Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Kutokana na uvamizi wa ardhi katika maeneo ya mashule, masoko na zahanati. (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha upimaji wa maeneo hayo? (b) Je, kutokana na ukubwa wa gharama za upimaji, kwa nini zoezi la upimaji lisitolewe bure kwa taasisi za umma kupitia Halmashauri hizo?

Supplementary Question 1

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, Angelina mwenzangu, nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Swali la kwanza, kwa kuwa Mheshimiwa naibu Waziri amekiri kuwa wananchi wanavamia na kuyamega maeneo ya Serikali kinyume na utaratibu; na kwa kuwa ametoa rai wananchi waondoke maeneo hayo kabla sheria haijachukua mkondo wake, sasa isije ikawa kwa wananchi kilio, kwa watendaji vigelegele.
Je, Serikali ina kauli gani juu ya watendaji ambao wanalipwa mshahara kwa kazi ya upimaji na katika maeneo yao hawajafanya lolote hadi sasa?
Swali la pili, kwa kuwa katika majibu ya msingi, Mheshimiwa Naibu Waziri amesema gharama elekezi za huduma ya upimaji siyo kubwa kama inavyoonekana au inavyodhaniwa.
Je, kwa nini gharama hizo zisiwekwe wazi ili wananchi na taasisi nyingine wafahamu na kuzitambua na waweze kujipanga kwa ajili ya kulipia? Ahsante.(Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali la kwanza ameulizia habari ya adhabu kwa watendaji ambao wanafanya makosa na tunaadhibu pengine wananchi. Kama nilivyomjibu muulizaji wa swali namba 44 majukumu na uwajibishaji yako chini ya mamlaka husika hasa katika maeneo yetu kwenye Halmashauri za Wilaya. Kwa hiyo, haya yanapobainika basi tuyachukulie hatua papo hapo ili tusiweze kuwafanya wananchi waumie zaidi kwa makosa ya watendaji wetu.
Swali la pili, ametaka kuewekewa gharama za upimaji wazi. Naomba niseme tu tutazitoa na tutawagawia Waheshimiwa Wabunge wote, lakini kwa kifupi tu nikianza kuzungumzia habari ya miji kwenye Mamlaka za Miji na Manispaa katika gharama za upimaji kuanzia square meter moja mpaka square meter 400 gharama yake kwa maeneo ya residential ni shilingi 65 lakini maeneo ya commercial ni shilingi 350 kwa square meter, kwenye industrial ni shilingi 450 na kwenye maeneo ya social services ni shilingi 150. Kwa miji yetu ya kwaida kwenye township ni shilingi 200 kwa makazi, maeneo ya biashara ni shilingi 300, maeneo ya viwanda 350 na maeneo ya services ni shilingi 100. Vivyo hivyo kwenye trading center ni shilingi 100 kwa makazi, shilingi 200 kwa commercial, shilingi 200 tena kwa industrial na shilingi 100 kwa services. Kwa sababu mlolongo pia unategemeana na ukubwa wa kiwanja vina-range kuanzia shilingi 300,000 mpaka milioni 14 kutegemeana na ukubwa kuanzia hekari moja mpaka 10 ni shilingi milioni tatu, zinakwenda zinaongezeka kadri ya ukubwa, tutaziandaa na tutawasambazia Waheshimiwa Wabunge wote.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Kutokana na uvamizi wa ardhi katika maeneo ya mashule, masoko na zahanati. (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha upimaji wa maeneo hayo? (b) Je, kutokana na ukubwa wa gharama za upimaji, kwa nini zoezi la upimaji lisitolewe bure kwa taasisi za umma kupitia Halmashauri hizo?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, shamba la Mnazi Estate kule Lushoto - Mlalo limevamiwa kwa sababu Mmiliki ambae alikuwa anendelea kulimiliki ameshindwa kuliendesha. Je, pamoja na mchakato ambao tulikuwa tumeuanza wa kufuta, Serikali imefika hatua gani ya kumuondoa mmiliki katika ardhi hiyo?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwenye kijiji cha Mnazi kuna Kampuni inatiwa Lemash Enterprise ambayo ilikuwa inamiliki shamba la Mkonge lenye hekta 1,275 lakini nataka nimhakikishie Mheshimiwa Shangazi kutokana na jitihada zake za kuondoa kero ya wananchi na katika kutekeleza spirit ya Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli walitimiza wajibu wao na nataka kumhakikishia kwamba na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli naye ametimiza wajibu wake. Tarehe 4 Septemba, 2017 shamba hilo limefutwa rasmi na mmiliki ameshaambiwa, nimeshachukua hatua ya kulitangaza kwenye Gazeti la Serikali kwa order ya Rais na hivi sasa nimeshamwandikia Mkuu wa Mkoa wa Tanga ili atupe mapendekezo mazuri zaidi ya namna ya kulitumia shamba hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo nakuomba Mheshimiwa Shangazi kwa kuwa umelianza, basi naomba ushirikiane na Mkuu wa Mkoa wa Tanga kulimalizia mlete mapendekezo mazuri yatakayowezesha kutumika shamba hilo kuinua uchumi wa wananchi wa Mnazi. Tungependa shamba hili liendele kuwa shamba la Mkonge lakini ninyi watu wa Tanga muamue nani aendesha kilimo hicho kwa ajili ya kuongeza tija ya ajira na uchumi wa Taifa. (Makofi)

Name

Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Kutokana na uvamizi wa ardhi katika maeneo ya mashule, masoko na zahanati. (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha upimaji wa maeneo hayo? (b) Je, kutokana na ukubwa wa gharama za upimaji, kwa nini zoezi la upimaji lisitolewe bure kwa taasisi za umma kupitia Halmashauri hizo?

Supplementary Question 3

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Moshi vijijini kuna mashamba ambayo toka mwaka 1968 yalitaifishwa na kimsingi ni mashamba ya umma, lakini baada ya kutaifishwa na kupewa Vyama vya Ushirika yamekuwa yakigawanywa kwa taasisi mbalimbali kwa ajili ya shughuli za wananchi. Sasa hizo taasisi zikitaka kupima hayo mashamba sasa kulingana na shughuli ambazo zinafanyika inakuwa vigumu kwa sababu tayari kuna hati ambazo zilikuwepo toka wakati huo, ikiwa ni pamoja na eneo kama la Uru Seminari ambalo nilishalifikisha kwa Mheshimiwa Waziri.
Naomba kujua kutoka kwenye Serikalini ni lini Serikali itakwenda kufanya upimaji upya ili kutoa hati kulingana na matumizi ambayo yapo sasa hivi katika yale mashamba katika Kata zote hizo?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Mkoa wa Kilimanjaro na mashamba ya ushirika ni tatizo kweli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamna mashamba haya yalikuwa ni ya settlers, uamuzi wa Baba wa Taifa yalichukuliwa yakapewa Vyama vya Ushirika na mashamba haya ni mengi sana Mkoa wa Kilimanjaro ambayo yalimilikishwa Vyama vya Ushirika. Wizara yangu kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo nimeshamwandikia lakini tunazungumza nia njema zaidi ya kuhakiki upya mashamba yanayomilikiwa na Ushirika Mkoa wa Kilimanjaro hivi sasa. Ni kweli Vyama vya Ushirika zamani vilipewa, lakini leo matumizi yake ya vyama vya ushirika na ushirika wenyewe ni tofauti na madhumuni ya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote wa Mkoa wa Kilimanjaro maana hoja hii siyo ya Mheshimiwa Mbunge peke yake, Wabunge wote wa Kilimanjaro mashamba haya yanawahusu. Watuachie bado tuko kwenye mazungumzo na Wizara ya Kilimo ambaye ndiyo Msajili wa Vyama vya Ushirika ili tuone namna gani njema ya kuyahuisha mashamba yote ya ushirika ya Mkoa wa Kilimanjaro ili yawe na tija kwa wananchi wote kulingana na mazingira ya sasa. (Makofi)

Name

Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:- Kutokana na uvamizi wa ardhi katika maeneo ya mashule, masoko na zahanati. (a) Je, ni lini Serikali itakamilisha upimaji wa maeneo hayo? (b) Je, kutokana na ukubwa wa gharama za upimaji, kwa nini zoezi la upimaji lisitolewe bure kwa taasisi za umma kupitia Halmashauri hizo?

Supplementary Question 4

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jiji letu la Tanga kuna upimaji unaoendelea katika eneo la Amboni kwa ajili ya kuongeza Kiwanda cha Saruji cha Sinoma cha Wachina. Katika maeneo yale kuna tatizo kubwa la kwamba, wananchi wenye mashamba yao wanaambiwa watalipwa fidia ya mazao ya muda mrefu tu na mazao ya muda mfupi kama mahindi, mihogo na mengineyo hayatalipwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali inalifahamu hilo na utaratibu huu ni utaratibu wa sheria gani inayotumika kulipa mazao ya muda mrefu, na pia pana maji koto au sulphur water pale katika eneo la Amboni ambayo ni kama tunu kwa mambo ya utalii.
Je, Serikali inafanya juhudi gani kuhakikisha ile sulphur bath itaendelea kuwepo ambayo iliendelezwa na Galanos lakini pia na wananchi wenye mzao mafupi nao watalipwa fidia yao?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili ni la Tanga. Walioamua kufanya haya ni Halmashauri ya Jiji la Tanga kwenye shamba hili. ningemuomba Mheshimiwa Mbunge kwa sababu kazi hii hata tathmini ya pale imesimamiwa na kufanywa na Wathamini waliopo kwenye Jiji la Tanga na upitishaji wa viwango huu ulikuwa shirikishi na maelekezo haya yametolewa pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba, unajua ni rahisi kufikiri kwamba Waziri akiwa hapa Dodoma anaweza akajua na akalitolea ufafanuzi kila jambo lakini jambo hili ni shirikishi limefanywa na Watendaji wenye Mamlaka ya Kisheria ya kutenda wa Jiji la Tanga kwahiyo kama halikufanyika vizuri, wale wananchi wanajua Bungeni hapa mwaka huu mmetunga Sheria ya Bodi ya Mfuko wa Fidia. Ninawaomba waisome, Waheshimiwa Wabunge muwasidie wananchi hawa wakate rufaa kwenye Bodi ya Mfuko wa Fidia ili iweze kufikiaria vinginevyo, lakini mimi kama aziri hapa siwezi kusimama nikatengua uamuzi halali uliofanywa na Halmashauri ya Jiji la Tanga. Hivyo, naomba wafuate hiyo sheria. (Makofi)