Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jamal Kassim Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Primary Question

MHE. JAMAL KASSIM ALI aliuliza:- Je, ni utaratibu gani unaotumika kukokotoa kodi katika forodha zetu zinazopokea bidhaa na vitu mbalimbali vinavyotokea Zanzibar, wakati vitu vilevile vinavyozalishwa Zanzibar ni vilevile vinavyotoka nje ya nchi?

Supplementary Question 1

MHE. JAMAL KASSIM ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza:
(a) Kwa vile Naibu Waziri ameeleza kwamba kuna database maalum ambayo TRA wanayo na kule Zanzibar inatumika, je, huu mfumo una tatizo gani, kwa sababu mizigo yote ambayo inapitia Zanzibar kuja Bara asilimia 100 ya mizigo ile inatozwa kodi inapoingia Tanzania Bara, wakati sheria inayotumika ni hiyo moja, na mamlaka ambayo inasimamia kodi na Kamishna ni huyo huyo mmoja?
(b) Mheshimiwa Naibu Waziri, alieleza katika jibu lake kwamba endapo vitu vinatoka Zanzibar kuja Bara wanaagalia tozo la awali ambalo lilitozwa Zanzibar na kuangalia ile tofauti ambayo kwa mujibu wa database zao wanam-charge yule mtu. Sasa je, kwa mtu ambaye ana tv moja anapopita bandarini pale kutokea Zanzibar hana entry…
NAIBU SPIKA: Naomba uulize swali Mheshimiwa Jamal,
MHE. JAMAL KASSIM ALI: Ahsante Mheshimiwa NAibu Spika, je, mtu ambaye kwa vitu ambavyo ni item moja moja kama tvna redio anapotoka Zanzibar kuja Bara wanatumia mfumo gani wa kukokotoa hiyo kodi?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEHDA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kodi inazotozwa kwa bidhaa zinazotika Zanzibar kuja huku kwetu, kwanza naomba nisahihishe, mfumo huu wa Import Export Commodity Database unaotumika Tanzania Bara kule Zanzibar hautumiki. Ndiyo maana inaonekana kule ambako hawatumii mfumo huu, bidhaa kule tathmini inapofanyika mara nyingi huonekana ipo chini ya thamani ya kiwango ambacho kinatakiwa kulipiwa kodi inapokuja Tanzania Bara.
Hivyo ndiyo maana bidhaa zinazotoka Zanzibar kuja huku zinatozwa tena kodi. Siyo kodi mara mbili lakini ni kuangalia utofauti wa kodi wa thamani, zilizothaminiwa kutoka Zanzibar na ambazo zimethaminiwa huku Tanzania Bara. Hivyo, tunaomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar waweze kufanya haraka kujiunga na mfumo huu, ili kwa pamoja hili tatizo wanalopata wafanyabiashara wetu wasiweze kulipata.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu bidhaa hiyo moja moja, mfumo ni huohuo mmoja, inapofika kama haikuzalishwa Zanzibar, inapofika Forodhani inatakiwa ichajiwe utofauti ule wa kodi ambao utaonekana ilichajiwa Zanzibar na huku Tanzania Bara. Ahsante.