Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA atauliza:- Watanzania wamehamasika sana na kilimo cha tangawizi na zao la tangawizi kwa sasa linalimwa siyo tu na wananchi wa Wilaya ya Same bali pia katika Mikoa kama Mbeya, Kigoma na Ruvuma. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kulitafutia zao hilo soko la nje?

Supplementary Question 1

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshmiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa masoko ya nje yanatawaliwa sana na ubora wa mazao na kwa kuwa wanunuzi wa tangawizi kule nje wanapenda sana organic ginger. Sasa Serikali ina mpango gani wa kupeleka elimu kwenye zile sehemu ambazo zinalima sana tangawizi kama vile Mkoa wa Kilimanjaro, Mkoa wa Kigoma, Mkoa wa Mbeya na Mkoa wa Ruvuma?
Mheshimiwa Spika swali la pili, kwa kuwa Kiwanda cha Tangawizi cha Mamba Miamba kilichopo Wilayani Same kinategemea kuanza kusindika tangawizi ya kupeleka nje ya nchi katikati ya mwaka 2018.
Je, Serikali itatumia njia gani kuwafanya wananchi ambao wamekata tamaa kulima tangawizi kutokana na bei kushuka sana ili waendelee kulima tangawizi kwa sababu kiwanda hiki cha Mamba Miamba kitahitaji malighafi kwa wingi? Ahsante.

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Spika, kwa idhini yako napenda nichukue fursa hii kumtambua Mama Malecela kama Malkia wa Tangawizi. Suala la tangawizi amelifanyia kazi sana. Nichukue fursa hii kushukuru Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ambayo ameshughulikia pacha wangu, zimetengwa pesa nzuri zaidi ya shilingi bilioni
• kusudi hicho kiwanda kiwe na hadhi ya Kimataifa, kizingatie ubora kama nilivyoeleza. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kuhusu maswali mawili uliyoniuliza, moja la ubora, Wizara yangu inayosimamia SIDO kwa kutambua suala la viwango, maeneo yote ninaojenga sasa katika mikoa yote mipya tunajenga ofisi za SIDO, sheli, maabara, mahali pa kuchakatia chakula kwa viwango vitakuwa ni kipaumbele; Katavi, Rukwa, Geita, Simiyu ndiyo nakwenda kuanza nalo na pesa tayari ninazo kama nilivyoeleza juzi. Kwa hiyo, nitawafundisha wananchi hasa akina mama kuzalisha vyakula kwa viwango vya kuuza Kimataifa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, sasa suala la pili kwamba tutafanyaje, ndiyo tangawizi ilikuwa inauzwa Sh.3,500 najua leo bei imeshuka, sawa sababu mojawapo ni muanguko wa bei za bidhaa, commodity price duniani zote zime-dive. Tutafanya nini?
Kazi ninayofanya sasa ni kutafuta masoko makubwa, masoko mengi ya Kimataifa ile demand pool iwawezeshe wananchi wetu waweze kuuza zaidi lakini zaidi kupitia ESDP II tutaongeza tija (productivity) katika uzalishaji kusudi watu walime sehemu kubwa kwa gharama ndogo ile productivity iweze kupeleka hiyo tangawizi. Kwa sababu kiwanda chako hakina mfano, tangawizi yote itakwenda Mamba, ichakatwe, tupeleke Bandari ya Tanga iende duniani kuuzwa.

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA atauliza:- Watanzania wamehamasika sana na kilimo cha tangawizi na zao la tangawizi kwa sasa linalimwa siyo tu na wananchi wa Wilaya ya Same bali pia katika Mikoa kama Mbeya, Kigoma na Ruvuma. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kulitafutia zao hilo soko la nje?

Supplementary Question 2

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tatizo la Mheshimiwa Mama Kilango linafanana na tatizo lilipo kwangu kuhusiana na mbaazi ambapo wananchi wengi wamelima mbaazi kwa wingi na walihamasishwa kwamba kuna soko kubwa kule India.
Naomba Serikali itoe tamko ni lini mbaazi zile ambazo wananchi wanazo kwa wingi zitaanza kununuliwa?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BISHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Spika, ningekuwa na uwezo hili ndiyo swali ambalo ningependa nisiulizwe leo. Tunalo tatizo la mbaazi, Mheshimiwa Modi, Waziri Mkuu wa India alikuja hapa na akatuhakikishia soko la mbaazi nchini kwake, wananchi walisikia na mimi siwezi kukana nilikuwa mojawapo ya watu waliowahamasisha wananchi walime mbaazi na wamelima. Kilichotokea kwa maandishi, Serikali ya India imetuandikia barua kwamba haitanunua mbaazi zetu.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais akanituma India, nimekwenda India na vielelezo kwamba kulingana na mkataba wa tarehe 14 Januari 2000, Tanzania na India tulikubaliana kwenye suala hili mnapaswa mnunue mbaazi zetu. Tukazungumza vizuri na Serikali ya India wakapitia makabrasha yao wakaona kweli kuna haja ya kununua mbaazi zetu. Wakatuuliza takwimu tunazopaswa kupeleka kule, nikaangalia takwimu mara ya mwisho tulikuwa tumepeleka tani 280, tukakisia kwamba tutawaletea tani 300, nikatoka na bashasha na nderemo narudi nyumbani.
Mheshimiwa Spika, baada ya kufika hapa yule Waziri wa Biashara akapandishwa cheo na kuwa Waziri wa Ulinzi ikabidi nifanye kazi sasa ya kuanza kujenga urafiki na Waziri mpya kumueleza katika makabidhiano waweke suala langu. Hapa nilipo kila siku nimeweka Afisa Mkurugenzi anayewasiliana na India kuangalia kitu gani kinachoendelea.
Mheshimiwa Sapika, katika nchi nyingine, watu wako sensitive na watu wao, kilichotokea India walikuwa wana deficit ya tani milioni tano za mbaazi sasa wananchi wao wamelima wame-bridge ile gap na wananchi wa India Serikali haifanyi lolote mpaka iwafikirie wao. Mimi sifanyi protectionism, lakini na mimi nataka kuangalia watu wangu, masoko yangu yanakuwaje ndiyo maana naweza nikafanya mambo mengine mtu anasema Mwijage unakurupuka, hapana, naagalia maslahi ya wakulima wangu na ndiyo maana mimi naonekana kama mtu wa korosho na mimi naangalia korosho zangu ziende namna gani.
Mheshimiwa Spika, hili ndiyo tatizo lililotupata kwenye mbaazi na nalifuatilia na napozungumza Bwana Gugu, Mkurugenzi wa Biashara ya Kimataifa kabla ya saa 6.00 unieleze huyo mhindi ameshasema kitu gani. (Makofi/Kicheko)