Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE Aliuliza:- Mradi wa maji Madibira ulianzishwa mwaka 1975 na sasa miundombinu yake imechakaa sana na banio (intake) lake imekuwa dogo sana wakati idadi ya watu imeongezeka sana. Je, Serikali haioni umuhimu wa kukarabati miundombinu hiyo ili kuwaokoa wananchi wa Mikumi na taabu ya maji?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na jitihada za Serikali za kukamilisha huu mradi wa World Bank, Mji wa Mikumi ni Mji wa kitalii na umekuwa ukipata wageni mbalimbali na idadi ya watu imeongezeka wamekaribia wakazi 30,000, lakini Mikumi kuna vyanzo vingi kama Iyovi, Madibila na pia Mto Muhanzi.
Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweza kutumia
vyanzo vingine ili viweze kusaidiana na mradi huu ili iweze kusaidia wananchi wa Jimbo la Mikumi na kadhia hii?
Swali la pili, katika ziara ya Naibu Waiziri ulipokuja uliagiza watalaam waje kuangalia chanzo cha maji cha Sigareti pale Kata ya Ruaha ambapo kingeweza kusaidia Kata ya Ruaha na Rwembe, wameshafanya hivyo na kukuletea taarifa na imeonekana takribani shilingi bilioni mbili zinahitajika ili kuwezesha wananchi wa Ruaha waweze kupata mradi huo.
Je, Mheshimiwa Waziri unaweza kuwaahidi vipi wananchi wa Ruaha ambao sasa wanakutazama kwamba je, huu mradi utaingizwa katika Bajeti ya 2017/2018 ili uweze kuwasaidia wananchi wa Jimbo la Mikumi kwa ujumla?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyotaja kwamba ni kweli nilishawahi kutembelea Jimbo la Mikumi kwenda kuangalia miundombinu ya maji. Ni kweli tulienda na yeye mpaka Kijiji cha Ruaha na tukaona chanzo cha Segereti na tukaagiza. Kwa sababu kwa sasa hivi tuna utaratibu Wizara kwamba tunaweka fedha kila Halmashauri, basi kwa kutumia nafasi hili niagize ule mradi ambao tuliagiza kamba waufanyie mchakato wa kufanyiwa usanifu ukikamilika basi watumie fedha tutakazozitenga katika Bajeti ya mwaka 2017/2018.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia chanzo cha Madibira tayari tumeshamuagiza Mkurugenzi wa Maji wa Mamlaka ya Morogoro (MORUWASA) ambaye Aprili anatanganza tender, ifikapo Juni na Julai tayari atakuwa amempata mkandarasi kwa ajili ya kuboresha kile chanzo cha Madibira ambacho kina umbali wa kilometa 17 kutoka chanzo kuja mjini Mikumi na kazi zitakazofanyika ni pamoja na kwanza kuboresha chanzo chenyewe cha maji cha Madibira ili kiweze kupanuliwa kuongeza kiwango cha maji na kuweka mabomba mapya ambayo yataleta maji katika Mji wa Mikumi.

Name

Mboni Mohamed Mhita

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE Aliuliza:- Mradi wa maji Madibira ulianzishwa mwaka 1975 na sasa miundombinu yake imechakaa sana na banio (intake) lake imekuwa dogo sana wakati idadi ya watu imeongezeka sana. Je, Serikali haioni umuhimu wa kukarabati miundombinu hiyo ili kuwaokoa wananchi wa Mikumi na taabu ya maji?

Supplementary Question 2

MHE. MBONI M. MHITA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuniona. Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Handeni Vijijini, Kata ya Mkata tulibahatika kupata mabwawa mawili, moja likiwa Mkata lakini la pili likiwa eneo la Manga.
Mheshimiwa Naibu Spika, mabwawa haya yako chini ya kiwango na mpaka sasa hayajaweza kuanza kutumika. Nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri katika ziara yake katika Jimbo la Handeni Vijijini alipita na kujionea hali halisi ya yale mabwawa. Pia aliweza kutuahidi wananchi wa Jimbo la Handeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja hapo. Mheshimiwa Naibu Waziri alituahidi baada ya kuona yale mabwawa kwamba wangefanyia kazi na kuweza kutupa ripoti ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa wale ambao wamefanya ubadhilifu ili kuweza kupata utatuzi wa maji.
Wananchi wa Handeni Vijijini wangependa kujua, je, utatuzi umefanyika na ripoti imeshafanyiwa kazi ili tuweze kujua na hatua stahiki ziweze kufanyika kwa wale ambao wamefanya ubadhilifu huu? Nashukuru sana.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Naibu Spika, nilitembelea kweli eneo hilo la Mkata nikakuta kazi iliyofanyika na kazi hiyo nilizungumza kwenye vyombo vya habari kwamba hata mimi sikuridhika nayo. Baada ya hatua hiyo Katibu Mkuu aliunda Tume ya Wahandisi kwenda kukagua hilo eneo, sasa hivi wanakamilisha kuandaa taarifa ili iweze kuwasilishwa Wizarani ili kuweza kuchukua hatua.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo lengo letu ni kuhakikisha wananchi wanapata maji. Tuliweka utaratibu mwingine tumeshatangaza tenda tayari kwa ajili ya kupanua mradi wa HTM pale Korogwe ili uhakikishe kwamba unapeleka maji hadi Handeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia tulishasema tunaweza tukatumia chanzo cha Wami ili tuweze kuchukua yale maji kuhakikisha kwamba eneo la Handeni Vijijini linapata maji ya kutosha.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE Aliuliza:- Mradi wa maji Madibira ulianzishwa mwaka 1975 na sasa miundombinu yake imechakaa sana na banio (intake) lake imekuwa dogo sana wakati idadi ya watu imeongezeka sana. Je, Serikali haioni umuhimu wa kukarabati miundombinu hiyo ili kuwaokoa wananchi wa Mikumi na taabu ya maji?

Supplementary Question 3

MHE. ORAN M. NJENZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana, suala la Mji Mdogo wa Mbalizi kuna changamoto kubwa za maji kama iliyokuwa kwa Mji wa Mikumi. Je, ni lini mtatatua changamoto kubwa ya maji kwenye Mji Mdogo wa Mbalizi? Ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya tuliwasiliana nae nikiwa kwenye ziara Mbeya na tukawa tumekubaliana kwamba tufanye mapendekezo, Wizara imeshaagiza tayari kwamba Mamlaka ya Maji ya Mkoa wa Mbeya ijipanue ili iweze kuhudumia mpaka eneo la Mbalizi. Tayari wanaendelea na utaratibu huo wameshafanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbalizi na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbalizi ameonekana kuridhia ili Mamlaka ya Maji ya Mbeya iweze kupeleka miundombinu mpaka Halmashauri ya Mbalizi.
Mheshimiwa Naibu Spika, niahidi kwamba taratibu hizi zitakamilishwa na wananchi wa Mbalizi watapata huduma ya maji kutokana na Mamlaka ya Maji ya Mji wa Mbeya.

Name

Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPH L. HAULE Aliuliza:- Mradi wa maji Madibira ulianzishwa mwaka 1975 na sasa miundombinu yake imechakaa sana na banio (intake) lake imekuwa dogo sana wakati idadi ya watu imeongezeka sana. Je, Serikali haioni umuhimu wa kukarabati miundombinu hiyo ili kuwaokoa wananchi wa Mikumi na taabu ya maji?

Supplementary Question 4

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mheshimiwa Naibu Spika, takribani mwezi sasa wakazi wa Jiji la Tanga wanapata maji kupitia mamlaka ya maji ambayo siyo safi na salama.
Je, Serikali ina taarifa kwamba wakazi wa Tanga wanaweza kupata maradhi ya milipuko kutokana na kutokunywa maji ambayo siyo safi na salama?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mamlaka ambazo zinaongoza kutoa huduma ya maji iliyo bora ni pamoja na Mamlaka ya Maji ya Tanga na Mamlaka ya Maji ya Moshi. Sasa kama hilo limejitokeza basi Mheshimiwa Mbunge nikuahidi kwamba tutalifuatilia kuona ni nini kimejitokeza katika hilo. Kwa taarifa tulizonazo ni kwamba mamlaka zinazoongoza ni pamoja na Mamlaka ya Maji ya Moshi na Tanga. Kwa hiyo, nikuahidi kwamba tutalifuatilia kuona ni eneo gani ambalo lilipata hiyo shida ya maji kutokuwa salama.