana inayofanywa na Serikali lakini bado kuna changamoto kubwa kwa akina mama wajawazito wanapokwenda hospitali za umma kwa ajili ya kupata vipimo na matibabu mengine, vifaa havipatikani. Je, Serikali inatoa tamko gani juu ya hili?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Serikali inafanya kazi nzuri sana ya zoezi la ukusanyaji damu salama na imetoa mwongozo mzuri kwa Halmashauri zetu kutenga bajeti kwa ajili ya kukusanya damu salama, lakini bado ziko Halmashauri zimeshindwa kutenga bajeti hiyo. Je, Serikali pia inatoa tamko gani kwenye Halmashauri hizi zilizoshindwa kufanya kazi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu katika swali langu la nyongeza na mwenyewe amekiri jitihada kubwa ambazo zinafanywa na Serikali ili kuhakikisha kwamba vifaa tiba vinapatikana na kuondoa adha na hasa kwa akinamama kama ambavyo na yeye mwenyewe amekuwa mdau mkubwa kuhakikisha kwamba akinamama hawapati adha hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee naomba niendelee kupongeza Halmashauri yake ambayo Mheshimiwa Mbunge amekuwa akihakikisha kwamba vifaa tiba vinanunuliwa. Nizitake Halmashauri zingine wahakikishe kwamba vifaa tiba vinatengewa pesa na vinanunuliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na Halmashauri yake kwa sababu katika hizi pesa ambazo zimelipwa milioni 41 niliyotaja ni pamoja na kitanda cha upasuaji kimeshalipiwa, mashine ya kutolea dawa ya usingizi, jokofu la kuhifadhia damu kama ambavyo amesema Halmashauri zingine hazifanyi, wao wanafanya vizuri sana; mashine ya kufulia moja, vitanda vya kujifungulia vinne, mfumo wa hewa ya oxygen, vitanda vya kubebea wagonjwa. Kwa hiyo, kwa ujumla nizitake Halmashauri zingine zote nchini waige mfano mzuri ambao wenzetu wanafanya ambako Mheshimiwa Mbunge amesemea.

Name

John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa vifaa tiba kwenye Hospitali ya Wilaya ya Singida Mjini au kituo cha afya Sokoine?

Supplementary Question 2

MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Serikali iliahidi kupeleka fedha za kutosha kwa ajili ya ukarabati na kuviwezesha vituo vya afya karibu sehemu yote ya nchi. Mojawapo ni kituo cha afya cha Ulyankulu. Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kutupa status ya utumaji wa fedha hizo kwenye vituo vya afya kote nchini?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS – TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri wangu kwa ufafanuzi mzuri wa swali la awali. Hata hivyo, napenda kutoa status ya suala la ujenzi wa vituo vya afya ambavyo tumesema ni ukarabati mkubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulifanikiwa kupata fedha kutoka mifuko miwili. Fedha kutoka World Bank ambapo lengo letu ni kukarabati vituo vya afya 100, lakini nyingine tulipata fedha kutoka Ubalozi wa Canada tumeshazipeleka katika kila kituo takriban shilingi milioni 500. Hali ya ujenzi mpaka sasa, wengine wako katika stage ya lenta na wengine wanapauwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, fedha zilizotoka Mfuko wa World Bank, fedha zile zilichelewa kidogo ambapo ndani ya wiki hii fedha hizo ndio zitafika vituoni, japokuwa tulitoa deadline kwamba, tarehe 30 mwezi wa 12 vituo vyote viwe vimeweza kukamilika, kwa sababu hizi fedha kutoka Mfuko wa World Bank zilichelewa kufika vituoni tuta-extend huo muda angalau tufike mwishoni mwa mwezi Januari. Hali halisi hivi sasa fedha za Canada zimeshafika, lakini za World Bank ndiyo wiki hii zinafika vituoni. (Makofi)

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa vifaa tiba kwenye Hospitali ya Wilaya ya Singida Mjini au kituo cha afya Sokoine?

Supplementary Question 3

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kupata nafasi hii. Napenda tu kumuuliza Mheshimiwa Waziri ni lini Kituo cha Bunda Mjini kitapewa hadhi ya hospitali ya Wilaya?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS – TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la mchakato wa kupandisha kituo cha afya kuwa hospitali ni utaratibu. Mchakato huo unaanzia katika Halmashauri kwenye Baraza la Madiwani linafanya hivyo and then inaenda DCC, RCC, baadaye inafika kwa Waziri mwenye dhamana wa sekta ya afya; atakapoona kwamba kituo hiki kimekidhi na inafaa kufanya hivyo, basi atafanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani kama mchakato huo umeshaanza basi, jukumu hilo litakuwa chini ya Ofisi ya Waziri wa Afya, atakapoona kwamba vigezo vimekamilika na inabidi kufanya hivyo basi atafanya hivyo bila tatizo. (Makofi)