Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saumu Heri Sakala

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAUMU H. SAKALA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza magari yaliyopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Pangani kwa haraka kutokana na uhaba wa magari unaosababishwa na ubovu wa magari?

Supplementary Question 1

MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ambayo nimepata kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini ningependa kumweleza kuwa Hospitali ya Wilaya ya Pangani ina magari mawili tu kati ya hayo magari 11 ambayo umeyataja, lakini magari yale ni chakavu mno kiasi kwamba yanapoenda service basi yanalazimika kutengeneza kitu zaidi ya kimoja yaani sio service tu ya kawaida, lazima unakuta na vitu vingine vinakuwa vimeharibika pale.
Mheshimiwa Spika, Serikali pengine haioni umuhimu wa kununua magari mengine mapya badala ya kuacha magari yale chakavu yaendelee kutumikia Hospitali ya Wilaya ya Pangani? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, ni kweli, na mimi nilivyofika Pangani, Mheshimiwa Mbunge anakumbuka nimefika pale nimeona changamoto hii ya magari. Magari yale ni kweli ni miongoni mwa magari chakavu kama ilivyo katika Halmashauri nyingine. Nikijua wazi kwamba kipaumbele cha kununua magari ya Halmashauri huwa yanafanywa hasa na Halmashauri yenyewe ikianzia katika mchakato wa awali. Hata hivyo, Serikali katika kuimarisha huduma ya afya, tulinunua karibu magari 50 tukapeleka katika maeneo ambayo vipo vifo vingi zaidi. Hata hivyo tuna mkakati mwingine, tukipata gari la ziada tutafanya hivyo.
Mheshimiwa Spika, suala la ununuzi wa magari naomba watu wa Halmashauri ya Pangani tuweke kipaumbele, lakini Serikali haitasita kusaidia wananchi wa Pangani tukijua wazi Jimbo lile na eneo lile jiografia yake iko tata sasa; ukitoka pale Hospitali watu wa Mwela huku na watu wa upande mwingine wana changamoto kubwa sana mpaka kwenda eneo lile.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Serikali tunaliangalia hilo, lakini tutashirikiana vyema na wenzetu wa Pangani kuhakikisha mambo yao yanaenda vizuri. (Makofi)

Name

Suleiman Ahmed Saddiq

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. SAUMU H. SAKALA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza magari yaliyopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Pangani kwa haraka kutokana na uhaba wa magari unaosababishwa na ubovu wa magari?

Supplementary Question 2

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Spika, naomba nami niulize swali moja dogo la nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Waziri umetembelea Wilaya ya Mvomero na umejionea mwenyewe hali halisi ya Wilaya; leo gari la afya ambalo linatumika kwa ajili ya chanjo ndilo linatumika kwa ajili ya kukusanya mapato, lakini Idara ya Ujenzi haina gari, magari yote ni chakavu.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kutusaidia sisi watu wa Mvomero ili tuweze kuendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, anachosema ni kweli. Siku ya Alhamisi tulikuwa Jimboni kwake pale na tulitembelea mpaka Hospitali ya Wilaya na kubaini changamoto na jiografia ya eneo lile kuanzia Turiani na maeneo mengine.
Mheshimiwa Spika, eneo lile ni kweli, hata nilipokutana
na wataalam pale, kuna changamoto ya magari. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama nilivyosema pale awali ni kwamba mchakato wa ununuzi wa magari mara nyingi sana unaanza na kipaumbele cha Halmashauri yenyewe, lakini kwa sababu tuko pamoja hapa na Mbunge siku ile tulikubaliana mambo mengine ya msingi. Tutaendelea kushirikiana vya kutosha kuona ni jinsi gani tutaiwezesha Halmashauri ya Mvomero iweze kufanya vizuri. Ndiyo maana Serikali hata katika suala zima la miundombinu, wewe unafahamu jinsi tunavyowekeza pale hata katika ujenzi wa lami. Lengo kubwa ni kwamba wananchi wa Mvomero wapate matunda mazuri ya Mbunge wao.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itashirikiana naye, pale kwenye mahitaji ya haraka tutafanya kwa ajili ya wananchi wake na watendaji waweze kufanya kazi vizuri katika Jimbo la Mvomero.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kutumia Bunge hili kupiga marufuku magari ya chanjo kutumika kwa shughuli tofauti na chanjo. Kuanzia sasa hivi magari ya chanjo tutayandika herufi kubwa neno “CHANJO” na lisitumike kwa matumizi mengine yoyote. Kwa sababu chanjo ni muhimu kuliko masuala mengine katika Halmashauri.
Mheshimiwa Spika, niliona nitumie Bunge lako kutoa ufafanuzi. Kwa hiyo, ni marufuku Halmashauri ya Mvomero kutumia gari la chanjo kwa ajili ya kukusanyia mapato. Ahsante.

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAUMU H. SAKALA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza magari yaliyopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Pangani kwa haraka kutokana na uhaba wa magari unaosababishwa na ubovu wa magari?

Supplementary Question 3

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, Bukoba Vijijini ni Wilaya ambayo
ina jiografia kubwa na magari ya Bukoba Vijijini yote hasa ya hospitali ni mabovu. Juzi imetolewa ambulance, badala ya kupelekwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Izimbya ikapelekwa kwenye Zahanati ya Kishanji. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri ndivyo mlivyopanga au ni mipango ya Halmashauri?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, tumelisikia hili. Kama alivyosema Mheshimiwa Waziri wa Afya, lengo letu kubwa ni kwamba haya magari ya chanjo yakienda katika maeneo yafanye kazi inayokusudiwa. Sasa kwako wewe kuna scenario tofauti kwamba gari lilitakiwa liende katika hospitali lakini limeenda katika zahanati, lakini ninachoamini ni kwamba kule kuna DMO, viongozi na Mkurugenzi pale, inawezekana kuna jambo ambalo tutaenda kulifanyia kazi tujue nini kilichoendelea.
Mheshimiwa Spika, letu kubwa ni kuhakikisha tunazozipeleka resources na hasa katika sekta ya afya, lazima watu wasimamie mwongozo huu. Gari kama ni la afya litumike kwa ajili ya afya. Ndiyo maana sasa hivi mikoa mingine hata kiwango cha chanjo wanashuka kumbe ni kwa sababu hawazingatii miongozo maalum ya Serikali ambayo tunaelekeza kila siku.