Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA Aliuliza:- Barabara ya Nanganga – Nachingwea – Masasi imeshafanyiwa upembuzi yakinifu toka mwaka wa 2015/2016. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini sambamba na hayo naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii ya Masasi – Nachingwea – Nanganga inahudumia Wilaya tatu, hivyo umuhimu wake katika mkoa na Taifa unafahamika sana kiuchumi. Majibu aliyoyatoa Mheshimiwa Waziri, naomba niyapokee kwa sababu kwanza wameonesha utashi wa kutenga shilingi bilioni tatu, lakini nilikuwa nataka nijue, kwa urefu wa barabara ile ambao tayari umeshafanyiwa upembuzi yakinifu kilometa 97, kwa kutenga shilingi bilioni tatu ambazo haziwezi kujenga hata kilometa zisizozidi 10, ni nini nia ya Wizara juu ya ujenzi wa barabara hii ambayo imekuwa kero kubwa kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi na Wilaya ya Nachingwea kwa ujumla?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, naomba kujua pia kupitia Naibu Waziri, upembuzi yakinifu ambao ulifanyika toka mwaka 2016 uwe umekamilika, umehusisha nyumba za wakazi ambao wamesimamisha shughuli zao. Nilikuwa nataka nijue, katika kiasi hiki cha fedha shilingi bilioni tatu, kinahusisha pia fidia kwa wale wananchi ambao wanapaswa kulipwa ili waweze kupisha ujenzi wa hii barabara? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MWASILIANO:
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina nia ya dhati ya kutaka kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami na ndiyo maana imeshatekeleza hatua ya kwanza muhimu sana ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kwa nini tumetenga fedha kidogo; kwanza hatujatenga; tunaomba tutengewe fedha kidogo siyo kwa sababu ya kutokuwa na dhamira ya dhati, bali ni kwa sababu ya fedha ambazo Wizara nzima inatarajia kuomba kutengewa imepungua sana ukilinganisha na mwaka uliopita. Kwa hiyo, tutagawana haka kasungura kadogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaanza mwaka huo ujao na miaka inayofuata tutaendelea kukamilisha na hatimaye tutakamilisha hiyo barabara kuijenga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili, naomba nimhakikishie kwamba tunapoanza kujenga na tunapotenga fedha kwa ajili ya ujenzi, inahusisha vilevile na fidia ya maeneo yale ambayo tutajenga katika mwaka huo wa fedha.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA Aliuliza:- Barabara ya Nanganga – Nachingwea – Masasi imeshafanyiwa upembuzi yakinifu toka mwaka wa 2015/2016. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wananchi wa Jimbo la Geita Vijijini miaka 56 ya uhuru hawajawahi kuona lami. Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni aliwaahidi lami kwenye barabara ya kutoka Geita – Bugurula – Nzela mpaka Nkome. Sasa namuuliza Mheshimiwa Waziri, je, ni lini Serikali imejipanga kuanza kufanya upembuzi yakinifu na kuanza kutengeneza kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo kawaida ya kutaja terehe kamili ya lini barabara itaanza kujengwa katika Wizara yetu kwa sababu taratibu zake za kufikia hadi ujenzi ni nyingi na zinahusisha taasisi mbalimbali ambazo huwezi ukazipangia muda wa kukamilisha hatua yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, ni ahadi ya Serikali ya Awamu ya Tano kwamba suala hili tutalitekeleza kama ambavyo Mheshimiwa Rais aliahidi wakati wa kampeni katika kipindi hiki cha miaka mitano.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA Aliuliza:- Barabara ya Nanganga – Nachingwea – Masasi imeshafanyiwa upembuzi yakinifu toka mwaka wa 2015/2016. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja la nyongeza. Barabara ya Nangurukulu – Liwale, Nachingwea – Liwale, ni barabara ambazo zimo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi, lakini mara nyingi nimekuwa nikiuliza barabara hizi, naambiwa itajengwa, itajengwa; sasa wana-Liwale wanataka kusikia ni lini barabara hizi zitaingia kwenye upembuzi yakinifu na hatimaye kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante sana.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI, UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua tunayoifanya sasa ni kutafuta fedha. Nimhakikishie Mheshimiwa Kuchauka, mara tutakapopata fedha, suala la upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii ambayo imeahidiwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi tutaitekeleza.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA Aliuliza:- Barabara ya Nanganga – Nachingwea – Masasi imeshafanyiwa upembuzi yakinifu toka mwaka wa 2015/2016. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa wananchi wa Wilaya ya Ngorongoro, Mkoani Arusha, wamekuwa wakipata shida sana ya usafiri kutokana na ubovu wa barabara.
Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ambayo ilikuwa kwenye bajeti ya 2016/2017 ya kujenga barabara ya lami inayoanzia Loliondo hadi Mto wa Mbu?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu kumhakikishia Mheshimiwa Magige na Mheshimiwa Olenasha kwamba mkandarasi tunatarajia kumpata muda siyo mrefu kwa sababu taratibu za kumpata mkandarasi zipo katika hatua za mwisho na mara tutakapompata mkandarasi barabara hii itaanza kujengwa.

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA Aliuliza:- Barabara ya Nanganga – Nachingwea – Masasi imeshafanyiwa upembuzi yakinifu toka mwaka wa 2015/2016. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya wananchi wa Mji wa Tunduma, napenda kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu wananchi wa Mji wa Tunduma wamekubali ushauri wa viongozi wao na kuondoa nyumba katika maeneo mbalimbali na kuhakisha kwamba barabara 42 zimepatikana kwenye Mji wa Tunduma, Serikali ina mpango gani wa kuwaunga mkono ili kuhakikisha kwamba barabara zile zinakuwa kwa kiwango cha lami kwenye Mji wa Tunduma, ukizingatia mji unaendelea kukua?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukulie kwamba taarifa hii ni ombi na kule wakati tunapita kwenye kampeni tulitoa ahadi zinazofanana na hayo ambayo ameyasema. Nimhakikishie tu kwamba ombi hili tutalipeleka katika timu ya wataalam ambayo ndiyo huwa inaandaa vipaumbele kulingana na ahadi za viongozi wakuu, ahadi za Wabunge, na kadhalika, waweze kuliangalia ili tuweze kulitekeleza kama ambavyo tuliahidi wakati wa uchaguzi.