Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:- Msongamano wa magari, ujenzi holela, miundombinu duni ya maji taka na kadhalika katika miji mikubwa hapa nchini vinatokana na udhaifu wa upangaji wa matumizi bora ya ardhi (poor land use planning). Je, Serikali imejiandaa vipi kuendesha zoezi la Mipango Miji na matumizi bora ya ardhi katika miji mipya ikiwemo Halmashauri ya Mji wa Njombe?

Supplementary Question 1

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, wananchi wapatao 200 wa Makambako Kata ya Kivavi, Mtaa wa Mashujaa waliondolewa katika maeneo yao mwaka1997 bila kupewa fidia, kwa ajili ya kupisha ujenzi wa soko la kimataifa, wamefuatilia wananchi hawa lakini hadi leo hakuna majibu. Pia kuna wananchi wa Idofi waliondolewa maeneo yao kwa ajili ya kupisha ujenzi wa mizani hadi leo hawajapata fidia.
Je, Serikali inampanga gani wa kuwalipa wananchi hawa fidia zao?
Swali la pili, kwa kuwa kila Halmashauri kuna Maafisa Mipango Miji. Je, ni kwa nini wananchi wanajenga sehemu zisizo sahihi na Serikali inawaangalia tu mwisho wa siku wanaanza bomoa bomoa? Naomba kupata majibu (Makofi).

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na sehemu yake ya kwanza wananchi 200 wa Makambako na wale wa Kidozi kwamba walipisha miradi ya Serikali na mpaka leo hawajalipwa fidia. Naomba nimhakikishie tu Mheshimiwa Mlowe kwamba mara pesa zitapopatikana watalipwa, kwa sababu Serikali inatambua kwamba ililitwaa lile eneo kwa ajili ya matumizi ya Serikali, kwa hiyo, asiwe na wasiwasi pesa ikipatikana watalipwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili anaongelea habari ya maafisa kwamba watu wanajenga ovyo na wanaangalia na hakuna hatua zinazochukuliwa baadae wanakuja kuwabomolea. Naomba nitoe rai tu kwa sababu pia ni sehemu ya Halmashauri na tunakaa katika vikao vyetu vya Halmashauri kwa maana ya Baraza la Madiwani, haya yanapotokea ni wajibu wetu pia kutoa maonyo kwa wale ambao wamepewa wajibu huo wa kufanya kazi lakini hawasimamii sawasawa. Kwa hiyo, namuomba Mheshimiwa Mbunge atakapokuwa amekaa katika Baraza lake la Madiwani wajaribu kuwakumbusha hasa wale watendaji ambao hawatimizi wajibu wao vizuri.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE aliuliza:- Msongamano wa magari, ujenzi holela, miundombinu duni ya maji taka na kadhalika katika miji mikubwa hapa nchini vinatokana na udhaifu wa upangaji wa matumizi bora ya ardhi (poor land use planning). Je, Serikali imejiandaa vipi kuendesha zoezi la Mipango Miji na matumizi bora ya ardhi katika miji mipya ikiwemo Halmashauri ya Mji wa Njombe?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali dogo la nyongeza.
Pamoja na kazi nzuri na jitihada za Serikali katika kuhakikisha miji inapangwa na zoezi zima la urasimishaji wa makazi ikiwemo upimaji shirikishi, naomba tu kujua Serikali inayo mkakati gani kuhakikisha kwamba pamoja na upimaji huu unaofanyika sasa ile gharama ya premium inaonekana kuwa mzigo mkubwa kwa wananchi na matokeo yake wanashindwa kufikia hatua ya kupewa hati miliki, hivyo inawapelekea kubaki katika maeneo ambayo yamepimwa bila hati hizo.
Je, ni nini mkakati wa Serikali kuondoa kabisa hizi asilimia 2.5 zilizopunguzwa japo ilikuwa Saba ikapunguzwa, nini mkakati wa Serikali kuondoa hizi lakini kuongeza muda wa upimaji shirikishi ili wananchi wengi zaidi waweze kupimiwa kuhakikisha maeneo yao yote yamekamilika? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia Bunge hili Tukufu kwanza naomba nimshukuru Mheshimiwa Mabula kwa sababu jana pia wakati anachangia Mpango wa Maendeleo amezungumzia suala la kuwajali sana wananchi na hasa katika suala zima la urasimishaji na mpango unaoendelea. Ametupa changamoto kama Wizara na sisi tunamshukuru na tumeona iko haja kweli ya kuangalia hawa wananchi ambao walitumia nguvu zao kujenga katika maeneo ambayo pengine hatukuwa makini katika kuwahi kupanga na wao wakavamia, basi tumesema kwa sababu hoja ni kupunguziwa mzigo, tumelichukua suala lake kuondoa premium na kabla ya mwisho wa mwezi huu tutakuwa tumempa jibu.
Je, ni lini zoezi hili litaendelea, naomba nimfahamishe Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa maeneo yale ambayo yanarasimishwa na yamekwishaanza kwa mwaka huu tutavumilia mpaka mwisho wa mwaka huu wa fedha. Baada ya mwaka wa fedha tuna imani na mipango miji katika maeneo hayo, mipango kabambe katika maeneo hayo itakuwa tayari kwahiyo ukomo wao itakuwa ni mwisho wa mwaka wa fedha mwaka huu 2017/2018.