Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Ili kuleta mapinduzi ya kweli ya kilimo, ujuzi na maarifa ya wataalam wa kilimo unatakiwa uwafikie wakulima mara kwa mara. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa kibali cha kuajiri Maafisa Ugani wa kutosha na kuwapeleka kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba sasa niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa upungufu huo wa Maafisa Ugani ni mkubwa sana kwenye Halmashauri ambazo zimeanzishwa hivi karibuni, kama Halmashauri ya Mji wa Nanyamba; je, Serikali ina mpango gani wa upendeleo kwa mamlaka hizi mpya za Serikali za Mitaa ambazo zimeanzishwa hivi karibuni?
Swali langu la pili, ukiangalia takwimu za ajira zilizotolewa hivi karibuni kwa Maafisa Ugani, na kwa kuwa nchi yetu ina takribani vijiji zaidi ya 12,000 utaona kwamba kuna vijiji vingi sana vinakosa Maafisa Ugani.
Je, Serikali ina mpango gani au mkakati gani wa haraka wa kuhakikisha kwamba kila kijiji katika nchi yetu kinakuwa na Afisa Ugani ili kuleta mapinduzi ya kweli katika kilimo?

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Utumishi inatambua kwamba Mamlaka mpya za Serikali za Mitaa zilizoanzishwa zinahitaji upendeleo mpya, hasa katika kupanga watumishi. Nataka nimuahidi kwamba siyo Nanyamba tu, Nanyamba ni Mamlaka mpya ya Serikali za Serikali za Mitaa, Halmashauri ya Mji wa Newala ni mpya, Halmashauri ya Mji wa Tarime ni mpya, Halmashauri ya Mafinga ni mpya, maeneo yale yote ambayo tumeanzisha Halmashauri mpya najua wakati wa kugawana watumishi zile mamlaka mpya hazikupata watumishi wengi. Kwa hiyo, nitakachofanya ni kuhakikisha zile mamlaka mpya zote zinapata watumishi wa kutosha ili zilingane, kama ni upungufu ulingane na zile mamlaka zilizokuwepo kabla.
Swali lake la pili, ni kweli kwamba vijiji vingi havina hawa Maafisa Ugani, hili limetokea kwa sababu muda mrefu katika nchi yetu, vile vyuo vinavyofundisha vyeti vya kilimo vilikuwa vimesimama, lakini baadae vimefufuliwa, sasa hivi kazi kubwa inaendelea. Nataka nimhakikishie kwamba tutaanzisha programu maalum kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo kuhakikisha kwamba vyuo vile wanachukua wanafunzi wengi zaidi ili wanapomaliza waweze kuajiriwa na Serikali katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. (Makofi)

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Ili kuleta mapinduzi ya kweli ya kilimo, ujuzi na maarifa ya wataalam wa kilimo unatakiwa uwafikie wakulima mara kwa mara. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa kibali cha kuajiri Maafisa Ugani wa kutosha na kuwapeleka kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa?

Supplementary Question 2

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na umuhimu wa watumishi katika kada hii ya Maafisa Ugani kama kweli tunataka kuleta mapinduzi ya kilimo kwenye nchi yetu. Jambo ambalo tunaliona sasa hivi ni kwamba kutokana na kutokuajiriwa kwa Watendaji wa Vijiji na Watendaji wa Kata wa kutosha, baadhi ya watumishi katika kada hii ya kilimo sasa ndiyo wamekaimishwa zile ofisi za Kata kwa maana ya kuwa Watendaji wa Vijiji na Watendaji wa Kata.
Je, ni lini Serikali itaajiri watumishi katika kada hiyo ya utendaji ili watumishi hawa muhimu wa eneo la kilimo warudi kufanya kazi ya kilimo na wananchi? (Makofi)

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli pale mahali ambapo Maafisa Watendaji wa Kata hawapo, Maafisa Ugani wamekaimishwa nafasi hizo, hii imetokana na upungufu wa kutotosheleza Watendaji wa Kata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilieleze Bunge lako Tukufu, kazi moja wapo ya Afisa Mtendaji wa Kata ni kusukuma maendeleo ndani ya kata, watu waliofanya vizuri sana katika shughuli hii ni Walimu, Maafisa Kilimo, Mabibi Maendeleo, kwa hiyo pale ambapo Afisa Kilimo anakaimishwa Kata siyo makosa, ni nafasi nzuri ya kumuangalia keshokutwa huenda akawekwa moja kwa moja. Jambo la msingi hapa ni kwamba Wizara yangu inakubali kwamba kuna haja ya kulifanyia kazi suala hili kuhakikisha kwamba Kata zetu zote na vijiji vyetu vinakuwa na Maafisa Watendaji wa kudumu. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Ili kuleta mapinduzi ya kweli ya kilimo, ujuzi na maarifa ya wataalam wa kilimo unatakiwa uwafikie wakulima mara kwa mara. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa kibali cha kuajiri Maafisa Ugani wa kutosha na kuwapeleka kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa?

Supplementary Question 3

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo tu la nyongeza.
Kwa kuwa uhaba wa Maafisa Ugani uko sawasawa kabisa na uhaba wa wataalam wa mifugo. Je, Serikali ina mpango gani wa kuajiri Maafisa Mifugo wa kutosha ili wananchi wasaidiwe haki katika Halmashauri zetu?

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itashughulikia tatizo la uhaba wa Maafisa Ugani sambamba na tatizo la Maafisa wa Mifugo.

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Ili kuleta mapinduzi ya kweli ya kilimo, ujuzi na maarifa ya wataalam wa kilimo unatakiwa uwafikie wakulima mara kwa mara. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa kibali cha kuajiri Maafisa Ugani wa kutosha na kuwapeleka kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa?

Supplementary Question 4

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami napenda kuuliza swali la nyongeza kwa kaka yangu, Mheshimiwa Kapteni Mkuchika kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la watumishi katika sekta ya kilimo ni sawasawa sana au zaidi ya katika sekta ya afya. Sasa hivi maeneo mengi, hasa vijijini, kuna upungufu mkubwa sana wa watumishi katika sekta ya afya.
Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kuajiri watumishi wa sekta ya afya ili kunusuru maisha ya Watanzania, hasa akina mama na watoto? (Makofi)

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba maeneo muhimu ambayo wananchi wanategemea kupata huduma ni upande wa afya, maji, hayo ni mambo yanayogusa maisha ya kila siku pamoja na elimu na barabara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka yote Serikali inapoajiri imekuwa ikiweka umuhimu mkubwa sana upande wa watumishi wa afya, kwa sababu Waziri wa Utumishi anaajiri hawa Maafisa Afya baada ya kuwa tayari wameshafunzwa na kuhitimimu, nataka niliahidi Bunge lako Tukufu kwamba nitazungumza na Waziri mwenzangu wa Elimu na Wizara ya Afya wapate mafunzo watumishi wengi zaidi katika fani ya afya ili wakazibe mapengo haya yaliyopo katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa.

Name

Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Ili kuleta mapinduzi ya kweli ya kilimo, ujuzi na maarifa ya wataalam wa kilimo unatakiwa uwafikie wakulima mara kwa mara. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa kibali cha kuajiri Maafisa Ugani wa kutosha na kuwapeleka kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa?

Supplementary Question 5

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Pamoja na kwamba wananchi wana haki ya kupata huduma ya watumishi, hasa walimu, wauguzi na watendaji wa vijiji na kata, pia jitihada nzuri ya Serikali inayoifanya ya kupeleka fedha za maendeleo vijijini inahitaji watumishi hawa waweze kusimamia miradi hii. Kwa upande wa Karagwe kuna shortage kubwa ya Walimu wasiopungua 850, kuna shortage kubwa ya wauguzi.
Je, nini tamko la Serikali, maana kila mwaka wa fedha Serikali inasema itapanga bajeti ya kutosha kwa ajili ya kuhakikisha tunakuwa na watumishi wa kutosha. Nini tamko la Serikali kuhusu hii shortage ya watumishi ya sasa hususan Wilaya ya Karagwe? Ahsante. (Makofi)

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa walimu na matabibu na wataalam wa idara ya afya na imekuwa ikichukua hatua kuona kwamba tunaziba mapengo haya. Kama mtakumbuka Waheshimiwa Wabunge, wakati tunaanza sekondari zetu za kata uhaba wa walimu ulikuwa mkubwa sana, lakini Serikali kwa kutambua umuhimu wa kuwepo walimu wa kutosha imefanya jitihada ya kuajiri walimu wengi na hivi sasa katika shule zetu za sekondari, hali ya walimu imekuwa nafuu ukiondoa labda mapungufu makubwa yaliyopo katika upande wa walimu wa masomo ya sayansi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni kazi ya kudumu ninamuahidi tu kwamba Serikali itaendelea na kasi ileile ya kuajiri watumishi wa afya na elimu ili wananchi wetu wapate huduma ya afya bora, ili watoto wetu wapate elimu inayojitosheleza. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Ili kuleta mapinduzi ya kweli ya kilimo, ujuzi na maarifa ya wataalam wa kilimo unatakiwa uwafikie wakulima mara kwa mara. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa kibali cha kuajiri Maafisa Ugani wa kutosha na kuwapeleka kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa?

Supplementary Question 6

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nimpongeze Waziri kwa kuteuliwa kwake pamoja na Mawaziri wengine wote.
Katika mwaka wa fedha wa 2016/2017, Serikali ilikuwa na nia njema ya kuajiri watumishi 52,000; je, Serikali sasa itatekeleza mpango ule wakati gani ili vijana wetu waliopo mitaani waweze kupata nafasi ya ajira?

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba baada ya mchujo wa watumishi hewa, Mheshimiwa Rais ametoa idhini, Serikali imeidhinisha waajiriwe watumishi wapya 15,000, hilo zoezi linafanyika. Pia katika mwaka huu wa fedha kuna kibali cha kuajiri watumishi 52,000, zoezi hilo litaendelea, nataka nihakikishe kwamba nafasi na fedha za kuwalipa zipo, kazi hiyo itatekelezwa. (Makofi)