Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza:- Mkoa wa Kigoma umebarikiwa kuwa na Ziwa Tanganyika, Mto Malagarasi na vyanzo vingine vya maji lakini Mkoa huu unakabiliwa na changamoto kubwa ya maji. Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Kigoma hususan katika Jimbo la Kigoma Kaskazini katika kuhakikisha wanapata maji ya kudumu ya kwenye mabomba?

Supplementary Question 1

MHE. MUNDE A. TAMBWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa swali la msingi linafanana kabisa na matatizo yaliyopo katika Wilaya ya Urambo na Kaliua na Serikali imekuwa ikituambia kwamba imekamilisha mchakato wote wa kutoa maji Mto Malagarasi kupeleka Kaliua na Urambo, fedha tu ndiyo bado hazijapatikana toka mwaka jana walituambia fedha hizo zitapatikana.
Je, status ya kupata pesa kupeleka maji katika Wilaya ya Urambo na Kaliua ikoje mpaka sasa kwa sababu hali ni mbaya sana kwa wananchi hao? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunao mradi wa usanifu unakamilika wa kutoa maji Malagarasi kupitia Kaliua kuja Urambo hadi Tabora, pia Mheshimiwa Rais ametuagiza kwamba huu mradi unaotoa maji Solwa kutoka Ziwa Victoria kupeleka Tabora wakati unaendelea tayari tumeshaagiza Mamlaka yetu ya Maji ya Tabora iangalie uwezekano wa kuweka mabomba mengine kutoka matanki ya Tabora kupeleka Urambo na ikiwezekana yafike mpaka Kaliua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuhakikishie Mheshimiwa Munde kwamba Serikali inafanya kazi kuhakikisha Kaliua na Urambo wanapata maji safi na salama. (Makofi).

Name

Kiza Hussein Mayeye

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza:- Mkoa wa Kigoma umebarikiwa kuwa na Ziwa Tanganyika, Mto Malagarasi na vyanzo vingine vya maji lakini Mkoa huu unakabiliwa na changamoto kubwa ya maji. Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Kigoma hususan katika Jimbo la Kigoma Kaskazini katika kuhakikisha wanapata maji ya kudumu ya kwenye mabomba?

Supplementary Question 2

MHE. KIZA H. MAYEYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri maswali ya nyongeza kama ifuatavyo:-
(a) Je, ni lini sasa Serikali mtatimiza ahadi yenu na kutekeleza mradi huu wa Maji katika Mji ya Manispaa ya Kigoma Mjini kufika katika Mji Mdogo wa Mwandiga?
(b) Serikali haioni sasa ni muda muafaka maji haya ya Ziwa Tanganyika kwenda katika Wilaya ya Kasulu? Ahsante. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa maswali yake mazuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upatikanaji wa maji kwa Mji wa Mwandiga unategemeana kabisa na utekelezaji wa mradi huu mkubwa ambao utakamilika mwezi huu Disemba. Mradi huu utazalisha lita milioni 42 na mahitaji ya Mji wa Kigoma ni lita milioni 20. Kwa hiyo, kutakuwa na maji ya kiasi kikubwa ambayo tutaweza kuyapeleka katika Mji wa Mwandiga. Kikubwa nataka niwahakikishie wananchi wa Mwandiga subira yavuta kheri na kheri itapatikana katika upatikanaji wa maji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la pili kuhusu suala la upatikanaji wa maji katika Mji wa Kasulu nataka nimhakikishie ndugu yangu Mheshimiwa Mbunge wali wa kushiba unaonekana kwenye sahani. Serikali imefanya kazi kubwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu mkubwa wa maji, sasa hivi Mji wa Kasulu upo miongoni mwa miji 17 ambayo kupitia fedha za India utapata maji. Kikubwa tumsubiri Mhandisi Mshauri atatushauri vipi ili tupate maji ili kuhakikisha kwamba wananchi wa Kasulu wanapata maji kwa wakati. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza:- Mkoa wa Kigoma umebarikiwa kuwa na Ziwa Tanganyika, Mto Malagarasi na vyanzo vingine vya maji lakini Mkoa huu unakabiliwa na changamoto kubwa ya maji. Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Kigoma hususan katika Jimbo la Kigoma Kaskazini katika kuhakikisha wanapata maji ya kudumu ya kwenye mabomba?

Supplementary Question 3

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya upatikanaji wa maji katika Mikoa ya Lindi na Mtwara bado ni mbaya sana na aliyekuwa Naibu Waziri wa Maji ambaye sasa ni Waziri wa Maji alipotembelea Mikoa ya Lindi na Mtwara alikagua baadhi ya miradi ambayo inaendelea katika Jimbo la Mtama, Mradi wa Maji wa Nyangamara na pengine hakufika lakini Mradi wa Maji wa Namangale na alituhaidi kwamba certificates za miradi hiyo zikifika Wizarani mara moja pesa zitalipwa, mpaka sasa huu ni mwezi wa pili au wa tatu certificates hizo zimefika Wizarani na hazijalipwa.
Je, ni lini Serikali italipa pesa hizi za hawa wakandarasi ili miradi hii ipate kukamilika wananchi wangu wapate maji?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Fedha na Mipango jana ametupatia shilingi bilioni 12. Kwa hiyo, nikuhakikishie kwamba hizo certificates kama zimeshaletwa wiki ijao tutahakikisha tumezilipa ili mkandarasi aendelee kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza:- Mkoa wa Kigoma umebarikiwa kuwa na Ziwa Tanganyika, Mto Malagarasi na vyanzo vingine vya maji lakini Mkoa huu unakabiliwa na changamoto kubwa ya maji. Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Kigoma hususan katika Jimbo la Kigoma Kaskazini katika kuhakikisha wanapata maji ya kudumu ya kwenye mabomba?

Supplementary Question 4

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya maji nchini kwa ujumla siyo nzuri na lengo Namba 6 la ajenda ya 2020/2030 ni maji, upatikanaji wa maji safi, salama kwa wote duniani na Tanzania ni mwanachama. Katika Jimbo la Vunjo sehemu za kata….
Mheshimiwa Mwenyekiti, sawa. Katika Kata ya Mwamba Kusini na Mwika Kusini hali ya maji ni mbaya sana na wananchi wananunua maji ndoo moja kwa shilingi 500.
Je, Serikali inachukuliaje jambo hili kwa dharura ili upatikanaji wa maji uweze kupatikana kwa haraka?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya upatikanaji wa maji nchi ni nzuri kupitia programu ya maendeleo ya sekta ya maji awamu ya kwanza. Tulilenga kutekeleza miradi 1,810, tayari tumeshatekeleza miradi 1,433, tumejenga vituo vya kuchotea maji 117,000 na vituo vyote vingetoa maji vijijini sasa hivi tungekuwa na asilimia 79 ya upatikanaji wa maji safi na salama. Kutokana na mabadiliko kidogo ya tabianchi vyanzo vingi vya maji kukauka sasa hivi hiyo asilimia kidogo imeshuka, lakini tayari tumejipanga kuhakikisha maeneo yote ambayo hayatoi maji tumetenga fedha kwenye bajeti ya mwaka huu tulionao ili hayo maeneo yaweze kupatiwa vyanzo vingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la Vunjo Mheshimiwa Mbunge naomba tukutane, tujadili ili tuone ni namna gani tutatoa kitu cha dharura kuhakikisha wale wananchi wanapata maji.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza:- Mkoa wa Kigoma umebarikiwa kuwa na Ziwa Tanganyika, Mto Malagarasi na vyanzo vingine vya maji lakini Mkoa huu unakabiliwa na changamoto kubwa ya maji. Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Kigoma hususan katika Jimbo la Kigoma Kaskazini katika kuhakikisha wanapata maji ya kudumu ya kwenye mabomba?

Supplementary Question 5

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kutokamilika kwa miradi ya maji katika Halmashauri zetu kumekuwa ni tatizo sugu, niliwahi kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri wakati huo ambaye sasa ndiyo Waziri alisema pesa Wizarani zipo ila watu wapeleke certificate. Ninasikitika kumwambia kwamba hapa ninayo makabrashi ambayo ni copy ya hizo certificate ambazo zimeshafika kwenye Wizara yake sasa ni zaidi ya mwaka mzima hizo pesa hazijawahi kutolewa, na kuna miradi kadhaa katika vijiji vya Kipule, Ngongowele pamoja na Mikunya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kauli ya Serikali ni lini miradi hii itakamilika ili wananchi wa vijiji hivi waweze kupata maji. (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, kwa sababu certificate, ni masula ya kiutendaji Mheshimiwa Mbunge, ninaomba baada ya Bunge hili leo tukutane, twende kwa watendaji tukaangalie certificate kama zipo, kama nilivyosema kwamba tayari nina fedha ili wiki ijayo tuweze kulipa.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza:- Mkoa wa Kigoma umebarikiwa kuwa na Ziwa Tanganyika, Mto Malagarasi na vyanzo vingine vya maji lakini Mkoa huu unakabiliwa na changamoto kubwa ya maji. Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Kigoma hususan katika Jimbo la Kigoma Kaskazini katika kuhakikisha wanapata maji ya kudumu ya kwenye mabomba?

Supplementary Question 6

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa niweze kuuliza swali dogo la nyongeza Wilaya ya Lushoto ina vyanzo vingi sana vya maji lakini wananchi wa Lushoto hawana maji safi na salama.
Je, Serikali ina mpango gani wa kumtua mama ndoo kichwani hasa akina mama wa Makanya, Kilole, Kwekanga, Kwemakame, Ngulwi, Ubiri, Handeni na Miegeo? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitembelea Lushoto nikakuta hilo tatizo na nikamuelekeza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Tanga aweze kutekeleza miradi ya maji katika Halmashauri yake, hadi jana nimepiga simu tayari wamekamilisha taratibu za manunuzi, Baada ya siku 14 mikataba itasainiwa, utekelezaji uanze.
Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie kwamba maeneo yote ya Halmashauri yako yatapata maji.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. KIZA H. MAYEYE aliuliza:- Mkoa wa Kigoma umebarikiwa kuwa na Ziwa Tanganyika, Mto Malagarasi na vyanzo vingine vya maji lakini Mkoa huu unakabiliwa na changamoto kubwa ya maji. Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Kigoma hususan katika Jimbo la Kigoma Kaskazini katika kuhakikisha wanapata maji ya kudumu ya kwenye mabomba?

Supplementary Question 7

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Mafinga ni kati ya miji inayokuwa kwa kasi sana hapa nchi na hivyo uhitaji wa maji umekuwa ukiongezeka kwa kasi. Kutokana na jitihada mbalimbali ambazo wananchi wa Mafinga wanajituma na uwekezaji katika mazo ya misitu.
Je, Serikali, iko tayari lini kutupa kibali kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa miradi ya mwaka huu wa fedha wa 2017/2018?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana, lakini nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, kaka yangu Mheshimiwa Cosato Chumi kwa kazi kubwa anazozifanya na namna anavyofuatatilia ili wananchi wake wapate maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka sasa Wizara imeshatoa kibali kwa mradi wa Mji wa Bumilianga ili kuhakikisha kwamba wananchi wanapata maji. Ahsante sana. (Makofi)