Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Barabara ya Mishamo imeombewa kibali ili ipandishwe hadhi na kuwa barabara ya Mkoa lakini hadi sasa hatujui kinachoendelea. Je, ni lini barabara hiyo itapandishwa hadhi na kuwa chini ya TANROADS?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa taratibu zote za kuipandisha hadhi barabara hii zilishafanyika ikiwemo kupitia vikao halali vya Wilaya na Mkoa na kikao cha Road Board mimi mwenyewe nilishiriki tukaipitisha hii barabara. Nilikuwa nataka kuuliza ni sababu ipi inayokwamisha kutokupandishwa hadhi kwa barabara hii?
Pili, kwa kuwa Mheshimiwa Rais wakati anaanza safari ya ushindi ya kuomba ridhaa ya wananchi, ziara yake ya kwanza aliifanya Mkoa wa Katavi na kituo cha kwanza alianzia maeneo ya Mishamo aliwaahidi wananchi wa Mishamo kuwaboreshea barabara hiyo ya kutoka Mishamo mpaka Ziwa Tanganyika kwenye jimbo la Mheshimiwa Hasna Mwilima.
Je, hawaoni sasa ni wakati muafaka wa kutekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais, ambayo aliwaahidi wananchi wa Mishamo ili kutekeleza ahadi iliyokuwa ameiahidi?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukurusana Mheshimiwa Moshi Kakoso kwa sababu itabidi nikapate ukweli ama mkoa haujawasilisha Wizarani ama pale Wizarani pana uzembe. Kwa hiyo, nitakwenda niangalie na nifuatilie hili suala kama kikao halali kilishakaa kwa nini Wizarani hatujapata hayo maombi.
Kwa hiyo, baada ya hapo nikishajua wether kuna tatizo Mkoani inawezekana walikaa lakini hawakuwasilisha au pengine pale Wizarani kuna tatizo.Nitakapopata jibu mtaona matokeo yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu barabara ya Mishamo kwenda mpaka Baharini ni ahadi ya Mheshimiwa Rais, wakati wa kampeni tumeipata tunayo katika orodha ya ahadi tulizonazo, nikuhakikishie kwamba tunakwenda awamu kwa awamu katika kutekeleza ahadi zote ambazo tuliziahidi katika kipindi hiki cha miaka mitano. Tutahakikisha ahadi hiyo nayo tutaitekeleza.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Barabara ya Mishamo imeombewa kibali ili ipandishwe hadhi na kuwa barabara ya Mkoa lakini hadi sasa hatujui kinachoendelea. Je, ni lini barabara hiyo itapandishwa hadhi na kuwa chini ya TANROADS?

Supplementary Question 2

MHE.GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Sasa hivi ninavyoongea barabara ya Ifakara - Mahenge haipitiki kabisa, wananchi wanakosa huduma za muhimu kama petroli, dizeli na dawa kwa ujumla. Je, wananchi wa Ulanga wanataka kusikia kauli ya Serikali nini kitafanyika sasa hivi ili watu hawa wa waweze kusafiri kwenda Mahenge? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kuitaka TANROADS Taifa na TANROADS Mkoa wa Mogororo washughulikie ufunguzi wa barabara hii iliyokatika.(Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Barabara ya Mishamo imeombewa kibali ili ipandishwe hadhi na kuwa barabara ya Mkoa lakini hadi sasa hatujui kinachoendelea. Je, ni lini barabara hiyo itapandishwa hadhi na kuwa chini ya TANROADS?

Supplementary Question 3

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Barabara ya kutoka Kitunda - Kivule -Msongola ninapozungumza sasa hivi haipitiki kabisa nauli imepanda kutoka shilingi 500/= mpaka shilingi 1,000/=; walimu na wanafunzi ambao wanasoma shule ya Mvuti, Mbondole, Kitonga wanatembea kwa miguu kwa umbali wa zaidi ya kilometa 11.
Ningeomba kujua ni hatua gani kwasasa Mheshimiwa Waziri unaweza akachukua kuwasaidia wananchi wale na hasa watumishi wa umma ili waweze kuendelea kupata huduma muhimu katika eneo hilo? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nafurahi sana hawa Wabunge wawili wanafanyakazi pamoja ikiwa ni pamoja na Mbunge Bonnah Kaluwa, Mbunge wa Segerea. Alishalileta hilo na kwa taarifa yako TANROADS Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na TANROADS Taifa hivi tunavyoongea wanalishughulikia hilo kwa namna ambayo lililetwa kwetu na Mheshimiwa Bonnah Kaluwa. (Makofi)

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Barabara ya Mishamo imeombewa kibali ili ipandishwe hadhi na kuwa barabara ya Mkoa lakini hadi sasa hatujui kinachoendelea. Je, ni lini barabara hiyo itapandishwa hadhi na kuwa chini ya TANROADS?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize swali ya nyongeza kwamba barabara ya kutoka Igurubi mpaka Igunga kwenda Loya tuliiombea na tulishapeleka maombi kwamba ipandishwe hadhi. Leo mwaka wa tano kuna shida gani?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, maombi ya kupandisha hadhi barabara tunayoyashughulikia sasa ni ya muda mrefu ya kuanzia mwaka 2011/2012 mpaka sasa. Kwa hiyo, nikuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara yako nayo tutakuja kutoa majibu ipi imekubalika kupandishwa hadhi, ipi imekubalika kukasimiwa na ipi tutapendekeza ibakie kwenye Halmashauri, muda sio mrefu maadamu Waziri wangu tayari ameshaanza kulifanyia kazi kwa kasi inayotakiwa kwa sasa...

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Barabara ya Mishamo imeombewa kibali ili ipandishwe hadhi na kuwa barabara ya Mkoa lakini hadi sasa hatujui kinachoendelea. Je, ni lini barabara hiyo itapandishwa hadhi na kuwa chini ya TANROADS?

Supplementary Question 5

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti…
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize kwali la nyongeza. Kuna barabara ya kutoka Nyororo – Igohole mpaka Mtwango ina kilometa 40 na upembuzi yakinifu ulishafanyika miaka miwili iliyopita. Je, Serikali ni lini itaanza ujenzi wa kiwango cha lami ile barabara? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamuomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane tupate takwimu sahihi ya barabara unayoongelea inaanzia wapi, inafikia wapi, ina kilometa kiasi gani na kama imeshajadiliwa kwenye Road Board ya Mkoa ili hatimaye tutende haki ya kile kinachotakiwa katika barabara hiyo.

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Barabara ya Mishamo imeombewa kibali ili ipandishwe hadhi na kuwa barabara ya Mkoa lakini hadi sasa hatujui kinachoendelea. Je, ni lini barabara hiyo itapandishwa hadhi na kuwa chini ya TANROADS?

Supplementary Question 6

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize swali kwamba kwa kuwa ahadi za Rais wakati anaomba kura zimekuwa nyingi na Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya kuzitekeleza ikiwepo barabara ya Monduli Juu kule kwa Sokoine. Ni kwa nini Serikali sasa isilete programu maalum inayoonyesha ni lini ahadi hizo zitatekelezwa na fedha zake katika nchi nzima? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi zote ambazo Mheshimiwa Rais alizitoa wakati wa kampeni tunazitekeleza awamu kwa awamu, hatuwezi kuzitekeleza zote katika kipindi cha mwaka mmoja. Kuna kipindi cha miaka mitano na tutahakikisha…
… ahadi zote tunazitekeleza.

Name

Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Barabara ya Mishamo imeombewa kibali ili ipandishwe hadhi na kuwa barabara ya Mkoa lakini hadi sasa hatujui kinachoendelea. Je, ni lini barabara hiyo itapandishwa hadhi na kuwa chini ya TANROADS?

Supplementary Question 7

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Kwa hali ilivyo sasa hivi Moshi Vijijini barabara nyingi hazipitiki na hali ni mbaya sana katika kata ya Mabogini barabara inayoanzia Bogini kwenda Chekereri mpaka kule Kahe na kule Uru Mashariki kata ya Uru Madukani, Mamboleo, Kishumundu mpaka kule Materuri. Hizi barabara zote zimeshaombewa kupandishwa daraja lakini hakuna kinachoeleweka. Sasa ninataka kufahamu kutoka kwa Waziri atakuwa tayari kutoa agizo kwa ajili ya kufanyika tathmini maalum ili hizi barabara tujue tatizo liko wapi? (Makofi)

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninaamini Halmashauri iendelee kurekebisha hii barabara iweze kupitika muda wote, lakini wakati huo huo majibu ya barabara zipi tutapandisha hadhi yatakuja muda sio mrefu ujao.