Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE Aliuliza:- Waliokuwa wafanyakazi wa Hoteli ya Seventy Seven ya Arusha hawajalipwa mafao yao hadi sasa:- Je ni lini watalipwa mafao yao?

Supplementary Question 1

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu yasiyoridhisha ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa katika jibu la msingi Mheshimiwa Naibu
Waziri amesema wafanyakazi hao wa Seventy Seven walilipwa, siyo kweli walilipwa awamu ya kwanza, awamu ya pili haikuwafikia wafanyakazi hawa na baada ya malalamiko Wizara ilituma wakaguzi mwaka 2003 wakakagua wakajua kuna tatizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa watu hao wamekuwa wakihangaika muda mrefu kutafuta haki zao waliandika barua Ofisi ya Rais, tarehe 17 Machi, 2016 walijibiwa barua kutoka Ofisi ya Rais ikienda kwa Waziri wa Maliasili kuwa ashughulikie tatizo hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, siyo hivyo tu, vilevile walilalamika Ofisi ya Waziri Mkuu na kuna barua ilikuja ya tarehe 4 Novemba, 2016 kuwa tatizo hili lishughulikiwe.
Je, Serikali haioni kwamba wanyonge hawa wanapoteza muda mwingi wakitafuta haki yao huku yenyewe ikidai imewalipa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri wa Maliasili alishapewa agizo kutoka Ofisi ya Rais ashughulikie, ni kwa nini wanasuasua wananchi wakiendelea kupata taabu?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni swali la nyongeza ambalo limejitokeza na hoja ambayo nimeisikia kwa mara ya kwanza hapa, basi nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge anipe fursa katika kipindi cha mapumziko leo hii nilifanyie kazi halafu nimpe majibu ambayo yatakuwa ni ya uhakika zaidi.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE Aliuliza:- Waliokuwa wafanyakazi wa Hoteli ya Seventy Seven ya Arusha hawajalipwa mafao yao hadi sasa:- Je ni lini watalipwa mafao yao?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Hapo kwenye hilo swali, napenda kuiuliza Serikali wapo wastaafu kule kwangu wengi zaidi ya 20 ambao wananifuata ofisini, ni wazee, wengine wameshafariki hawajalipwa waliokuwa watumishi wa Afrika Mashariki, waliokuwa watumishi kama Game Officers. Sasa kwa nini Serikali isiwe proactive kuwafuatilia hao wazee huko waliko ili waweze kulipwa mafao yao, badala ya kutusumbua Wabunge ambao tumeingia hivi karibuni?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo Watanzania wote ni mashahidi, Wizara ya Fedha na Mipango ina zaidi ya miezi mitatu sasa ikizunguka mikoa mbalimbali kufanya tathmini na kuhakiki wastaafu wote. Kwa hiyo, hilo alilolisema Mheshimiwa Kakunda, Wizara ya Fedha ilishafika Tabora na tayari imeshafika Sikonge. Kama wapo ambao hawakufikiwa tuna utaratibu zoezi hili ni endelevu waweze kufika na kuhakikiwa na haki yao watapata bila tatizo.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE Aliuliza:- Waliokuwa wafanyakazi wa Hoteli ya Seventy Seven ya Arusha hawajalipwa mafao yao hadi sasa:- Je ni lini watalipwa mafao yao?

Supplementary Question 3

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na majibu ya Serikali hususan Wizara ya Fedha kwamba wastaafu wote wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki walishalipwa mafao yao. Hapa nina check ya mzee mmoja ambaye anaitwa Mzee Malembeka na Mheshimiwa Naibu Waziri unamfahamu, katika madai yake alikuwa anadai shilingi milioni 15 Serikali imemlipa shilingi milioni tano tu. Sasa na hapa ni wazee wengi sana, naomba kauli ya Serikali.
Je, ni kweli kwamba wazee wastaafu wote wa Afrika Mashariki wamelipwa fedha zao na kwamba hawaidai Serikali? Atoe tu tamko ili tujue hili jambo limekwisha au bado wazee hawa wanaidai Serikali.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, Bunge lako Tukufu linajua ilishatolewa kauli ya Serikali ndani ya Bunge hili kuhusu malipo ya wastaafu wa Afrika Mashariki kwamba wastaafu wote walishalipwa. Kama nilivyosema hiyo ndiyo kauli ya Serikali iliyotolewa ndani ya Bunge hili, tulishafungua milango mtu ambaye anaona hajalipwa ana udhibitisho Wizara ipo tayari kumpokea na tuweze kuhakiki na kumlipa malipo yake.