Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) katika Mkoa wa Simiyu na kukijengea uwezo wa kutengeneza vifaa vya baiskeli, pikipiki na magari?

Supplementary Question 1

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Waziri alivyosema kwamba usanifu wa majengo utakamilika mwezi Novemba 2017, swali langu linauliza, ni maeneo gani yaliyobainishwa kujengwa chuo hicho? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, wakati Serikali inaendelea na mpango wa kujenga Chuo cha VETA Mkoa wa Simiyu, Serikali ina mpango gani kuwasaidia vijana wanaomaliza kidato cha nne wanaokosa sifa ya kuendelea na kidato cha tano? (Makof)

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Spika, Chuo cha Mkoa cha Simiyu kinategemewa kujengwa eneo ambalo lipo umbali wa takribani kilometa tisa mpaka kumi ambapo kilikuwa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi (FDC), eneo linalojulikana kama Kinamhala, nashindwa kidogo kutamka jina hilo, lakini ni eneo hilo.
Mheshimiwa Spika, vilevile katika swali lake la pili juu ya Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wanafunzi wanaomaliza kidato cha nne na hawajafanikiwa kidato cha tano. Kwanza ni kwamba tunavyo vyuo mbalimbali vinavyoweza kuchukua wanafunzi wa aina hiyo lakini vilevile Serikali kupitia mpango mpya wa ESPJ, mpango ambao unajipanga katika kuzalisha ajira nyingi kwa vijana wetu wale waliomaliza darasa la saba, kidato cha nne na ngazi nyingine zote ili waweze kupata ujuzi kamili wa kuweza kujiajiri. Kwa hiyo, kuna fedha tumeshapata nyingi kabisa, niwafahamishe tu Waheshimiwa Wabunge, Waziri wangu ameshatoa maelekezo kuwa kutakuwa na semina kwenu ya kuwapitisha juu ya mpango huo ambao utakuwa na manufaa makubwa sana katika nchi yetu.