Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Primary Question

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA (K.n.y. MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE) aliuliza:- Maeneo ya Munguatosha na Hondogo ni baadhi ya maeneo ambayo yanahitaji transfoma ili umeme uwake. Je, Serikali ina mpango gani juu ya kupeleka transfoma katika maeneo hayo?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwepo na kilio kikubwa sana cha mahitaji ya umeme Kata ya Mkange pale Chalinze ukizingatia kuwa sehemu hii inachangia kwenye uchumi wetu wa Taifa hususan katika Wilaya ya Bagamoyo, pia na Halmashauri ya Chalinze na Tanzania kwa ujumla hususan katika viwanda pamoja na utalii.
Je, Serikali inajipangaje kusaidia wananchi pamoja na wawekezaji wa viwanda umeme ili kupunguza ukali wa maisha wa eneo hili la Kata ya Mkange? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi mkubwa wa Stiglers Gorge unadhamiria kuikomboa nchi yetu katika umeme hususan katika viwanda vinavyojengwa pamoja na treni hii ya umeme.
Je, Serikali inawaachaje wananchi wa Jimbo la Rufiji ambao wametunza bwawa hili pamoja na Mto Rufiji kwa miaka mingi sana hususan wakazi wa Kata ya Mwaseni, Kipugira, Ngorongo na Mkongwa? (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru kwa maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge Mchengerwa na naomba nimpongeze kwa jitihada zake za kufuatilia changamoto mbalimbali za nishati katika jimbo lake pamoja na muuliza swali la msingi. Ameuliza swali juu ya mahitaji ya umeme kwenye Kata ya Mkange iliyoko Jimbo la Chalinze na ni kweli Kata hii ya Mkange imepakana na Mbuga ya Saadani.
Naomba nimtaarifu kwamba katika mradi ambao unaendelea waUrban Peri Urban Edification Project of Coast Region na Kigamboni – Kata ya Mkange itapata umeme kupitia Miono. Kwa hiyo, naomba nimtaarifu kwamba Serikali imezingatia na kwa kuwa ina dhamira kwamba kila kijiji ifikapo 2020/2021 kipate umeme kwa hiyo Kata ya Mkange itapata umeme kupitia Miono.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ameulizia suala la Stiglers Gorge. Naomba nilitaarifu Bunge lako Tukufu ni kweli Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli imedhamiria kwa dhati kuongeza upatikanaji wa nishati nchini kwetu na imedhamiria kwa dhati kutekeleza mradi huu ambao utaongeza megawati 2100, tender imeshatangazwa na zaidi ya makampuni…
Mheshimiwa Mwenyekiti, na nimtaarifu tu Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa mradi huu unatekelezwa katika maeneo ya Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Pwani eneo la Rufiji Kata alizotaja Mwaseni na Ngorongo ni Kata ambazo ni kweli zimetunza bwawa hili na zitafaidika kwanza kupitia upatikanaji wa nishati hii ya umeme lakini pia kupitia ajira ambazo zitapatikana kipindi cha ujenzi wa bwawa hili, lakini tatu, Wilaya hii ya Rufiji imekuwa ikikumbwa na mafuriko ya mara kwa mara. Kupitia ujenzi wa bwawa hili ni dhahiri kwamba ule uhifadhi wa maji utasaidia kuzuia masuala ya mafuriko katika maeneo haya.
…lakini langu lingine pia ujenzi wa bwawa hili litasaidia shughuli za kilimo cha umwagiliaji kwa maeneo yale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba Watanzania muamini mradi huu unatekelezwa kwa pesa za ndani za nchi yetu. (Makofi/Vigelegele)