Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA Aliuliza:- Jumuiya ya Ulaya inatekeleza Mkakati wa Ajenda ya Mabadiliko. Je, Tanzania imejipangaje kukubaliana na changamoto zinazotokana na Ajenda hiyo ya Mabadiliko ya Jumuiya ya Ulaya?

Supplementary Question 1

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: MheshimiwaNaibu Spika, ahsante sana. Ninayo maswali madogo mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Swali la kwanza, kwa kuwa Jumuiya ya Ulaya katika mpango wake wa miaka mitano au kwa lugha nyepesi Multiannual Financial Framework waliahidi kuisaidia Tanzania Euro milioni 629, kwa kuwa hii inaendana na mpango wa Agenda For Change ina dalili ya kupungua misaada hiyo.
Je, kwa Tanzania misaada hiyo itatoka kama walivyoahidi au inapungua kwa kuzingatia sera yao ya ajenda ya mabadiliko?
Swali la pili, kwa kuwa hivi sasa tunaandaa GSP,
Tanzania tumefanya uamuzi katika Bunge hili kwamba sasa EPA basi ikiwezekana, lakini sasa kwa uamuzi huo maana yake sasa tutafanya biashara ya kupitia GSP au DSP Plus.
Je, kulingana na hii ajenda ya mabadiliko tunajiandaaje sasa kuingia katika mlolongo huu?

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuthibitisha au kusema kwamba ahadi ambayo ilifanywa na Jumuiya ya Ulaya ya kuahidi kuisaidia Tanzania Euro milioni 628 kwamba itabaki pale pale au itapungua au kuongezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika vigezo ambavyo wao wameviweka kama framework ya kuweza kutoa misaada hiyo ni kuhakikisha kwamba nchi inaweza kuhakikisha inasimamia vizuri suala la la haki za binadamu na utawala bora, usawa wa jinsia, kuhakikisha kwamba vyama vya kiraia vinafanya kazi zake vizuri, kusimamia shughuli zinazofanywa na Serikali za Mitaa, kusimamia vizuri na kuhakikisha kwamba tunapambana na rushwa, kuhakikisha kwamba tunasimamia sera za usimamizi wa kodi na usimamizi wa sekta ya umma. Hivi vyote vinafanyika ndiyo maana unakuta kwamba mpaka sasa hivi hata World Bank wanaendelea kutupa misaada.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunachotakiwa kufanya
kama Watanzania ni kuhakikisha kwamba tunaendelea kuishi na kusimamia utawala bora na sekta ya umma inasimamiwa vizuri. Hilo ndiyo jibu langu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kwamba katika
Bunge hili liliamua kwamba suala la kusaini mkataba wa EPA sasa basi, kwa hiyo, sasa Tanzania inafanyaje. Tanzania imejipanga vizuri kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi kuhakikisha kwamba inahamasisha sekta binafsi ifanye kazi pamoja na Serikali. Vilevile inahamasisha mashirika ya nje na nchi nyingine za nje kuja kuwekeza katika nchi yetu.
Wizara yangu imefanya kazi hiyo vizuri na mifano mmeiona. Vilevile kama nilivyosema kwamba diaspora tunaendelea kuwasimamia na kuwahamasisha katika Balozi zetu, Mabalozi wanafanya mikutano na hawa diaspora ili kuhakikisha kwamba wao pia wanatumia fursa ya kuwekeza katika nchi yetu. Katika mwelekeo huo tutakuwa tunalinda maslahi ya nchi yetu na siyo kuyapoteza.