Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Singida Mjini ni Mji unaokuwa kwa kasi sana na tumetenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji:- Je, Serikali iko tayari kuleta wawekezaji?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, namwomba Mheshimiwa Waziri awahakikishie wananchi wa Jimbo la Singida Mjini kwamba miradi hiyo aliyoitaja, miradi 33 iliyosajiliwa yenye kutoa ajira zaidi ya 4,000 itaanza lini?(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Serikali imehamia Dodoma na yako Mashirika ndani ya Wizara, Ofisi za Kanda zipo Dodoma: Je, Mheshimiwa Waziri, sasa upo tayari Mashirika hayo kwa mfano TFDA, TBS na mengine kuanzisha Ofisi za Kanda Singida Mjini ili kuweka ufanisi wa kazi hiyo? (Makofi)

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ile miradi 33 niliyoisema, nimesema kuanzia mwaka 1996 mpaka Aprili, 2017, miongoni mwa viwanda hivyo ni kiwanda cha mafuta cha Mount Meru, kimeshaanza kazi. Viwanda hivyo vimeshaanza kazi; na mojawapo ya viwanda hivyo ni Kiwanda cha Maziwa anachokijasiria Mheshimiwa Kingu. Tumeshaanza kazi. Tanzania sasa tunajenga viwanda. Sasa labda anieleze wapi anataka mimi nisukume kwa nguvu kusudi mambo ya nchi yetu yaendelee vizuri na yeye yamnyookee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuanzisha kanda za TBS na TIRDO, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba hakuna tija kuwa Dodoma ukaanzisha Branch Singida, kwa sababu unaweza kuondoka asubuhi ukafanya kazi Singida, ukarudi hapa, ukarudi tena, ukarudi tena. Kwa hiyo, itabaki Dodoma na itakuwa rahisi hata Mheshimiwa Waziri kwenda na Mheshimiwa, rafiki yake wakaweza kuhamasisha shughuli za viwanda.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Singida Mjini ni Mji unaokuwa kwa kasi sana na tumetenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji:- Je, Serikali iko tayari kuleta wawekezaji?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuelekea kwenye nchi za viwanda; na ninavyofahamu mimi ili twende huko, lengo kubwa ni kuchakata mazao yanayolimwa hapa nchini; lakini kama ambavyo swali namba 206 lilivyojibiwa, sijaona mkakati unaowekwa kwenye zao la ufuta. Ni namna gani Serikali imejipanga kutangaza ili tupate wawekezaji kwenye kusindika mazao ya ufuta?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua haya maneno ya mkakati na vipaumbele yanaleta shida. Nilivyosema kwenye swali la msingi Na. 206 nimesema, viwanda vidogo na viwanda vya kati ni viwanda tunavyoweza kuvimudu. Nikaenda zaidi nikasema sisi Waheshimiwa Wabunge tuwe wa kwanza, kwa sababu sisi ni watu ambao tunafuatwa na watu, ni influential, ukianzisha kiwanda wewe cha shilingi milioni 200, watu wa kwenu wote wakianzisha viwanda, viwanda vitatekelezwa. Ndivyo hivyo nilivyosema.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Singida Mjini ni Mji unaokuwa kwa kasi sana na tumetenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji:- Je, Serikali iko tayari kuleta wawekezaji?

Supplementary Question 3

MHE. JUMAA H. AWESO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Kwa kuwa Mkoa wa Tanga ni miongoni mwa Mikoa ambayo imetenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji. Je, Serikali ina mkakati gani ya kufufua na kuwekeza viwanda vipya? Ahsante sana.

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ningekuwa na uwezo hili swali nisingelijibu, kwa sababu Mheshimiwa Mbunge ananilazimisha nisome hotuba ya bajeti yangu kabla ya muda na shughuli ni kesho kutwa. Nimejipanga kwa ajili ya Tanga na Jumatano nitawaonesha. (Makofi)