Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara ya kilometa 40 ya kutoka Nyololo - Igowole - Mtwango kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini hii barabara ina miaka minne sasa tangu upembuzi yakinifu kukamilika. Naibu Waziri wa Ujenzi aliyepita aliwahi kuja kule akaongea na wananchi akasema kwamba ujenzi wa kiwango cha lami utaanza mara moja. Naibu Waziri naomba awaambie wananchi ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kwa sababu upembuzi yakinifu ulishakamilika? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi wa kijiji cha Nyololo, Nziwi, Igowole, Mninga, Kibao, Lufuna na Mtwango waliwekewa alama ya ‘X’ kwenye nyumba zao na Serikali iliahidi kwamba alama ya ‘X’ ambayo ni ya kijani watapewa fidia. Wananchi wameshindwa kuendeleza nyumba za biashara kwa sababu zimewekewa alama ya ‘X’. Ni lini Serikali italipa fidia wananchi wale ambao wanasubiria mpaka leo? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi barabara hii tutaanza kuijenga mara tutakapoanza kupata fedha. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Kigola kwamba Serikali itatumia kila aina ya nguvu zake kuhakikisha kwamba inapata fedha na kutekeleza ahadi au dhamira ambayo Naibu Waziri aliyepita aliionyesha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ni kwamba ni kweli wote waliowekewa alama ya ‘X’ za kijani watalipwa fidia na zitalipwa tutakapopata hizi fedha za ujenzi. Ulipaji wa fidia unaenda sambasamba na ujenzi wa barabara husika. Kwa hiyo, fedha hizi tunazozitafuta tunazitafuta zote, za ujenzi na za kulipa fidia.

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara ya kilometa 40 ya kutoka Nyololo - Igowole - Mtwango kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa barabara ya Kichangani - Tubuyu katika Manispaa ya Morogoro ambayo ina urefu wa kilometa nne imejengwa kwa kilometa moja kwa shilingi bilioni tatu yaani kilometa nne imejengwa kwa shilingi bilioni 12. Je, Serikali iko tayari kupeleka wataalam kwenda kubaini ubadhirifu wa ujenzi wa barabara hii ambayo imejengwa kwa Mfuko wa Benki ya Dunia? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepata concern hii kutoka kwa Wabunge hasa wa Mkoa wa Morogoro na hasa barabara hizi zinazojengwa under Strategic Cities Project pamoja na barabara zingine ambazo zinajengwa katika Manispaa. Bahati nzuri kwa taarifa za Morogoro tunazifanyia kazi, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaenda kufanya verification kuangalia value for money katika eneo lile lakini zoezi hilo tutalifanya maeneo mbalimbali ikiwemo katika Mji wa Hai, Mkoa wa Kilimanjaro. Lengo letu ni kwamba thamani ya fedha ipatikane ili wananchi waweze kupata huduma inayolingana na thamani ya fedha. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge kilio chake kimesikika tutaenda kulifanyia kazi eneo hili.

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara ya kilometa 40 ya kutoka Nyololo - Igowole - Mtwango kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naiomba Serikali itoe tamko hapa kuwaeleza wananchi wa Ilongelo, Mdida, Singa, Mtinko, Nkungi hadi Haydom kwa ahadi yao waliyoahidiwa na Rais wa Awamu ya Nne kwamba barabara ya lami itajengwa kutoka Singida kupita maeneo hayo hadi Haydom lakini sasa hivi hakuna kinachoendelea. Naomba Serikali iwaambie wananchi hao. Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Martha Mlata, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Singida na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa huo, kama ifuatavyo:- (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba juhudi zake za kufuatilia ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami hatimaye zitazaa matunda kwa sababu ahadi ambayo ilitolewa na Rais wa Awamu ya Nne tunayo na nimhakikishie kwamba ahadi hiyo tutaitekeleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaenda kutekeleza ahadi hizi awamu kwa awamu kama ambavyo nimekuwa nikimueleza yeye pamoja na Wabunge wenzake wanaofuatilia sana barabara hii, barabara hii inaunganisha Wabunge wengi sana.