Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:- Mwaka 2012/2013 Serikali ilichukua ardhi ya wananchi wa Mtwara Mjini eneo la Mji Mwema na Tangira. Aidha, Serikali imewazuia wananchi hao kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo hayo. Serikali iliahidi kuwalipa wananchi hao fidia lakini hadi sasa fidia hiyo haijalipwa. Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa wananchi wao?

Supplementary Question 1

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Ahsante Mheshimiwa Mwenyekiti naomba kwa namna ya kipekee nishukuru kwa sababu suala hili la ulipaji wa maeneo haya fidia hii ni suala la muda mrefu sana kwa kuwa Wizara hii ya TAMISEMI na Wizara ya Ardhi imekubali sasa kulimaliza suala hili tunashukuru kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Mtwara Mjini, lakini hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, nilikuwa naomba kujua sheria inatueleza kwamba kwa kuwa maeneo haya yamechukuliwa mwaka 2012/2013 ni muda mrefu hivi sasa wananchi wale wamekosa maeneo ya kulima na kufanya shughuli zao za kimaendeleo, je, Serikali ipo tayari kulipa pamoja na fidia ya nyongeza?
Swali la pili, kwa kuwa ahadi hii ya kuwalipa wananchi hawa Jimbo la Mtwara Mjini ni la muda mrefu, je Mheshimiwa Waziri yupo tayari kulithibitishia Bunge hili kwamba wananchi wa Mtwara Mjini wa maeneo haya ya Mji mwema na Tangira kwamba tarehe hizo walizotaja ni kweli wataenda kulipa fidia? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Mbunge kulifuatilia hili jambo kwa sababu ni haki za wananchi wako kwa hiyo commitment yako kwa wananchi wako imekuwa vizuri, lakini jambo la pili, utaratibu wa malipo ya fidia ni kwamba mara baada ya tathimini ikishafanyika ikipita miezi sita maana yake malipo yanatakiwa yalipwe ndani ya miezi sita; ikipita miezi sita lazima kuna malipo ya nyongeza yatafanyika. Kwa hiyo, naomba nikuhakikishie kwamba Wananchi haki zao zitalindwa kulingana na muda uliocheleweshwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala la pili kwamba commitment ya Serikali sasa itaenda kulipa hili nimezungumza hapo awali kwamba kilicho chelewesha mwanzo kutokana na Bodi ilikuwa haijaundwa na bahati nzuri sasa bodi imeshaundwa na ndio maana sisi ofisi yetu ina jukumu la kutoa kibali tumeshatoa kibali. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba uondoe hofu kwamba wananchi wa Mtwara leo hii wananisikiliza live kupitia vyombo vya habari kwamba Serikali imejipanga katika hili na itaenda kutekeleza kwa kadri mipango yote ilivyowekwa vizuri kupitia Halmashauri yenyewe.

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:- Mwaka 2012/2013 Serikali ilichukua ardhi ya wananchi wa Mtwara Mjini eneo la Mji Mwema na Tangira. Aidha, Serikali imewazuia wananchi hao kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo hayo. Serikali iliahidi kuwalipa wananchi hao fidia lakini hadi sasa fidia hiyo haijalipwa. Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa wananchi wao?

Supplementary Question 2

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru kwa kunipa nafasi, kwanza naipongeza Serikali kurudisha Ardhi ya Dodoma mikononi mwa wananchi yaani Baraza la Madiwani. (Makofi)
Kwa kuwa CDA imevunjwa na ndio mamlaka iliyokuwa na madaraka juu ya ardhi ya Dodoma na wakati inavunjwa wapo wananchi ambao walishapata barua za kumiliki ardhi, lakini walikuwa hawajaonyeshwa maeneo yao na wapo wananchi ambao wanalipa kidogo kidogo pale CDA, je, Serikali imeweka utaratibu gani wa dharura wa kuhakikishwa kwamba wananchi wa Manispaa ya Dodoma wanahudumiwa wakati taratibu zingine zinaendelea?(Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tunashukuru kwa Mheshimiwa Mbunge ku- recognize kwamba kilio cha wananchi wa Dodoma katika hilo, lakini jambo la pili government works on papers, hakuna haki mtu itayopotea. Kwa hiyo, Serikali itaandaa utaratibu wowote ambao unawezekana na kikosi kazi kwa mujibu Serikali itakavyokuwa imejipanga naomba muondoe hofu kwamba Ofisi ya Rais, Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo jambo hili inaisimamia vizuri tutakuja kutoa taarifa hapa iliyokuwa rasmi juu ya jinsi gani jambo hili linatekelezeka na wananchi wote wa Dodoma wasiwe na hofu kila jambo litakuwa limewekwa vizuri kwa utaratibu wa Kiserikali.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Ahsante Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa majibu ya nyogeza kwa niaba Waziri wa Ofisi ya Rais -TAMISEMI kuhusiana na swali lililoulizwa na Mheshimiwa Bura kama ifuatavyo:-
Naomba niwahakikishie wananchi wa Dodoma kwamba mbali na kuvunjwa na CDA huduma zote za ardhi zinaendelea chini ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma na watumishi waliokuwa wakifanya kazi sekta ile wapo ambao wataendelea na kazi hiyo na wale ambao walikuwa wamelipia nusu ya maeneo yao wataendelea na utaratibu huo mpaka pale watakapokamilisha kulingana na makubaliano waliopeana awali.
Aidha, wale wote ambao wana zile hati ambao si
hati miliki ambazo tunazitambua kutakuwa na utaratibu wa kubadilishiwa na kupewa zile hati ambazo watapewa muda wa miaka 99 kuanzia pale alipopewa awali. Kwa hiyo, wasiwe na hofu Wizara imejipanga vizuri na kila mmoja atapata haki yake kadri utaratibu wa ofisi ilivyopanga.(Makofi)

Name

Halima Ali Mohammed

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:- Mwaka 2012/2013 Serikali ilichukua ardhi ya wananchi wa Mtwara Mjini eneo la Mji Mwema na Tangira. Aidha, Serikali imewazuia wananchi hao kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo hayo. Serikali iliahidi kuwalipa wananchi hao fidia lakini hadi sasa fidia hiyo haijalipwa. Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa wananchi wao?

Supplementary Question 3

MHE. HALIMA ALI MOHAMMED: Ahsante, Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri swali moja.
Mheshimiwa Waziri kwa kuwa suala la Mtwara linafanana sana na suala la Halmashauri ya Kisarawe kata ya Kibongwa, wananchi wamechukuliwa ardhi yao, ikakatwa viwanja, lakini wao hawakupatiwa viwanja wala hawakupatiwa fidia yoyote ile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Mheshimiwa Waziri ni lini wanmanchi wa jimbo lako hili watapatiwa haki yao ya fidia?(Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli viwanja vilipimwa toka mwaka 2005 na ni kweli baadhi ya wananchi walichukuliwa eneo, lakini suala zima la mchakato wa fidia lilikuwa halijalipwa na ndio maana katika kulinda haki za wananchi tulisema hata vile viwanja vya mwanzo watu walitakiwa wapewe na wengine miongoni mwenu ni Wabunge humu ndani, tulivizuia kwamba watu wasipate vile viwanja mpaka wananchi wa pale wapate haki zao.
Kwa hiyo, jambo hili chini ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri linashughulikiwa vizuri na kila mtu atapata haki yake stahiki kwa sababu jambo hili viongozi tumelisimamaia kulinda haki za wananchi wetu.