Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Lengo la Serikali ni kuwainua kiuchumi wananchi maskini vijijini hasa wanawake ambao hawana dhamana ya kuweka benki ili waweze kupata mikopo kwa sababu nyumba nyingi za vijijini hazina Hatimiliki ambazo zingeweza kutumika kama dhamana benki. Je, Serikali inawasaidiaje wananchi na hasa wanawake kwa kuzungumza na benki ili zikubali kukpokea Hatimiliki za kimila kama dhamana ya mikopo?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mojawapo ya shida inayowapata wanawake ni mitaji na Serikali imeweka pesa nyingi sana kwenye mabenki ili wakope, lakini wanapotaka kwenda kukopa kwenye mabenki wanaambiwa wapeleke hati, wanapokwenda kutafuta hati kwenye Ofisi za Ardhi wanahangaishwa sana; wanaambiwa wapeleke vitu vingi sana na wanaambiwa milolongo ya mambo mpaka wanaamua kuacha, zaidi ya mwaka mtu anafuatilia hati. Ni lini sasa Serikali itaweka gharama halisi za kupata hati?(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Benki ya Wanawake ipo Dar es Salaam tu, ni lini sasa Serikali itaamua kufungua matawi mengine katika mikoa mingine ili wanawake wapate huduma hiyo? (Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna usumbufu katika kupata hati na hasa hizi Hakimiliki za kimila ambazo tunazizungumzia kwasababu shughuli yote inafanyika katika maeneo husika na katika vijiji husika. Kwa hiyo, mimi niseme pale ambapo Halmashauri yoyote inaonekana kwamba ni kikwazo katika kuwapatia wananchi hati za Hakimiliki za kimila tuwasiliane kwa sababu lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba mwananchi wa Kijijini tunamuwezesha kuweza kupata hati yake ya Hakimiliki ya kimila.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni kwasababu ndio sehemu pekee ambayo inaweza kumkomboa na mpaka sasa kama nilivyosema hati 400,761 zimeshatoka ni kwasababu tu ya ushirikiano wa karibu sana na wenyewe baada ya kuwa tumewaelimisha kwamba hati zile zinakwenda kuwakomboa katika shughuli za kimaendeleo. Kwa hiyo, pale wanapokwama naomba tuwasiliane ili tushughulikie.

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru; naomba kujibu swali la pili la nyongeza la Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata na ninaomba majibu yangu yaende kwa wanawake wote wa Tanzania kwamba Benki ya Wanawake ilianzishwa kwa malengo ya kuwahudumia, lakini kwa sasa ina changamoto kubwa za kimtaji na tutafungua matawi mikoani pindi ambapo uwezo wetu wa kimtaji wa Benki ya Wanawake utakavyoimarika. Ila kwa sasa tulichokifanya ni kuhakikisha tunafungua vituo vya kuwahudumia na kuwawezesha wanawake kwenye mikoa zaidi ya 18 nchini ili kuwapa elimu ya ujasiriamali lakini pia mikopo midogo midogo isiyo na dhamana ambapo wanawake wanadhaminiana wao kwa wao. (Makofi)

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Lengo la Serikali ni kuwainua kiuchumi wananchi maskini vijijini hasa wanawake ambao hawana dhamana ya kuweka benki ili waweze kupata mikopo kwa sababu nyumba nyingi za vijijini hazina Hatimiliki ambazo zingeweza kutumika kama dhamana benki. Je, Serikali inawasaidiaje wananchi na hasa wanawake kwa kuzungumza na benki ili zikubali kukpokea Hatimiliki za kimila kama dhamana ya mikopo?

Supplementary Question 2

MHE. ZAINAB A. KATIMBA:Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza.
Serikali ina mpango kabambe wa kupima na kurasimisha ardhi nchi nzima na imekuwa ikishirikisha sekta binafsi katika kufanya hivyo. Aidha, kumekuwa na gharama kubwa sana katika upimaji na urasimishaji huo wa ardhi. Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya mapitio ya gharama hizo ili kuweza kuwapunguzia wananchi mzigo? (Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Zainab anazungumzia habari ya gharama kubwa katika suala zima la upimaji. Lakini naomba nimkumbushe tu bajeti ya mwaka jana ilivyosomwa gharama zile zilishuka kutoka shilingi 800,000 kwa heka mpaka shilingi 300,000 kitu ambacho ilipunguza sana gharama zinaongezeka kulingana na ukubwa wa eneo ambalo linaenda kupimwa. Kwa mwaka huu pia katika bajeti yetu nadhani kuna maeneo ambayo Serikali imeyafanyia kazi mtayasikia wakati tunatoa bajeti.
Kwa hiyo, niseme kwamba gharama tunaziangalia
na namna bora ya kuweza kumuwezesha mwananchi wa kawaida aweze kupima ardhi yake na kuweza kumiliki ili kumletea maendeleo katika shughuli zake.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Lengo la Serikali ni kuwainua kiuchumi wananchi maskini vijijini hasa wanawake ambao hawana dhamana ya kuweka benki ili waweze kupata mikopo kwa sababu nyumba nyingi za vijijini hazina Hatimiliki ambazo zingeweza kutumika kama dhamana benki. Je, Serikali inawasaidiaje wananchi na hasa wanawake kwa kuzungumza na benki ili zikubali kukpokea Hatimiliki za kimila kama dhamana ya mikopo?

Supplementary Question 3

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwa kuwa Serikali kwa kutambua wanawake inakuwa vigumu kupata mikopo kwenye mabenki, imekuwa ikitoa hela na wakati mwingine pia ikipeleka kwenye mabenki, lakini wanawake wanakopeshwa kupitia kwenye vikundi vyao zikiwemo mabilioni ya JK.
Swali langu nauliza, wanawake wa vijijini hawakunufaika na hizo hela, sasa Serikali inafanyaje kuhakikisha kwa kuwa zile hela ni za mzunguko na bado tuna amini zipo, zitawafikiaje wale wanawake wa vijijini?(Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda tu niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge kwamba sisi wote ni wajumbe katika zile Halmashauri zetu na mikopo inapopitishwa inapitia katika vikao vya Baraza la Madiwani.
Kwa hiyo, mimi naomba pale ambapo tunapitisha vikundi vyetu viweze kupewa mikopo ni lazima tuzingatie pia tunao akina mama wanaotoka katika maeneo ya Vijiji ili na wao waweze kufikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa suala la mabenki, benki wana masharti yao ambayo yanatakiwa yatimizwe, kwa hiyo tujaribu kuwaelimisha wakina mama ili waweze kukidhi vigezo vinavyotakiwa na mabenki na sisi wenyewe tuwe mstari wa mbele katika kuangalia ni vikundi vipi ambavyo vimekidhi vigezo hivyo na tuawasidie katika hatua za kuweza kupata mikopo either kutoka katika benki au kutoka katika Halmashauri kupitia ule Mfuko wa Wanawake na Vijana.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Lengo la Serikali ni kuwainua kiuchumi wananchi maskini vijijini hasa wanawake ambao hawana dhamana ya kuweka benki ili waweze kupata mikopo kwa sababu nyumba nyingi za vijijini hazina Hatimiliki ambazo zingeweza kutumika kama dhamana benki. Je, Serikali inawasaidiaje wananchi na hasa wanawake kwa kuzungumza na benki ili zikubali kukpokea Hatimiliki za kimila kama dhamana ya mikopo?

Supplementary Question 4

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, zaidi ya asilimia 70 ya nguvu kazi ya kilimo ni wanawake, lakini ni kwa bahati mbaya sana inapokuja suala la umiliki wa ardhi, wanawake wanaomiliki ardhi ni pungufu hata ya asilimia 20. Na hata ninavyozungumza hati za kawaida na hati za kimila haziwanufaishi wanawake kwasababu sheria za nchi yetu zinatambua Sheria za Kimila ambazo zina ubaguzi.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nilitaka Wizara inisaidie katika mpango wenu mpana wa kuweza kufanya maboresho kwenye sekta ya ardhi mna mikakati gani ya kuweza kuondokana na sheria kandamizi ili umiliki wa ardhi usiwe na ubaguzi hivyo shughuli za uchumi zinufaishe makundi yote? (Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda nimhakikishie Mheshimiwa kwamba sheria zetu tulizo nazo sasa pamoja na kanuni pamoja na kwamba Sera ya Ardhi pia inapitiwa upya, hazikandamizi wala hazibagui mwanamke kuweza kupata hati. Ndio maana zoezi linaloendelea sasa la kutoa hati miliki za kimila kuna mahali ambapo unakuta mke na mume wote wanakabidhiwa hati kwa pamoja, aidha wanakubaliana iandikwe jina la mke au iandikwe majina yote mawili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo tumeshaanza kuangalia kwa sababu wengi walikuwa wakinyanyasika katika hilo. Kwa hiyo, tunajaribu kupitia upya pia sera tuweze kuona lakini haya yote yanawezekana katika kufanyika ili kuweza kuhakikisha kwamba akina mama nao pia hawako nyuma katika umiliki wa ardhi. Ni kweli lilikuwepo tatizo hilo lakini limeanza kuondoka kwa taratibu.

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kumalizia kazi la Mheshimiwa Mdee, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri kwamba ni kweli sheria hazibagui, lakini pia hata kama akipata mwanaume hati ya kimila au hati ya muda mrefu, wakati wowote ule mwanamke ajue ile hati ni salama. Hii ni kwa sababu kwa utaratibu wa sasa mwanaume akitaka kuuza au kubadilisha ile hati hatumkubalii mpaka tumuulize mkewe na vilevile mwanamke akitaka kuuza lazima tumuulize mumewe ili kuonyesha kwamba mali haipotei whether imeandikwa mwanaume au mwanamke wakati wa kupoteza lazima yoyote aulizwe. Kwa hiyo, mwanamke amelindwa sana katika sheria za sasa. (Makofi)

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Lengo la Serikali ni kuwainua kiuchumi wananchi maskini vijijini hasa wanawake ambao hawana dhamana ya kuweka benki ili waweze kupata mikopo kwa sababu nyumba nyingi za vijijini hazina Hatimiliki ambazo zingeweza kutumika kama dhamana benki. Je, Serikali inawasaidiaje wananchi na hasa wanawake kwa kuzungumza na benki ili zikubali kukpokea Hatimiliki za kimila kama dhamana ya mikopo?

Supplementary Question 5

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana; sambamba na wenzangu ni lini Serikali itakwenda vijijini kukutana na akina mama ambao wanahodhi maeneo mengi na maeneo hayo wanaweza wakaanzisha viwanda vidogo vidogo lakini unakuta wanakwama kwa kuwa hawana hati za kimila au zile za kiserikali ambazo zinaweza zikawasaidia kuwapa mikopo na wao kuingia katika uchumi wa viwanda? (Makofi)

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kumalizia kazi la Mheshimiwa Mdee, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri kwamba ni kweli sheria hazibagui, lakini pia hata kama akipata mwanaume hati ya kimila au hati ya muda mrefu, wakati wowote ule mwanamke ajue ile hati ni salama. Hii ni kwa sababu kwa utaratibu wa sasa mwanaume akitaka kuuza au kubadilisha ile hati hatumkubalii mpaka tumuulize mkewe na vilevile mwanamke akitaka kuuza lazima tumuulize mumewe ili kuonyesha kwamba mali haipotei whether imeandikwa mwanaume au mwanamke wakati wa kupoteza lazima yoyote aulizwe. Kwa hiyo, mwanamke amelindwa sana katika sheria za sasa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Vulu nataka kukushauri tu kwamba hayo mashamba na maeneo ambayo wanawake wanamiliki au yapo kwenye mtaa au vijiji, washauri hao wanawake wajihusishe na mamlaka zinazohusika ndani ya Halmashauri ili wawapimie waweze kupata. Kama wapo mijini hawapati hati za kimila wanapata Title Deed za muda mrefu, lakini kama wapo vijijini wapete hati za kimila. Ardhi inapimwa na inamilikishwa na Halmashauri za Wilaya. (Makofi)