Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA Aliuliza:- Serikali imekuwa ikisisitiza na kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kulinda na kutunza vyanzo vya maji kwa kutokata miti ovyo na kutojenga karibu na vyanzo hivyo, lakini wako baadhi ya wananchi wenye tabia ya kushirikiana na baadhi ya watumishi wachache wa Serikali kukata miti ovyo na kujenga karibu na vyanzo vya maji. (a) Je, ni lini Serikali itasimamia kikamilifu sheria za kulinda mito na miti nchini? (b) Je, Serikali haioni umefika wakati sasa kutunga sheria kali zaidi ili kujihami na global warming?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa uharibifu wa mazingira umekuwa ni tatizo sugu sana hususan katika Jimbo langu la Kilindi katika Kata za Negero, Mkindi, Kilindi Asilia pamoja na Msanja kutokana na shughuli za kibinadamu; je, Waziri yuko tayari kwa kushirikiana na Wataalamu wetu wa Chuo Kikuu cha SUA, kwa mfano, tuna Watalamu wazuri, akina Profesa Dhahabu na Mariondo kwa ajili ya kupeleka timu kule kuweza kufanya tathmini kubwa? (Makofi)
Swali la pili, suala hili la mazingira limekuwa ni sugu sana; je, Serikali iko tayari sasa kwa kushirikiana na Halmashauri kuhakikisha kwamba inapeleaka wataalamu wa kutosha wa mazingira kulinda maeneo yetu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeshindwa kujizuia kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa swali lake zuri, Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua. Nampongeza kwa swali lake zuri sana leo la mazingira hapa Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali yake ya nyongeza naomba niyajibu kama ifuatavyo:-
Moja, kwanza ofisi yangu inashirikiana vizuri sana na wataalam wa mambo ya mazingira hasa katika mambo ya hewa ya ukaa ambao wako pale SUA. Nimhakikishie kwamba ofisi yangu haina kipingamizi chochote cha kuja kufanya tathmini ya maeneo yaliyoathirika katika Kata alizozitaja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaunda hiyo timu, itakuja na hao wataalam na nimhakikishie kwamba Ofisi ya Makamu wa Rais ina watalaam waliobobea katika mambo ya mazingira vizuri sana, kwa hiyo, hakuna kitu ambacho kitaharibika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kwamba wasiwasi wake kuhusu wataalam wa mazingira ambao anahisi kwamba Halmashauri nyingi hazina wataalam na sekta nyingine, nimhakikishie tu kwamba hivi karibuni Waziri wangu anakamilisha orodha ya wataalam ambao tutawateua ambao ni Wakaguzi wa Mazingira (Environmental Inspectors) zaidi ya 400 hapa nchini na watasambazwa kwenye sekta mbalimbali. Hivyo basi, tatizo hili na kiu kubwa ya kuwahitaji wataalam hawa watakuwepo katika sekta kama Mheshimiwa Mbunge ambavyo ameomba.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA Aliuliza:- Serikali imekuwa ikisisitiza na kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kulinda na kutunza vyanzo vya maji kwa kutokata miti ovyo na kutojenga karibu na vyanzo hivyo, lakini wako baadhi ya wananchi wenye tabia ya kushirikiana na baadhi ya watumishi wachache wa Serikali kukata miti ovyo na kujenga karibu na vyanzo vya maji. (a) Je, ni lini Serikali itasimamia kikamilifu sheria za kulinda mito na miti nchini? (b) Je, Serikali haioni umefika wakati sasa kutunga sheria kali zaidi ili kujihami na global warming?

Supplementary Question 2

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu yako mazuri ya Mheshimiwa Waziri, kusema kwamba kuna sheria ya mita 60 kutofanya huduma yoyote kutoka kwenye chanzo cha maji, lakini bado vyanzo vya maji vinaendelea kuathirika katika maeneo ya wazi na mpaka ndani ya mbuga zetu ambayo ni maeneo yanayolindwa na kuhifadhiwa na Serikali.
Je, Serikali sasa ina mpango gani mahsusi wa kufanya utafiti wa miti ambayo inazalisha maji, iwe imepandwa kuzunguka vyanzo vya maji? Ni mkakati upi hasa mahsusi wa kudhibiti hivi vyanzo vya maji visiathirike? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mita 60 na vyanzo vya maji kuendelea kuharibiwa na utafiti ambao unafanyika, napenda nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tulipokuwa tunaandaa Mkakati wa Kitaifa wa Upandaji Miti wa mwaka 2016 hadi mwaka 2021, tulizingatia hayo na mpaka sasa hivi tumeshabaini aina ya miti inayofaa kupandwa katika vyanzo vya maji na utaratibu huu tutausambaza kwa wataalam wote. Kwa kushirikiana na TFS na wataalam wa Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, tumeshaandaa tayari aina ya miti ambayo inafaa kwa ajili ya kuhifadhi vyanzo vyetu vya maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jithada unaziona, juzi hapa Mheshimiwa Makamu wa Rais amezindua mpango mkubwa wa kuokoa hali ya uharibifu wa mazingira ambayo inaendelea katika Mto Mkuu Ruaha. Katika kufanya hivyo, hatuishii hapo, tutaendelea kufanya tathmini katika vyanzo vyetu vya maji vyote ili tuje na solution ya uhakika na tuweze kutenga fedha zinazokidhi kwa ajili ya kuhakikisha kwamba mazingira haya tunayalinda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile suala la mazingira ni gumu sana, ulinzi wake ni mgumu. Inatakiwa kila mwananchi, sisi wenyewe Wabunge tuhakikishe kwamba tunasaidia kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba mazingira yetu yanalindwa.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA Aliuliza:- Serikali imekuwa ikisisitiza na kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kulinda na kutunza vyanzo vya maji kwa kutokata miti ovyo na kutojenga karibu na vyanzo hivyo, lakini wako baadhi ya wananchi wenye tabia ya kushirikiana na baadhi ya watumishi wachache wa Serikali kukata miti ovyo na kujenga karibu na vyanzo vya maji. (a) Je, ni lini Serikali itasimamia kikamilifu sheria za kulinda mito na miti nchini? (b) Je, Serikali haioni umefika wakati sasa kutunga sheria kali zaidi ili kujihami na global warming?

Supplementary Question 3

MHE. JUMAA H. AWESO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Mheshimiwa Aweso.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mabadiliko ya tabianchi athari zake zimeonekana wazi wazi katika Mji wa Pangani. Serikali pamoja na jitihada kubwa wanazozifanya kukarabati ukuta wa Pangani, lakini bahari imekula kwa kiasi kikubwa kwa eneo la Pangadeco; je, ni lini Serikali itafanya tathmini ya haraka kuhakikisha kwamba inaanza ujenzi wa ukuta kwa eneo la Pangadeco?

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itafanya tathmini katika eneo lililobaki la Pangani ambalo kwa jina maarufu Pangadeco katika mwaka ujao wa fedha wa 2017/2018. Serikali itafanya tathmini ya eneo hilo na kutafuta namna bora tutakayoitumia, aidha kujenga ukuta au njia nyingine.