Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA aliuliza:- Wananchi wa Ludewa wamekuwa wakisikiliza mipango ya Serikali juu ya miradi mikubwa ya Makaa ya Mawe, Mchuchuma na Liganga ambapo kumekuwa na mipango mingi ambayo kwa sasa inaonekana kutekelezwa:- (a) Je, ni lini wananchi walioachia ardhi yao kupisha miradi hiyo watalipwa fidia? (b) Je, ni lini miradi hiyo inatarajiwa kuanza?

Supplementary Question 1

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini bado ulipaji wa fidia huu umeonekana kuwa ni kitendawili, kwa mara ya kwanza tuliambiwa kwamba fidia hizi zitalipwa tarehe 16 Februari, lakini sasa hivi Serikali inakuja na majibu mengine kwamba itaanza kulipa mwezi Juni. Sasa tunaomba kujua specific date ya fidia hiyo itakuwa ni lini?
Pili, kumekuwa na usumbufu mkubwa katika ulipaji wa hiyo fidia, je, kwa sababu muda utakuwa umeshapita fidia hii italipwa pamoja na fidia?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli fidia ilianza kulipwa tangu mwezi Februari mwaka huu.
Mheshimiwa Spika, lakini tutambue kwamba suala la ulipaji fidia ni suala endelevu, kadri tathmini inavyofanyika ndiyo fidia inavyoendelea kulipwa na ndiyo maana tunasema hata mwezi huu na mwezi ujao wataendelea kulipwa fidia. Suala kubwa Mheshimiwa Mbunge ni kwamba shughuli za ujenzi wa mradi huu zitaanza mapema tu baada ya fidia kukamilika.
Mheshimiwa Spika, swali la pili kama wananchi watalipwa pia pamoja na nyongeza ya mapunjo ya awamu iliyopita.
Mheshimiwa Spika, taratibu za fidia kwa waathirika hufanyika wakati tathmini inapofanyika, kwa hiyo malipo ya fidia hulipwa kulingana na viwango wakati tathimini inafanywa na siyo vinginevyo.

Name

Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA aliuliza:- Wananchi wa Ludewa wamekuwa wakisikiliza mipango ya Serikali juu ya miradi mikubwa ya Makaa ya Mawe, Mchuchuma na Liganga ambapo kumekuwa na mipango mingi ambayo kwa sasa inaonekana kutekelezwa:- (a) Je, ni lini wananchi walioachia ardhi yao kupisha miradi hiyo watalipwa fidia? (b) Je, ni lini miradi hiyo inatarajiwa kuanza?

Supplementary Question 2

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Spika, suala la ulipaji wa fidia Ludewa pia linafanana na sehemu ya Wilaya ya Geita ambapo wananchi wa mtaa wa Mgusu wanaishi katika eneo ambalo liko ndani ya beacon ya Geita Gold Mine na wananchi hawa wamekuwa wakiathirika na taka zenye sumu zinazomwagwa katika eneo lao.
Je, Serikali inaweka msukumo gani kwa Geita Gold Mine kuhakikisha kwamba inawalipa wananchi wa mtaa wa Mgusu fidia ili waweze kupisha eneo hilo na wasiathirike na taka katika hilo eneo la Geita? Asante.(

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa wananchi wa Mgusu wanaishi sehemu ya leseni ya utafiti wa GGM, lakini taratibu ya Sheria za Ardhi na Sheria za Madini zote hulingana. Kimsingi, mahali ambapo mgodi haulitumii eneo hilo wananchi wanaweza waka-co-exist na shughuli za mgodi, lakini mahali ambapo shughuli za mgodi zinafanyika, basi wananchi wanaoishi katika maeneo hayo hufanyiwa fidia na kupisha shughuli za ujenzi.
Mheshimiwa Spika, eneo la Mgusu linalozungumzwa, Mgodi wa GGM haujaanza kulitumia. Kwa sasa hivi wananchi wanaishi Mgusu na kimsingi Mgusu imeshakuwa ni mjini na GGM sasa hivi haioni sababu ya kulichukua. Ila itakapofika wakati wa kulichukua eneo hilo, Mheshimiwa Mbunge atawasiliana na sisi na taratibu za fidia za wananchi wa Mgusi zitafanyika.