Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jamal Kassim Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Primary Question

MHE. JAMAL KASSIM ALI aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani katika kuwasaidia wafanyabiashara wa Kitanzania kuwekeza kwenye viwanda nchini?

Supplementary Question 1

MHE. JAMAL KASSIM ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza, Mheshimiwa Waziri katika jibu lake la msingi amekiri kwamba moja ya mambo muhimu kabisa ya Watanzania hawa kwenda kuwekeza kwenye viwanda ni pamoja na kuwa na mitaji. Watanzania hawa wamefanya biashara kubwa sana na Serikali na wana madeni makubwa ambayo wanaidai Serikali.
Je, Serikali haioni ipo haja sasa madeni haya ambayo wamekuwa wakidaiwa kwa muda mrefu kuyalipa kwa haraka ili Watanzania hawa nao sasa wapate fursa ya kwenda kushiriki katika uchumi wa viwanda ambao Mheshimiwa Waziri ameeleza? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, je, Serikali haioni ipo haja sasa ya kuja na sera maalum ambayo itatoa special incentive package kwa wawekezaji wazawa Watanzania ili nao waweze kushiriki kikamilifu katika uchumi wa viwanda kutokana na kuwa nyuma kiteknolojia, kifedha na mambo mengine ambayo ukiwaweka na wenzetu wa mataifa mengine Watanzania hawa hawawezi ku-compete? Ahsante. (Makofi)

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo wapo wafanyabiashara, wakandarasi ambao wamefanya kazi na Serikali na wanadai stahiki yao, Serikali itawalipa. Utaratibu wa Serikali unapitiwa na Mheshimiwa Waziri wa Fedha amekuwa akilisema mara kwa mara kwamba jambo kubwa ni kufanya uhakiki na kadri uhakiki unapofanyika hao watu wanalipwa na niwahakikishie kwamba Serikali itawalipa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na vivutio, sasa hivi kuna vivutio, suala la muhimu kwa wafanyabiashara wa Tanzania au kwa Watanzania ambao wangependa kupewa vivutio maalum waone hivi vivutio vilivyopo watuambie ni wapi sio vizuri. Hatuwezi kubadilisha vivutio, kwanza anza utuambie hiki siyo kizuri hiki ndiyo kizuri ndiyo tutabadilisha.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. JAMAL KASSIM ALI aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani katika kuwasaidia wafanyabiashara wa Kitanzania kuwekeza kwenye viwanda nchini?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona, naomba niulize swali la nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kuna mfuko wa NEDF ambao Mheshimiwa Waziri ameutaja yaani National Entrepreneur Development Fund, kwa mwaka huu pesa hizo hazijatoka. Napenda kupata kauli ya Serikali, je, ni lini hizo shilingi bilioni 2.5 zitatolewa ili ziweze kuwawezesha Watanzania wanaotaka kufungua biashara ndogondogo au kufungua viwanda vidogo vidogo waweze kuwezeshwa na kufanya hivyo? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mfuko wa NEDF kama mlivyoona taarifa ambayo imekuja pekee ni mfuko ambao unawachangamsha wawekezaji ukitoa mikopo mbalimbali. Katika mwaka wa fedha tunaomaliza tulitengewa shilingi bilioni 2.4, pesa hizo hazijatoka, lakini mwaka huu haujaisha. Nina imani hizo pesa zitakuja katika mwaka huu wa fedha na nimemkumbusha Waziri wa Fedha kwamba fedha hizo Wabunge wanazihitaji haraka wazipeleke Majimbo. Nina imani kabla jua halijazama pesa hizo zitapatikana.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. JAMAL KASSIM ALI aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani katika kuwasaidia wafanyabiashara wa Kitanzania kuwekeza kwenye viwanda nchini?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa sababu tunataka tuingie kwenye Tanzania ya viwanda na Tanzania ya viwanda ni lazima iende sambamba na uwekezaji kwenye ardhi lakini uwekezaji kwenye ardhi unakumbwa na matatizo makubwa. Tatizo la kwanza vijiji vyetu vingi havijaingia kwenye matumizi bora ya ardhi, matokeo yake mwekezaji anakosa nafasi na hata pale ambapo vijiji vimeshaingia kwenye matumizi bora ya ardhi kuna tatizo kwenye Makamishna wa Kanda katika upatikanaji wa ardhi lakini sio hivyo tu, hata kwenye Ofisi ya Rais ambapo nako kuna matatizo...
Je, nini kauli ya Serikali kwa wawekezaji wanaohangaika kutafuta ardhi ya kufanya uwekezaji katika kilimo? (Makofi)

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa rafiki yangu Alhaj ametaka kujua kauli ya Serikali. Tunalitambua tatizo la upatikanaji wa ardhi, ndiyo maana si mara moja Mheshimiwa Waziri Mkuu na Ofisi ya TAMISEMI wametoa maelekezo kwa mamlaka za Mikoa na Wilaya, watenge maeneo kwa wale walio tayari waweze kuwekeza mara moja. Nirudie, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, tengeni maeneo yule anayetaka kuwekeza msimsubirishe.