Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza:- Kumekuwa na matukio ya mara kwa mara ya ujambazi na unyang’anyi wa kutumia silaha ndani ya Mji wa Bunda na wahanga wa matukio hayo ni wafanyabiashara wadogo wadogo. Je, ni hatua zipi za kiusalama zimechukuliwa ili kukabiliana na wimbi la ujambazi na unyang’anyi katika Mji wa Bunda?

Supplementary Question 1

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, Mwenyekiti wangu wa zamani wa vijana.
Mheshimiwa Spika, kama ilivyo kwenye majibu yake, anasema moja ya mikakati ni kuhakikisha wanafanya doria imara; ni jambo zuri kabisa. Sasa huwezi kufanya doria imara kama huna magari mazuri.
Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Bunda kuna magari mawili na mabovu na ndiyo ambayo yanatakiwa yafanye doria kwenye Jimbo la Kangi na Jimbo la Boni. Sasa uhalifu unazidi kuongezeka.
Mheshimiwa Spika, maswali yangu, katika kuhakikisha
hiyo doria imara kama Mheshimiwa Waziri amejibu, je, Serikali iko tayari sasa kutupatia gari jipya ili kupunguza vitendo vya uhalifu kwa kufanya hiyo doria imara? (Makofi)
Swali la pili, ili kuweza kukabiliana na hizi changamoto, moja ya vituo ambavyo vipo hohehahe ni Kituo cha Polisi cha Bunda. Sasa wameanza mradi wa ujenzi wa jengo la upelelezi kupitia michango ya polisi, ya wadau, nami Mbunge wa Jimbo kupitia Mfuko wa Jimbo nimewachangia. Serikali mpo tayari kuungana na jitihada zetu kukamilisha jengo hilo? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala la magari, naomba nichukue nafasi hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tumepokea changamoto yake ya magari. Wakati ambapo magari yatapatikana tutatoa kipaumbele kwa Jimbo lake ili tumpatie gari la ziada ili aweze kuongeza nguvu ya yale magari machache yaliyopo sasa hivi.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ni suala la ujenzi
wa kituo cha upelelezi. Kwanza nachukua fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kuamua kutoa fedha za Mfuko wake wa Jimbo kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha polisi. Natambua kwamba Mfuko wa Jimbo una fedha kidogo na Majimbo yetu yanachangamoto nyingi. Kwa hiyo, kitendo cha Mheshimiwa Mbunge kuamua kwamba sehemu ya fedha hizo ziende kwenye ujenzi wa vituo vya polisi ambavyo vina changamoto kubwa ni jambo la kupongezwa na kuungwa mkono. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Ester kwamba jitihada zake pamoja na za wananchi zimezaa matunda, kituo hicho kimekamilika, tunatarajia wakati wowote mwaka huu tutakizindua. (Makofi)

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza:- Kumekuwa na matukio ya mara kwa mara ya ujambazi na unyang’anyi wa kutumia silaha ndani ya Mji wa Bunda na wahanga wa matukio hayo ni wafanyabiashara wadogo wadogo. Je, ni hatua zipi za kiusalama zimechukuliwa ili kukabiliana na wimbi la ujambazi na unyang’anyi katika Mji wa Bunda?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa matukio ya Bunda yanazidi kuwa mengi kidogo, ni lini sasa Waziri au Naibu Waziri atatembelea Bunda ili kuona hali halisi ya mambo hayo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimuahidi kwamba tutashauriana na Mheshimiwa Waziri ili kati yangu ama yeye tuweze kwenda Bunda haraka iwezekanavyo. Tutakaa pamoja tushaurine ratiba hiyo ya kutembelea Bunda muda siyo mrefu sana. (Makofi)

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza:- Kumekuwa na matukio ya mara kwa mara ya ujambazi na unyang’anyi wa kutumia silaha ndani ya Mji wa Bunda na wahanga wa matukio hayo ni wafanyabiashara wadogo wadogo. Je, ni hatua zipi za kiusalama zimechukuliwa ili kukabiliana na wimbi la ujambazi na unyang’anyi katika Mji wa Bunda?

Supplementary Question 3

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Matatizo ya usalama katika eneo la Bunda yanafanana sana na Jimbo langu la Mji wa Tunduma.
Mwaka 2016 katika swali langu la msingi, niliuliza kuhusiana na ujenzi wa kituo chenye hadhi ya Wilaya, lakini pia niliuliza kuhusiana na nyumba zenye gharama nafuu kwa ajili ya polisi wetu kwenye Mji wa Tunduma. Majibu yake ni kwamba walisema katika Bajeti ya mwaka 2016/2017 nyumba hizi zingeweza kujengwa pamoja na Kituo cha Polisi chenye hadhi ya Wilaya. Je, Serikali inasema nini kuhusiana na changamoto hizi katika mji wetu wa Tunduma? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nakiri kabisa kwamba Jimbo la Tunduma lipo mpakani na lina changamoto nyingi sana za kiusalama. Kwa hiyo, mahitaji ya kuwa na kituo cha polisi cha kisasa pamoja na nyumba za askari ni mambo ya kipaumbele.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi hiyo iliyotolewa na Serikali iko pale pale na hatua ambazo zitafikiwa tutamjulisha kwa kadri ambavyo upatikanaji wa fedha utakavyokuwa unaruhusu.