Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Kadi za kulipia Ngorongoro zimekuwa kero kwa wageni na wahudumu kwani muda mwingi umekuwa ukipotea wakati kufanya malipo. Je, ni lini Serikali itafanya marekebisho ili kuwe na mfumo wa kadi kama za TANAPA?

Supplementary Question 1

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri baada ya kero hiyo kurekebishwa lakini bado driver guides wanapofika pale getini wanatakiwa kuandikisha majina ya wageni ambao wanawapeleka Ngorongoro ama Serengeti. Kwa hiyo, hilo nalo bado linaleta usumbufu mkubwa kwa sababu counter inayotumika katika uandikishwaji pamoja na ku-submit zile risiti ni moja. Je, Mamlaka haioni kwamba kuna ulazima sasa na umuhimu wa kuongeza madawati yale ya kutolea huduma hiyo ili kuokoa muda wa wageni unaopotea pale getini? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa biashara yoyote inahitaji huduma bora kwa wateja yaani customer care na hili limeonekana likikosekana maeneo ya geti la Lodware na Naabi Hill. Je, Mamlaka haioni kwamba wafanyakazi wale wanahitaji kupatiwa indoor training ya mara kwa mara ili kuweza kufanya utalii wa ushindani na nchi jirani ambako customer care iko juu? Ahsante. (Makofi)

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nishukuru sana kwa maswali mazuri ambayo Mheshimiwa Mahawe ameyauliza. Maswali haya ni relevance kabisa kwa kazi ambayo tunaifanya pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza suala la kuongeza madawati tumeliona na pale kwenye lango kuu kutoka Karatu unavyoingia Ngorongoro tumeongeza watendaji kazi kwa ajili ya kuwatambua watu ambao wanataka kuingia ndani ya hifadhi. Shughuli hii ni muhimu kwa sababu za usalama, lakini pia kwa sababu ya kuweza kukagua mapato tuliyokusanya na watu ambao wameingia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini napenda nimueleze Mheshimiwa Mahawe kwenye swali lake la pili kwamba ni kweli wafanyakazi wanahitaji kupatiwa mafunzo ya mara kwa mara ili kuongeza ubora wao katika customer care, lakini pia katika kushirikisha na kutoa maelekezo kwa wageni. Kwa hiyo, shughuli hii tutaendelea kuifanya kila siku na tunategemea kwamba itaongeza ufanisi wa eneo hili.

Name

Omary Ahmad Badwel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Kadi za kulipia Ngorongoro zimekuwa kero kwa wageni na wahudumu kwani muda mwingi umekuwa ukipotea wakati kufanya malipo. Je, ni lini Serikali itafanya marekebisho ili kuwe na mfumo wa kadi kama za TANAPA?

Supplementary Question 2

MHE. OMARY H. BADWEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa utozaji huu wa ushuru na kodi mbalimbali kutoka Wizara hii ya Maliasili na Utalii katika maeneo mbalimbali mahali pengine umekuwa ama haukufikiria vizuri au umekuwa kero. Kwa mfano katika mazao ya ubuyu na ukwaju, mazao ambayo yana bei ndogo sana kwa maana ya shilingi 100 kwa kilo na katika masoko ya Dar es Salaam na maeneo mengine ya miji yanauza kwa shilingi 200. Mazao haya yamekuwa yakivunwa ama na kina mama wenye kipato cha chini au vijana na watu wengine ambao wanapambana na umaskini.
Hata hivyo, Wizara hii kupitia Maliasili wanatoza shilingi 350 kwa kilo na imewafanya sasa wafanyabiashara hawa washindwe kabisa kufanya hii biashara kwa sababu bei yenyewe ni ndogo na sasa inafikia shilingi 500 baada ya ushuru huu.
Je, Mheshimiwa Waziri anafikiria nini juu ya kufuta ushuru huu ili kuwasaidia wale wafanyabiashara wadogo wadogo waweze kupambana na umaskini? (Makofi)

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba katika tozo za mazao ya misitu na mazao katika sekta ya utalii zingine ni kero sana kwa wananchi. Moja ya tozo hizo ambazo ni kero kwa wananchi ni tozo ya matunda ya ubuyu na matunda mengine ya misituni ambayo wananchi wanakusanya na kupeleka kuuza. Napenda kulihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba tozo hizi ambazo ni kero zitafutwa pamoja na hii ya kutoza kodi ya ubuyu. (Makofi)

Name

Anna Joram Gidarya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:- Kadi za kulipia Ngorongoro zimekuwa kero kwa wageni na wahudumu kwani muda mwingi umekuwa ukipotea wakati kufanya malipo. Je, ni lini Serikali itafanya marekebisho ili kuwe na mfumo wa kadi kama za TANAPA?

Supplementary Question 3

MHE. ANNA J. GIDARYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kumekuwa pia na kero katika sekta ya uwindaji katika utoaji leseni hasa kwa wazawa. Soko hili limemilikiwa zaidi kwa wageni kuliko wazawa. Kwa mfano, leseni ya uwindaji kwa mwaka unalipa dola 600 na tena unalipa dola 200.
Je, Wizara haioni umuhimu wa kuwapa wazawa zaidi ili pia waweze kulinda hifadhi zetu? (Makofi)

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka uliopita wa uwindaji unaoishia mwezi Juni, 2017 vitalu vilivyokuwa vimetolewa asilimia 85 walipewa wazawa na ni vitalu asilimia 15 tu ambavyo walipewa wageni. Kwa hiyo, siyo kweli kwamba utoaji wa vitalu unawapendelea wageni.