Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lathifah Hassan Chande

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATHIFAH H. CHANDE aliuliza:- Uzalishaji wa zao la ufuta limeongezeka kwa msimu wa mwaka 2015/2016 na kusababisha kushuka kwa bei ya ufuta sokoni:- Je, ni lini Serikali itajenga kiwanda cha kukamulia ufuta Wilayani Liwale?

Supplementary Question 1

MHE. LATHIFAH H. CHANDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kutokana na kwamba demand ya Soko la Dunia ni ufuta mweupe, lakini Tanzania tumekuwa tukilima ufuta wa brown ambao bei yake inakuwa haina thamani kubwa kama ilivyo ufuta mweupe: Je, Serikali ina mpango gani wa kuweza kuwasaidia wakulima wa ufuta nao waweze kuanza kulima ufuta mweupe ili kuweza kuongeza kipato? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, ni juu ya Kiwanda cha Korosho kilichopo Lindi, Kiwanda cha TANITA ambacho kilikuwa kinaendeshwa na Serikali na kiliweza kuwapatia ajira wananchi wengi. Sasa hiki Kiwanda cha Korosho, TANITA, kimebinafsishwa ambapo hamna shughuli yoyote inayoendelea baada ya ubinafsishwaji huu na kupelekea wananchi kukosa ajira. Je, Serikali ina mpango gani juu ya kukifufua kiwanda hiki kutokana na kwamba Sera ya Serikali ya Awamu ya Tano ni Tanzania ya viwanda? Ina mpango gani juu ya kufufua hiki kiwanda na viwanda vingine vingi vilivyoko Mkoani Lindi? Ahsante.

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Lathifah ameuliza swali lake la kwanza wakati muafaka; bajeti ya Wizara ya Kilimo inafuata nami nitamhimiza Waziri wa Kilimo kwamba tulete mbegu zinazozalisha ufuta mweupe ambao una soko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kiwanda cha korosho, Serikali ina mpango gani? Mpango wetu ni kuhakikisha kwamba viwanda vyote vilivyobinafsishwa vinafanya kazi. Hatuendi kwa kasi inayotakiwa kama nitakavyoeleza kwenye bajeti yangu kesho kutwa, ni kwa sababu viwanda vingine vina matatizo ya mikataba ya kisheria, lakini dhamira yetu ni hiyo na tutahakikisha viwanda vyote vinafanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na viwanda hivi, wako wawekezaji wanakuja na nitahakikisha Mheshimiwa Mbunge tunashirikiana kwamba Waheshimiwa Wabunge wanaokuja waende Lindi na nimeshazungumza hata na ndugu yangu, viwanda vingi vitakwenda vitaanzishwa ikiwemo na kufufua vile vya zamani.

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATHIFAH H. CHANDE aliuliza:- Uzalishaji wa zao la ufuta limeongezeka kwa msimu wa mwaka 2015/2016 na kusababisha kushuka kwa bei ya ufuta sokoni:- Je, ni lini Serikali itajenga kiwanda cha kukamulia ufuta Wilayani Liwale?

Supplementary Question 2

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Swali langu ni kwamba, kwa kuwa Mkoa wa Pwani wanalima sana matunda ya aina mbalimbali na kwa kuwa kiwanda kipo eneo moja tu Mkuranga ambacho sasa hivi kinazalishana kiwanda kingine kinajengwa Chalinze. Je, ni lini Serikali itawashawishi wenye Kiwanda hicho kuhakikisha wanakuwa na maeneo maalum ya kuwasaidia wakulima kwenda kupeleka mazao yao na kuuza badala ya kutafuta magari na kupeleka mpaka kwenye kiwanda? (Makofi)

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kiwanda cha Evelyne kinachokausha matunda asilia na Kiwanda cha Sayona kitakachochakata matunda ya aina zote, mara wanapoanza uzalishaji wataweka collection point. Evelyne wakati wowote atazinduliwa na kuanza kazi, mboga tunategemea aanze mwezi wa Tisa. (Makofi)

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATHIFAH H. CHANDE aliuliza:- Uzalishaji wa zao la ufuta limeongezeka kwa msimu wa mwaka 2015/2016 na kusababisha kushuka kwa bei ya ufuta sokoni:- Je, ni lini Serikali itajenga kiwanda cha kukamulia ufuta Wilayani Liwale?

Supplementary Question 3

MHE. KHADIJA N. ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Serikali imekuwa ikiagiza tani laki nne za mafuta kila mwaka, wakati tuna malighafi za kutosha hapa nchini. Je, Serikali ina mpango gani wa kutumia mazao hayo ipasavyo ili kuweza kuokoa fedha za kigeni zinazopotea kwenye kuagiza mafuta hayo nje ya nchi? (Makofi)

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunatumia mafuta tani laki nne kwa mwaka na 70 percent inaagizwa kutoka nje. Tunahamasisha ulimaji wa alizeti; tuna mpango wa kulima migaze au michikichi Kigoma na Pwani; pindi tutakapokuwa tumejitosheleza, tutaweza kuzuia mafuta kutoka nje. Hatuwezi kufanya makosa ya kuzuia mafuta kutoka nje, matokeo yake ni kwamba mafuta yatapanda bei.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kigoma wakiwa tayari, Pwani wakawa tayari na alizeti zikawa za kutosha, hatutazuia ugavi kutoka nje. Ugavi kutoka ndani utazuia mafuta yasije. Sisi ni member wa WTO na katika mpango wa WTO, bei ni nguvu ya soko inayomzuia mshindani asiingie kwenye soko letu.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATHIFAH H. CHANDE aliuliza:- Uzalishaji wa zao la ufuta limeongezeka kwa msimu wa mwaka 2015/2016 na kusababisha kushuka kwa bei ya ufuta sokoni:- Je, ni lini Serikali itajenga kiwanda cha kukamulia ufuta Wilayani Liwale?

Supplementary Question 4

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa nchi za Uturuki, Ujerumani na Italy wanakunywa sana chai ya Tanzania. Je, ni lini Serikali itapeleka Kiwanda katika Wilaya ya Rungwe kwa ajili ya wakulima wa chai ili waweze kuuza chai yao ambayo ni nyingi ikaweza kusaidia katika hizo nchi nyingine?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo tulilonalo ni nguvu ya soko. Mheshimiwa Sophia tumeshazungumza kwenda kwenye maonesho ya Kimataifa kwenda kutafuta hayo masoko. Leta hizo order zako kusudi demand pool iwashawishi watu wachakate chai. Kuna watu wana chai hawana soko, sasa wewe nimeshakuruhusu uende kwenye maonesho. Nenda basi ulete hizo order. (Kicheko/Makofi)