Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO Aliuliza:- Kumekuwa na changamoto ya upatikanaji wa leseni za udereva katika Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya kutokana na kutokuwepo kwa huduma hiyo. Hali hiyo inapelekea wananchi kupata adha kubwa ya kufuata huduma za leseni Musoma Mjini ambao ni Mkoa mwingine wa Polisi; kutokana na adha hiyo wananchi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali waliamua kujenga na kukamilisha jengo la usalama barabarani:- (a) Je, ni lini Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya utafungiwa mitambo ya kutoa leseni za udereva ili kuondoa usumbufu uliopo sasa wa kutumia gharama na muda kufuata huduma hiyo Musoma Mjini? (b) Je, ni lini Ofisi za Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya zitajengwa ili kurahisisha utoaji huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nasikitika kwamba Wizara ya Mambo ya Ndani leo hii inaita kwamba ni Wilaya ya Tarime/Rorya haijui kwamba ni Mkoa wa Kipolisi wa Tarime/Rorya.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya masikitiko yangu, nipende kumwambia Naibu Waziri kwamba tayari tuna miuondombinu kwa maana ya mtandao wa TRA pale, tayari wananchi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wamejenga hilo jengo na tuna rasilimali watu. Sasa nataka kujua ni lini sasa baada ya kutambua kwamba Tarime/Rorya ni Mkoa wa Kipolisi na hivyo ni Makao Makuu ya Mkoa wa Kipolisi, ni lini mtakuja kufunga huo mtambo ili kupunguza adha ya wananchi kwenda kwenye Mkoa wa Polisi wa Mara kutafuta huduma? (Makofi)
Swali la pili ni kuhusiana na kujenga ofisi ya Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya ambao Mheshimiwa Waziri amesema ni mkoa mpya. Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya ni wa siku nyingi ukilinganisha na Katavi, Simiyu na Geita. Kwa mikakati yenu ya ndani ningependa kujua ni lini mtakuja kujenga jengo zuri lenye hadhi ya Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya ili kuondokana na kukaa kwenye magodauni ambayo wanakaa sasa hivi na kushusha hadhi ya Kipolisi Mkoa wa Tarime/Rorya?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nataka nirudie majibu yangu ya msingi ambayo nimejibu kwamba, changamoto kubwa ambayo inakabili kutokukamilisha ujenzi wa vituo vya Polisi na miundombinu mingine ikiwemo hii miundombinu ya utoaji wa leseni ni ufinyu wa kibajeti. Azma ya Serikali ni kuhakikisha kwamba mikoa na wilaya zote nchini zinapata huduma hizo muhimu. Changamoto nyingine kubwa ambayo nimeizungumza ni katika mikoa ile mipya.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nichukue fursa hii kumhamasisha Mheshimiwa Mbunge, nimefanya ziara katika maeneo mbalimbali ikiwemo hii mikoa mipya na nimeona jitihada mbalimbali ambazo viongozi wa maeneo hayo wamekuwa wakifanya ili kuhamasisha wananchi, pamoja na sisi tupo tayari kuweza kuwasaidia nguvu kazi kupitia Jeshi la Magereza kuanza mchakato wa ujenzi wa vituo vya kisasa kwa mikoa mipya hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati hayo yakiendelea tutaendelea kuhakikisha kwamba tunajitahidi itakavyowezekana kadri ya bajeti itakavyoruhusu kwa upande wetu kujenga vituo hivyo vya Polisi, wakati huo huo kuzungumza na mamlaka ya TRA kuhakikisha kwamba huduma za utoaji leseni zinapatikana katika mikoa na wilaya zote nchini Tanzania, ikiwemo sehemu ambayo Mheshimiwa Mbunge anatoka.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO Aliuliza:- Kumekuwa na changamoto ya upatikanaji wa leseni za udereva katika Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya kutokana na kutokuwepo kwa huduma hiyo. Hali hiyo inapelekea wananchi kupata adha kubwa ya kufuata huduma za leseni Musoma Mjini ambao ni Mkoa mwingine wa Polisi; kutokana na adha hiyo wananchi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali waliamua kujenga na kukamilisha jengo la usalama barabarani:- (a) Je, ni lini Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya utafungiwa mitambo ya kutoa leseni za udereva ili kuondoa usumbufu uliopo sasa wa kutumia gharama na muda kufuata huduma hiyo Musoma Mjini? (b) Je, ni lini Ofisi za Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya zitajengwa ili kurahisisha utoaji huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kuna changamoto kubwa sana ya vijana wa Lushoto hasa wa bodaboda kupata leseni; Je, ni lini Serikali itaipandisha hadhi Wilaya ya Kipolisi Lushoto ili vijana wa Lushoto waweze kupata leseni bila kutumia gharama kubwa za kwenda hadi mkoani?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, ili Wilaya iweze kupandishwa hadhi, iwe Kanda Maalum ama Mkoa wa Kipolisi kuna utaratibu ambao unatakiwa ufuatwe kabla ya kutoa maamuzi. Naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Lushoto siyo katika maeneo ambayo mpaka sasa tumeweza kupata maombi rasmi ya mchakato wa kuongeza hadhi ya Kipolisi, ikiwa kuna vigezo vinakidhi basi Mheshimiwa Mbunge kwa kushirikiana na Viongozi wa Jeshi la Polisi katika eneo lake waanze mchakato huo ili tuweze kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa taratibu zilizopo.

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO Aliuliza:- Kumekuwa na changamoto ya upatikanaji wa leseni za udereva katika Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya kutokana na kutokuwepo kwa huduma hiyo. Hali hiyo inapelekea wananchi kupata adha kubwa ya kufuata huduma za leseni Musoma Mjini ambao ni Mkoa mwingine wa Polisi; kutokana na adha hiyo wananchi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali waliamua kujenga na kukamilisha jengo la usalama barabarani:- (a) Je, ni lini Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya utafungiwa mitambo ya kutoa leseni za udereva ili kuondoa usumbufu uliopo sasa wa kutumia gharama na muda kufuata huduma hiyo Musoma Mjini? (b) Je, ni lini Ofisi za Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya zitajengwa ili kurahisisha utoaji huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa, kumekuwa na vijana wengi sana wa bodaboda nchini maeneo mbalimbali wamejiajiri kwa kubeba abiria, lakini bodaboda hao wengi hawana leseni. Je, Serikali ipo tayari kuwasaidia bodaboda kuwapatia leseni, kwa kuwa wengi walikuwa wanajihusisha na matukio ambayo siyo mazuri sasa wameamua kujiajiri. Sasa Serikali ipo tayari kuwapatia leseni bodaboda ili kuwasaidia?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa kuendesha bodaboda au chombo chochote cha usafiri bila leseni ni uvunjifu wa sheria. Hatutakuwa tayari kuendelea kulea uvunjifu wa sheria. Hatuwezi kuwapa leseni watu kwa kisingizio kwamba walikuwa wanaendesha bila leseni kuhalalisha uvunjifu wa sheria.
Tunachokisisitiza hapa ni kwamba Mheshimiwa Mbunge uendelee kuhamasisha wananchi wote kufuata sheria ikiwemo hao vijana ambao wanaendesha bodaboda bila leseni. Wafuate utaratibu wa kupata leseni kwa kufanya test ili waweze kupata leseni kisheria, siyo kupata leseni kwa sababu wamekiuka sheria. Sisi tutawachukulia hatua za kisheria wale wote ambao tutawabaini kwamba wanaendesha gari na pikipiki kinyume na sheria. Tunaomba ili sheria isiweze kuwakumba basi wafuate sheria kwanza.