Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA Aliuliza:- Majanga ni mambo yasiyotarajiwa ila huwa yanatokea tu, majanga kama ajali za baharini, ziwani, barabarani, matetemeko, vimbunga, majanga ya njaa na kadhalika yamekuwa yakitokea:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha na kuimarisha nyenzo na ujuzi kwa Kikosi cha Uokoaji wa Majini kinachojulikana kama Coast Guard kwa ajili ya uokoaji?

Supplementary Question 1

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri ila nina maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, kwa kuwa nyendo zimekuwa nyingi, watu wanakwenda sana kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa ajili ya kiuchumi na mengineyo, kwa hiyo ajali za majini, baharini na kwenye maziwa yawezekana zikatokea. Serikali imejipanga hivi ilivyojipanga; Je, Serikali inaonesha vipi shughuli zinazofanywa na SUMATRA na kule Zanzibar, kwa sababu bado ajali zitakuwa zinatokea tunafanyaje?
Swali la pili; Serikali ina mpango gani kwa wale waliopatwa na msiba na kupoteza ndugu zao wakati ilipopata tatizo MV Bukoba, MV Spice Islander iliyozama kule Nungwi na ajali nyingine. Je, watu wote hawa wameshalipwa fidia zao?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mahusiano ya MRCC na upande wa Zanzibar, naomba nimhakikishie kwamba MRCC ni ya masuala ya Muungano na yanasimamiwa na SUMATRA, kwa hiyo Zanzibar Maritime Authority watashirikiana na taasisi yetu katika kusimamia hii MRCC iweze kuhudumia pande zote za Muungano mara ajali inapotekea.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili nimuombe tu Mheshimiwa Asha Juma kwamba ajali ya MV Bukoba na ajali nyingine zote zimeshughulikiwa na Serikali kwa kiwango kikubwa sana, maadam sina takwimu hapa nisingeweza kumpa undani wa nini kilifanyika, lakini ni masula ambayo yalishughulikiwa na Idara yetu ya maafa iliyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ukamilifu kabisa.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA Aliuliza:- Majanga ni mambo yasiyotarajiwa ila huwa yanatokea tu, majanga kama ajali za baharini, ziwani, barabarani, matetemeko, vimbunga, majanga ya njaa na kadhalika yamekuwa yakitokea:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha na kuimarisha nyenzo na ujuzi kwa Kikosi cha Uokoaji wa Majini kinachojulikana kama Coast Guard kwa ajili ya uokoaji?

Supplementary Question 2

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza. Ni dhahiri kwamba Watanzania wengi wanapoteza maisha katika bahari au katika maziwa zinapotokea ajali na ni ukweli uliowazi kwamba hatuna wataalam wa uokozi wa kutosha kama divers ndani ya nchi yetu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha kikosi kazi chenye wataalam kama divers na wakiwa na zana za kisasa za uokoaji ili kuepusha ajali zinazotokea na kuokoa maisha ya watu wetu?
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:
Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania tuna kikosi maalum kwa ajili ya uokoaji kama kumetokea ajali, kikosi hicho kinashirikisha pamoja na Jeshi la Wananchi, Marine Police, SUMATRA na wadau wengine mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kawaida ajali ikitokea baharini chombo kinatakiwa kipeleke signal maalum ambayo tunaita distressing signals, signal hiyo ikipelekwa meli zote zilizopo zinakwenda kusaidia kuokoa kwa sababu ukisubiri wewe mpaka wataalam watoke Dar es Salaam na meli imetokea pengine kilometa 200 ulipo itakuwa ni too late. Kwa ufupi tu tuna vikosi maalum ambavyo ikitokea tu vikosi hivyo vinakwenda na vinafanya kazi hiyo. Kwanza Polisi, Jeshi la Wanamaji na Zanzibar kuna KMKM na wataalam wengine wapo ili kuhakikisha kwamba tunawasaidia wale wanaopata ajali.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutaendelea kama Serikali kuwaimarisha hawa kiutaalam ili waweze kufanya kazi na teknolojia za kisasa za uokoaji.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA Aliuliza:- Majanga ni mambo yasiyotarajiwa ila huwa yanatokea tu, majanga kama ajali za baharini, ziwani, barabarani, matetemeko, vimbunga, majanga ya njaa na kadhalika yamekuwa yakitokea:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha na kuimarisha nyenzo na ujuzi kwa Kikosi cha Uokoaji wa Majini kinachojulikana kama Coast Guard kwa ajili ya uokoaji?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Ziwa Victoria kumekuwa na meli nyingi ambazo zimekuwa zikisaidia wananchi kubeba mizigo na abiria kwenda Ukerewe na nchi za jirani. Hivi sasa ni meli moja tu inayotembea MV Umoja imepaki, MV Serengeti imepaki, inayotembea ni MV Clarias peke yake. Wananchi wanaoenda visiwani hasa Ukerewe wanatumia feri za mizigo, sasa za kwetu zimeharibika, sina hakika kama Wizara imeshindwa kukarabati zile feri ama watumishi walioko kule wanafanya mipango na wale watu wenye maferi. Nataka kujua kwa Waziri ni lini feri hizi zitaanza ku-operate kwa muda muafaka?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tunazo meli ambazo zimesimama kwa sababu ya kuharibika ikiwa ni pamoja na MV Umoja na MV Serengeti na hata hii MV Clarias siyo muda mrefu sana imekarabatiwa ni karibuni tu imeanza kutoa hiyo huduma, nayo ilikuwa imeharibika.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti iliyopita ya 2016/2017, tulitenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa meli za Ziwa Victoria, nimhakikishie pamoja na kwamba taratibu za kumpata mtu wa kuweza kufanya hiyo kazi zimeshakamilika, muda siyo mrefu kazi hiyo itaanza na kazi hiyo itakapokamilika meli hizo zitarudi majini. Aidha, tuna mpango wa muda mrefu wa kujenga meli mpya itakayohudumia Ziwa Victoria na maziwa mengine Tanganyika na Nyasa, kwa Nyasa tumeshakamilisha ili kuhakikisha kwamba meli hizo ambazo zimefanya kazi muda mrefu sana katika maziwa hayo zinapunguziwa uzito na meli mpya zitakazokuwa zimejengwa. Utaratibu wa kujenga meli hiyo bado tunaendelea nao na muda si mrefu tunatarajia kupata mkandarasi wa kujenga meli hiyo.

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA Aliuliza:- Majanga ni mambo yasiyotarajiwa ila huwa yanatokea tu, majanga kama ajali za baharini, ziwani, barabarani, matetemeko, vimbunga, majanga ya njaa na kadhalika yamekuwa yakitokea:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha na kuimarisha nyenzo na ujuzi kwa Kikosi cha Uokoaji wa Majini kinachojulikana kama Coast Guard kwa ajili ya uokoaji?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Swali langu ni dogo tu, majanga ya moto katika Jiji la Mbeya yamekuwa yanajitokeza mara kwa mara hususan Soko la SIDO Mwanjelwa, Uhindini na sababu kubwa ni uchakavu na ubovu wa miundombinu. Naomba Serikali iniambie ina mkakati gani katika kuondoa tatizo hili kwa kushirikiana na Halmashauri?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, emphasis ya swali lake ipo katika miundombinu na ndiyo maana nilikuwa nadhani nilijibu na kama kutahitajika maelezo ya ziada yataweza kutolewa, emphasis yake ameitoa kwenye miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie muda si mrefu hapa tutasoma bajeti yetu ataona ni kwa namna gani Wizara yetu imezingatia haya ambayo ameyauliza, vilevile wakati tunapitisha Bajeti ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI unafahamu kuna baadhi ya fedha zimetengwa kwa ajili ya kushughulikia miundombinu katika Jiji la Mbeya.

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ameyatoa kuhusiana na vifaa vya Zimamoto siyo tu kwa Mkoa wa Mbeya lakini nchi yetu kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, upande wa Mbeya binafsi nilifanya ziara katika Mkoa wa Mbeya na nataka nipongeze sana uongozi wa Jeshi la Zimamoto, Mkoa wa Mbeya kwamba umefanya ubunifu wa hali ya juu kwa kuhakikisha kwamba unapanua huduma za zimamoto katika Wilaya nyingine za Mkoa wa Mbeya.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuwaunga mkono tuliweza kuhakikisha kwamba tunafanya mambo makubwa matatu. Moja, tumewapatia gari ambayo itakuwepo katika Wilaya ya Rungwe, pili kulikuwa kuna changamoto ya gari ya zimamoto ya Mkoa wa Mbeya ambayo tumefanya jitihada ya kukamilisha matengenezo yake na sasa inaendelea kutoa huduma katika Mkoa wa Mbeya, pamoja na mambo mengine ambayo zaidi yanalenga katika kuongeza utoaji wa elimu ya uokoaji katika Mkoa mzima wa Mbeya na Wilaya nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ujumla nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba katika bajeti inayofuata na katika bajeti zilizopita tumetoa kipaumbele sana katika kuhakikisha kwamba tunatenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa magari ya ziada ya zimamoto. Hizo ni kati ya jitihada ambazo tunachukua ukiachilia mbali mchakato ambao unaendelea sasa hivi wa mazungumzo na kampuni ya Ubelgiji pamoja na Austria kuweza kupata mkopo wa vifaa vya zimamoto na uokoaji kwa Tanzania nzima.