Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Vijana wengi walioathirika na dawa za kulevya wanaleta kero kubwa ndani ya jamii, kutengwa na wazazi wao na kukosa msaada wa kifedha pale wanapoamua kuacha na kujiunga na kituo cha tiba. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa matibabu bure kwa vijana hao ili warudi katika hali zao za kawaida na hatimaye kuendelea na ujenzi wa Taifa?

Supplementary Question 1

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naipongeza Serikali kwa kuunda Tume ya Kupambana na Kudhibiti Dawa za Kulevya na kuongeza vituo vya tiba. (Makofi)
Swali langu la kwanza, Serikali baada ya kupiga marufuku uingizaji wa biashara za viroba na kuteketeza mashamba ya bangi, je, adhabu gani iliyowekwa kwa wale watakaoingiza viroba na wale watakaopanda mbegu za bangi katika mashamba yao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, je, ni Mkoa gani unaoongoza kwa idadi ya vijana walioathirika zaidi kwa dawa za kulevya? Na Serikali inawaangaliaje vijana hao baada ya kupona? Watawapa msaada gani ili waweze kujiendeleza na maisha yao?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, adhabu gani watapata; adhabu zimeainishwa kwenye sheria zetu, tuna sheria inayozuia matumizi ya vilevi, hususan dawa za kulevya (The Narcotic and Drug Abuse Act) kwa hivyo, ndani mle imeainishwa adhabu ya mtu anayetumia na mtu anayeingiza na mtu anayesaidia kuwezesha mambo hayo. Kwa hiyo, adhabu itatolewa kwa mujibu wa sheria hizo, sikumbuki ni adhabu yenye ukubwa kiasi gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali lake la pili, ni Mkoa gani ambao unaongoza; Mkoa wa Dar es Salaam unaongoza kwa kuwa na wagonjwa wengi kuliko mikoa yote, ukifuatiwa na majiji mengine na sasa Serikali inachukua hatua gani kuwasaidia watu ambao wameathirika na dawa za kulevya. Mikakati tuliyonayo ni kama hii ya kuanzisha kliniki za kutoa dawa ya methadone. Hii dawa ya methadone inasaidia sana kwa wagonjwa kuacha kutumia hizi opioids kwa sababu methadone na yenyewe ni katika group hilo hilo la opioids, lakini uzuri wa methadone haisababishi utegemezi kama zile dawa nyingine. Kwa sababu dawa hizo nyingine kama heroin na cocaine zinasababisha utegemezi ambapo utegemezi ule unaweza ukaondolewa na dawa nyingine ambayo inafanya replacement ya dawa zile, kwa hiyo, mtu anaweza akaacha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hilo ni la kwanza, lakini la pili, ni kuwasaidia kwenye shughuli mbalimbali za kurudi kwenye jamii, kama kushiriki kwenye ufundi na kuwapa mafunzo mbalimbali, ili waweze kuwa intergrated kwenye jamii.

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Vijana wengi walioathirika na dawa za kulevya wanaleta kero kubwa ndani ya jamii, kutengwa na wazazi wao na kukosa msaada wa kifedha pale wanapoamua kuacha na kujiunga na kituo cha tiba. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa matibabu bure kwa vijana hao ili warudi katika hali zao za kawaida na hatimaye kuendelea na ujenzi wa Taifa?

Supplementary Question 2

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nichukue nafasi hii kuwapa pole wananchi wangu waliopotea na chombo baharini, leo ni wiki hawajaonekana, niwaombee Mwenyezi Mungu awajalie kama bado wako hai awafanyie wepesi na kama wamefariki awaweke pema peponi, Amina.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naiona azma nzuri ya Serikali katika kupambana na dawa za kulevya; na ninaisifu sana, naipongeza Wizara hii kwa usimamizi mzuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kukinga ni bora kuliko kutibu, kwa muda mrefu imesemekana na ni ukweli usioshaka kwamba, Zanzibar imekuwa ni lango kuu la kupitisha dawa za kulevya. Tumeona juhudi ya Serikali pale inapowaonea huruma wananchi wake wa Zanzibar katika mambo tofauti mbalimbali yanapojitokeza. Je, ni lini Serikali itachukua kwa makusudi jitihada za kuiweka Zanzibar katika uangalizi maalum wa kukomesha kuwa corridor muhimu ya kupitisha dawa za kulevya ambazo uingiaji wake na matumizi yake makubwa inakuwa ni hapa Tanzania Bara?Ni lini Serikali itaonesha kujali na kuchukua hatua madhubuti kukomesha janga la Zanzibar kuendelea kuwa uchochoro wa dawa za kulevya? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niungane na yeye kumpa pole juu ya wananchi wake waliopotea na boti.
Lakini la pili, jibu lake kwenye swali lake ni kwamba nakubaliana na yeye Zanzibar kwa muda mrefu imekuwa ni corridor ya dawa za kulevya, lakini kwenye mikakati ya kupambana na dawa za kulevya kuna maeneo mawili; kuna supply reduction na kuna demand reduction, kwa hiyo, kwenye supply reduction wenzetu wa Tume ya Dawa za Kulevya ambayo inaongozwa na Kamishna Siang’a wanaongoza mapambano kweye eneo hilo na mikakati yao zaidi ni ya kiintelijensia na mambo mengi wanayoyafanya hayasemwi hovyo hovyo. (Makofi)
Kwa hivyo, nikuhakikishie tu Mheshimiwa Khatib, Tume kwa sasa kwa kweli imepunguza sana supply ya dawa za kulevya kwenye nchi yetu, ikiwemo kule Zanzibar. Na hilo wala halina shaka na huo mfereji unaousema kwa hakika kwa sasa umezibwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kwenye demand ni kutoa tiba na kuwasaidia kwenye impact reduction. (Makofi)

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Vijana wengi walioathirika na dawa za kulevya wanaleta kero kubwa ndani ya jamii, kutengwa na wazazi wao na kukosa msaada wa kifedha pale wanapoamua kuacha na kujiunga na kituo cha tiba. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa matibabu bure kwa vijana hao ili warudi katika hali zao za kawaida na hatimaye kuendelea na ujenzi wa Taifa?

Supplementary Question 3

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Naipongeza Serikali kwa jitihada zake za kupambana na dawa za kulevya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa mara ya pili tena.
Ni kwamba naipongeza Serikali kwa jitihada zake.
Na vijana hawa wanapoathirika na hizi dawa za kulevya moja kwa moja tayari wanaingia katika kundi letu, kwa maana ya kundi la watu wenye ulemavu. Na kwa sababu wimbi ni kubwa kwa hivi sasa, je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba inaongeza Madaktari Bingwa kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa hawa walioathirika na dawa za kulevya? Ahsante.

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nijibu maswali haya mawili, Mheshimiwa Waziri wa Nchi atamalizia kwa ujumla yanayohusu supply reduction.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye eneo la kwanza la Mheshimiwa Amina Mollel, kwanza nimpongeze siku ya jana aliniletea wageni kutoka Chama cha Wananchi ambao wanajihusisha na Afya ya Akili Nchini na katika mazungumzo tuliyoyafanya ni pamoja na hili suala la Madaktari Bingwa wa Afya ya Akili kwenye Mikoa nchini. Mkakati tulionao na ndio taarifa niliyowapa wale wananchi wenzetu ni kwamba Serikali ina-scale up huu mkakati wa kuwa na hizi kliniki kama iliyopo Muhimbili, Temeke na Mwananyamala kwa mwaka huu kwenye mikoa kumi ya Tanzania Bara na kwa mwaka ujao tutaongeza mikoa mingine kumi, tunakwenda kwa awamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, kila tutakapoanzisha hii kliniki ya methadone ni lazima awepo Daktari Bingwa anayehusika na ku-administrate hiyo dawa kwa sababu methadone inalindwa kwa taratibu maalum za kuitunza na kuitoa kwa wagonjwa. Kwa hiyo, ni lazima awepo Daktari Bingwa anayeweza kufanya hivyo kwa hivyo, kwa mwaka huu nimhakikishie Mheshimiwa Amina Mollel kwamba tutakuwa na Madaktari Bingwa kwenye mikoa kumi ncjini, pindi kliniki za methadone zitakapoanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ni la Mheshimia Ritta Enespher Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kuhusu hizi kliniki na rehabilitation centres kwenye Mikoa; kwa sasa kweli, tuko Dar es Salaam peke yake, lakini kwenye mkakati wetu tunakwenda kwenye mikoa kumi kama nilivyosema. Na kwenye kila kanda tunakwenda kuanzisha rehabilitation centre ambapo tutakuwanazo nne sasa katika nchji nzima. Kwa hivyo, hii ni mikakati ambayo tunayo katika siku za usoni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ruzuku, Serikali haina utaratibu wa kutoa ruzuku kwenye taasisi mbalimbali za binafsi, kwa sababu wao wanafanya kwa hiyari na tunawaomba na kuwatia moyo waendelee kufanya hivyohivyo kwa hiyari, lakini sisi kama Serikali tuna mikakati yetu ya kuwasaidia wenzetu ambao wameathirika na dawa za kulevya.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninaomba nijibu maswali ya nyongeza yaliyoulizwa kwa umoja wake, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwanza nianze kumpongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya, kwa majibu mazuri aliyokwishakuyatoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze tena kwa kulipongeza Bunge letu Tukufu kwa sababu mwaka 2015, ndilo lililosababisha kufanyika kwa mageuzi makubwa ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini kwa kutungwa kwa sheria mpya ambayo imeunda hiyo mamlaka sasa ambayo tumemuona Kamishna Jenerali akifanya kazi kubwa sana kwa kushirikiana na makamishna wenzake kuhakikisha kwamba tunapambana na tatizo la dawa za kulevya nchini.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niliarifu Bunge
lako Tukufu Kamishna Jenerali baada ya kuteuliwa na mamlaka kuanza kazi rasmi, ameshahakikisha ametengeneza Mpango Mkakati Maalum wa Taifa wa kuhakikisha kwamba tatizo hili la dawa za kulevya nchini linaondoka. Na mpango mkakati huo unashirikisha pande zote mbili za Muungano, upande wa Zanzibar na upande wa huku Bara. Kwa hiyo, Mheshimiwa Khatib wala usiwe na wasiwasi, tunafanya kazi hizi kwa pamoja, vyombo hivi vyote viwili vinafanya kazi kwa pamoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumegundua kwamba, wenzetu wa private sector wanafanya kazi nzuri sana kwenye mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini. Na hivyo nichukue nafasi hii kwanza niwapongeze wale wote ambao wameamua kujitolea kusaidiana na Serikali katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya katika nchi yetu ya Tanzania, tunawashukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika mwaka huu wa bajeti, Ofisi ya Waziri Mkuu imeamua kuweka bajeti kidogo ambayo itasaidia kushirikiana na hao wenzetu ambao wameonesha kwamba, wana nia ama ya kuanzisha sobber houses kwa ajili ya kuwasaidia hawa walioathirika na dawa za kulevya, lakini vilevile kufanya kampeni na kuleta uhamasishaji mkubwa wa kuwasaidia vijana wetu kuwaondoa kwenye tatizo hili.
Kwa hiyo, tuko pamoja tunafanya kazi hii kwa pamoja, mapambano yanaendelea na tunataka kuona kwamba tunaondoa tatizo hili katika nchi yetu. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:- Vijana wengi walioathirika na dawa za kulevya wanaleta kero kubwa ndani ya jamii, kutengwa na wazazi wao na kukosa msaada wa kifedha pale wanapoamua kuacha na kujiunga na kituo cha tiba. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa matibabu bure kwa vijana hao ili warudi katika hali zao za kawaida na hatimaye kuendelea na ujenzi wa Taifa?

Supplementary Question 4

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, Mheshimiwa Waziri alipokuwa anajibu majibu yake alisema kwamba, kwenye miji mikubwa kuna hiyo huduma inatolewa, lakini ukija kwenye miji midogo kwa mfano Iringa kuna vijana wengi sana wameathirika. Lakini tumshukuru sana Dkt. Ngala pale Iringa, ameweza kuhamasisha wananchi wamefungua vituo kama hivi, lakini sasa wananchi wanashindwa gharama imekuwa kubwa sana kwenda kwenye vituo.
Sasa je, Serikali iko tayari kutoa ruzuku kwa watu ambao wamenzisha vituo hivi ili viweze kusaidia kwenye miji midogo kama Iringa?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nijibu maswali haya mawili, Mheshimiwa Waziri wa Nchi atamalizia kwa ujumla yanayohusu supply reduction.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye eneo la kwanza la Mheshimiwa Amina Mollel, kwanza nimpongeze siku ya jana aliniletea wageni kutoka Chama cha Wananchi ambao wanajihusisha na Afya ya Akili Nchini na katika mazungumzo tuliyoyafanya ni pamoja na hili suala la Madaktari Bingwa wa Afya ya Akili kwenye Mikoa nchini. Mkakati tulionao na ndio taarifa niliyowapa wale wananchi wenzetu ni kwamba Serikali ina-scale up huu mkakati wa kuwa na hizi kliniki kama iliyopo Muhimbili, Temeke na Mwananyamala kwa mwaka huu kwenye mikoa kumi ya Tanzania Bara na kwa mwaka ujao tutaongeza mikoa mingine kumi, tunakwenda kwa awamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, kila tutakapoanzisha hii kliniki ya methadone ni lazima awepo Daktari Bingwa anayehusika na ku-administrate hiyo dawa kwa sababu methadone inalindwa kwa taratibu maalum za kuitunza na kuitoa kwa wagonjwa. Kwa hiyo, ni lazima awepo Daktari Bingwa anayeweza kufanya hivyo kwa hivyo, kwa mwaka huu nimhakikishie Mheshimiwa Amina Mollel kwamba tutakuwa na Madaktari Bingwa kwenye mikoa kumi ncjini, pindi kliniki za methadone zitakapoanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ni la Mheshimia Ritta Enespher Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kuhusu hizi kliniki na rehabilitation centres kwenye Mikoa; kwa sasa kweli, tuko Dar es Salaam peke yake, lakini kwenye mkakati wetu tunakwenda kwenye mikoa kumi kama nilivyosema. Na kwenye kila kanda tunakwenda kuanzisha rehabilitation centre ambapo tutakuwanazo nne sasa katika nchji nzima. Kwa hivyo, hii ni mikakati ambayo tunayo katika siku za usoni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ruzuku, Serikali haina utaratibu wa kutoa ruzuku kwenye taasisi mbalimbali za binafsi, kwa sababu wao wanafanya kwa hiyari na tunawaomba na kuwatia moyo waendelee kufanya hivyohivyo kwa hiyari, lakini sisi kama Serikali tuna mikakati yetu ya kuwasaidia wenzetu ambao wameathirika na dawa za kulevya.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninaomba nijibu maswali ya nyongeza yaliyoulizwa kwa umoja wake, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwanza nianze kumpongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya, kwa majibu mazuri aliyokwishakuyatoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze tena kwa kulipongeza Bunge letu Tukufu kwa sababu mwaka 2015, ndilo lililosababisha kufanyika kwa mageuzi makubwa ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini kwa kutungwa kwa sheria mpya ambayo imeunda hiyo mamlaka sasa ambayo tumemuona Kamishna Jenerali akifanya kazi kubwa sana kwa kushirikiana na makamishna wenzake kuhakikisha kwamba tunapambana na tatizo la dawa za kulevya nchini.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niliarifu Bunge
lako Tukufu Kamishna Jenerali baada ya kuteuliwa na mamlaka kuanza kazi rasmi, ameshahakikisha ametengeneza Mpango Mkakati Maalum wa Taifa wa kuhakikisha kwamba tatizo hili la dawa za kulevya nchini linaondoka. Na mpango mkakati huo unashirikisha pande zote mbili za Muungano, upande wa Zanzibar na upande wa huku Bara. Kwa hiyo, Mheshimiwa Khatib wala usiwe na wasiwasi, tunafanya kazi hizi kwa pamoja, vyombo hivi vyote viwili vinafanya kazi kwa pamoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumegundua kwamba, wenzetu wa private sector wanafanya kazi nzuri sana kwenye mapambano dhidi ya dawa za kulevya nchini. Na hivyo nichukue nafasi hii kwanza niwapongeze wale wote ambao wameamua kujitolea kusaidiana na Serikali katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya katika nchi yetu ya Tanzania, tunawashukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika mwaka huu wa bajeti, Ofisi ya Waziri Mkuu imeamua kuweka bajeti kidogo ambayo itasaidia kushirikiana na hao wenzetu ambao wameonesha kwamba, wana nia ama ya kuanzisha sobber houses kwa ajili ya kuwasaidia hawa walioathirika na dawa za kulevya, lakini vilevile kufanya kampeni na kuleta uhamasishaji mkubwa wa kuwasaidia vijana wetu kuwaondoa kwenye tatizo hili.
Kwa hiyo, tuko pamoja tunafanya kazi hii kwa pamoja, mapambano yanaendelea na tunataka kuona kwamba tunaondoa tatizo hili katika nchi yetu. (Makofi)