Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Suleiman Ahmed Saddiq
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mvomero
Primary Question
MHE. SULEIMAN A. SADDIQ (K.n.y. MHE. GOODLUCK MLINGA) aliuliza:- Kumekuwa na ongezeko kubwa la wanyama waharibifu kama vile viboko na tembo kwenye maeneo ya mashamba katika Kata za Ruaha, Chilombola, Ilonga, Ketaketa, Mbuga ya Lukande na Lupilo. Je, Serikali ina mpango gani kuzuia uharibifu huo wa mazao?
Supplementary Question 1
MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa Mikumi National Park imepakana na Wilaya ya Mvomero na kata za Doma, Msongozi, Melela, Malaka pamoja na Mangaye; kwa kuwa wanyama waharibifu wanaingia sana katika mashamba ya wakulima na wanaharibu sana mazao ya mahindi, mpunga, nyanya na kadhalika na kwa kuwa tembo wengi sana wameshafanya uharibifu mkubwa, je, Serikali sasa iko tayari kuongeza Askari wa Wanyamapori katika maeneo hayo angalau kila kata kuwe na askari mmoja ili kuondoa tatizo ambalo wananchi wanakabiliana nalo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Wilaya ya Mvomero ina upungufu mkubwa wa vitendea kazi, je, Serikali iko tayari sasa kuisaidia Wilaya ya Mvomero vitendea kazi pamoja na masuala mengine ya usafiri ili tuweze kukabiliana na hali hiyo? (Makofi)
Name
Prof. Jumanne Abdallah Maghembe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mwanga
Answer
WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba wanyama wakali na waharibifu wameongezeka katika maeneo mbalimbali hapa nchi na katika eneo la Wilaya ya Mvomero wanyama hawa wameongezeka sana katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saddiq Murad Mbunge wa Mvomero, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi pamoja na Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Wilaya tumetembelea hayo maeneo ambayo yamezidiwa sana na uvamizi wa wanyama wakali na waharibifu. Wizara itaongeza askari kusaidiana na wale walioko katika Wilaya ya Mvomero ili kupambana na kadhia hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Wizara itashirikiana na Halmashauri ya Mvomero kwa kuipa vitendea kazi zaidi pamoja na kuwasaidia katika usafiri ili waweze kukabiliana na tatizo hili ambalo limeongezeka sana katika Wilaya hiyo. (Makofi)
Name
Mbaraka Kitwana Dau
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mafia
Primary Question
MHE. SULEIMAN A. SADDIQ (K.n.y. MHE. GOODLUCK MLINGA) aliuliza:- Kumekuwa na ongezeko kubwa la wanyama waharibifu kama vile viboko na tembo kwenye maeneo ya mashamba katika Kata za Ruaha, Chilombola, Ilonga, Ketaketa, Mbuga ya Lukande na Lupilo. Je, Serikali ina mpango gani kuzuia uharibifu huo wa mazao?
Supplementary Question 2
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Tatizo la viboko lililopo katika Jimbo la Ulanga linafanana sana na tatizo la viboko lililopo Kisiwani Mafia. Wananchi wa kata za Ndagoni, Baleni na Kirongwe wameharibiwa mazao yao na ng’ombe wao wameuwawa na viboko waharibifu. Kutokana na ongezeko kubwa sana la viboko hawa na Kisiwa cha Mafia ni eneo dogo, je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kutoa ruhusa tuanze kuwavuna viboko hawa kwa sababu kule ni kitoweo pia? Ahsante. (Kicheko)
Name
Prof. Jumanne Abdallah Maghembe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mwanga
Answer
WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue fursa hii kumpa pole sana Mheshimiwa Dau na wananchi wake wa Mafia kwa kadhia hii ambayo imewakumba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ambayo tutachukua ni pamoja kutuma wataalamu waende wakafanye sensa ili tujue kwamba kuna viboko wangapi katika eneo hilo na tuweze kuangalia kama kuna uwezekano wa kuweza kuwavuna hao viboko ili kupunguza madhara yake kwa wananchi wa eneo la Mafia.
Name
Ester Amos Bulaya
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SULEIMAN A. SADDIQ (K.n.y. MHE. GOODLUCK MLINGA) aliuliza:- Kumekuwa na ongezeko kubwa la wanyama waharibifu kama vile viboko na tembo kwenye maeneo ya mashamba katika Kata za Ruaha, Chilombola, Ilonga, Ketaketa, Mbuga ya Lukande na Lupilo. Je, Serikali ina mpango gani kuzuia uharibifu huo wa mazao?
Supplementary Question 3
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la wanyama waharibifu ni kubwa sana katika Jimbo langu la Bunda Mjini na Jimbo la kaka yangu Boni. Sisi wananchi wa Mkoa wa Mara hatuhitaji kuomba chakula na mwaka jana Mheshimiwa Waziri wa Sera, Uratibu na Bunge, Mheshimiwa Jenista alikuja akaliona tatizo hilo na Mheshimiwa Waziri mwenyewe anajua, tatizo la tembo kuharibu mazao ya wananchi, kuua wananchi pamoja na mali zao. Sasa nataka kujua, ni lini Serikali mtahakikisha mnakuwa na mkakati wa kudumu wa kumaliza tatizo hili katika vijiji vyote vinavyozunguka hifadhi? (Makofi)
Name
Prof. Jumanne Abdallah Maghembe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mwanga
Answer
WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba katika Mkoa wa Mara na hasa Wilaya za Bunda, Serengeti, Tarime na Wilaya za maeneo yale kuna kadhia kubwa sana ya wanyama waharibifu wanaotoka hasa katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kuingia katika mashamba na wakati huu ambapo mavuno yanakaribia ndiyo kadhia hii inaongezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua za muda mfupi, mwaka tutachukua hatua ya kuongeza askari na magari ya patrol ili kuhakikisha kwamba kama mwaka jana tunawaokoa wananchi na tatizo hili.
Pili, tunazungumza na washirika wetu wa maendeleo kuona ni namna gani tunaweza kuweka fensi ya kilometa 140 ili kuangalia kwa majaribio kama itakuwa ni suluhisho la tatizo hili.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved