Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA (K.n.y. PHILIPO A. MULUGO) aliuliza:- Mji wa Mkwajuni ndio Makao Makuu ya Wilaya mpya ya Songwe. Katika mji huu hakuna maji na idadi ya wananchi na wakazi wanaongezeka kwa kasi:- Je, ni lini Serikali itajenga miradi katika mji huu pamoja na sehemu nyingine zisizo na maji katika Jimbo la Songwe?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, la kwanza, maji yanapokuwa ni adha kubwa waathirika wakubwa kwa kiwango kikubwa wanakuwa ni wanawake. Katika Wilaya hii mpya ya Songwe iliyoko Mkwajuni ni kilometa kumi tu kutoka katika Ziwa Rukwa, sasa nataka kujua, nini mpango wa Serikali katika kuvuta maji kutoka Ziwa Rukwa ambalo Mheshimiwa Mulugo amekuwa akililia kwa muda mrefu? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, Wilaya hii mpya ya Songwe, matatizo yake yanafanana sana na Wilaya ya Chunya ambayo ilikuwa ni Wilaya moja katika Mkoa wa Songwe. Katika Wilaya hii ya Chunya kuna Kata za Makongolosi, Matundasi na Bwawani hazina maji kwa muda mrefu sana. Nini mkakati wa Serikali katika hilo? Nashukuru.(Makofi)

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nimpongeze kwa swali zuri ambalo ameliuliza kwa niaba ya Mulugo. Kuhusu kwamba Mkwajuni iko kilometa kumi kutoka Ziwa Rukwa na angependelea kwamba maji yale yangepelekwa kwenye Mji wa Mkwajuni, jibu ni kwamba, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi kwamba tumetenga milioni 100 kwa ajili ya kufanya usanifu. Sasa usanifu ndiyo utaelekeza ni wapi tuchukue maji. Kama tutaona maji ya Ziwa Rukwa yanafaa basi tutachukua hapo na kuweza kupeleka maji katika Mji wa Mkwajuni. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu mkakati wa hizo
Kata za Makongolosi na zingine katika Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, mkakati wa Serikali ni kwamba katika bajeti kila Halmashauri tumeitengea fedha na tumetoa mwongozo kwamba wao watoe vipaumbele kulingana na zile bajeti. Inasikitisha kwamba unaweza kufika mahali kwenye Halmashauri ikiwepo hata hii ya Songwe, katika bajeti ya mwaka uliotangulia walitengewa milioni 752, lakini mpaka leo tunamaliza mwaka fedha zipo lakini hakuna kazi iliyofanyika.
Mheshimiwa Spika, nitakwenda kule kuangalia matatizo yao ni yapi ili tuweze kuwasaidia tuweze kutatua matatizo ya wananchi. (Makofi)

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA (K.n.y. PHILIPO A. MULUGO) aliuliza:- Mji wa Mkwajuni ndio Makao Makuu ya Wilaya mpya ya Songwe. Katika mji huu hakuna maji na idadi ya wananchi na wakazi wanaongezeka kwa kasi:- Je, ni lini Serikali itajenga miradi katika mji huu pamoja na sehemu nyingine zisizo na maji katika Jimbo la Songwe?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Mji wa Mkwajuni hauna tofauti na Mji wa Kasulu. Mji wa Kasulu sisi tuna maji mengi tu, tatizo letu ni maji machafu yanayotoka kwenye bomba. Sasa Mheshimiwa Waziri, ni lini atatujengea treatment plant ili tupate maji masafi kama sera za nchi yetu na Sera za CCM zinavyoagiza?

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kama anavyosema kwamba Mji wa Kasulu unapata maji ambayo ni machafu, lakini mkakati wa Serikali tumeshatoa maelekezo kwamba kuanzia sasa hatutatoa maji ambayo si salama kwa wananchi. Kwa hiyo, kitu cha kwanza tutaanza na mitambo midogo ya kuweka dawa, lakini jinsi hali ya uchumi inavyoboreka, tutapeleka mitambo ya kuweza kusafisha maji kubadilisha rangi kuwa rangi ya tope yawe maji meupe. Kwa hiyo, huu ndio mkakati wa Serikali katika kuhakikisha wananchi wetu wanapata maji safi na salama na ni meupe, mazuri.