Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

STELLA I. ALEX aliuliza:- Kwa kuzingatia umuhimu wa taulo za kike nchini. Je, Serikali inaonaje ikiondoa kodi kwenye taulo hizo?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kutokana na umuhimu wa taulo hizi za kike kwa wanawake na watoto wa kike Tanzania na kutokana na ughali wake ambao unapeleka wanawake wengi na watoto wa kike kushindwa kumudu kuzitumia na kwa kuwa Serikali imekiri kwamba maombi haya yameshawasilishwa na wadau wengi.
Mheshimiwa Spika, sasa Serikali inaweza ikatuambia nini wanawake wa Tanzania kwamba watoto wengi wanapata shida hasa watoto wa vijijini kwa sababu wanashindwa kuzipata hizi taulo kwa ughali wake. Sasa Serikali inaweza ikatuambia ni lini tutegemee kwamba lini huu mchakato utakamilika?
Mheshimiwa Spika, ingekuwa ni vizuri wakatuambia ni lini mchakato huu utakamilika kwa sababu kweli hili jambo ni suala nyeti sana kwa wanawake na watoto wa kike Tanzania? Ahsante. (Makofi)

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, na mimi kwa kweli namshukuru sana Mheshimiwa Stella Ikupa kwa swali lake zuri la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, mimi ni mwanamke lakini pia nina watoto wa kike wawili, kwa hiyo, nakubaliana na yeye kabisa kwamba tuna changamoto kubwa sana ya upatikanaji wa taulo za kike hasa kwa watoto walio vijijini na tunazo taarifa kuna watoto wanaweka mpaka majini ili kuweza kujisitiri pale wanapokwenda shule, lakini pia kuna watoto wanakosa hadi siku tano za masomo kwa sababu hawana zana za kujisitiri ili waweze kufanya masomo yao bila shida. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwahiyo, Wizara yangu nimeshamuandika Waziri wa Fedha kumuomba aharakishe mchakato huu, nilikuwa namtimizama hayupo lakini naamini wenzetu wa Wizara ya Fedha wanalifanyia kazi na tutakuja na majibu mazuri kadri itakavyokamilika, ahsante sana. (Makofi)