Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itayakubali maombi ya wananchi wa Halmashauri ya Busokelo ya kuifanya Halmashauri hiyo iwe Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Serikali kwamba Halmashauri ya Busokelo haijakidhi vigezo vya kuwa Wilaya, nina maswali mawili kwa Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo vigezo anavyosema haijakidhi sijui ni vipi kwa sababu vigezo ambavyo vinazingatiwa, hasa ni idadi ya watu pamoja na jiografia ya eneo husika, kwetu kwa sababu hii tathmini ilishafanyika tangu miaka 2013 na sasa hivi ni 2017. Hauoni kwamba kuna
umuhimu sasa wa kuanzisha hiyo Halmashauri ya Busokelo iwe inaitwa Wilaya ya Busokelo badala ya sasa ilivyo? Swali la pili, kwa kuwa Mkuu wa Wilaya pamoja na DAS wanafanya kazi nzuri katika Wilaya ya Rungwe, kwa bahati mbaya kwa sababu ya jiografia ya Rungwe ilivyo kuna zaidi ya kata 40 na huyu Mkuu wa Wilaya hawezi kusimamia ama kufuatilia zote kwa wakati mmoja kufuatana na jiografia ilivyo.
Je, hauoni pia ni miongoni mwa sababu ambayo
inaweza ikasababisha ianzishwe Wilaya ya Busokelo na hivyo iweze kuanzishwa haraka iwezekanavyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwa sababu specification inataka angalau eneo hilo liwe na eneo lisilopungua kilometa za mraba 5,000 nwakati pale kiuhalisia ziko kilometa za mraba 969. Kwa hiyo, hii ilikuwa ni kigezo kimojawapo ambacho kimesababisha isiweze ku-qualify. Kipindi kile idadi ya watu kwa muongozo inatakiwa watu wasiopungua 250,000 lakini katika kipindi kile tathmini ilivyofanyika kulikuwa na watu takribani 96,348.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninafahamu muda mrefu sasa hivi umeshapita kutoka kipindi kile mpaka sasa hivi hii tathmini ukiiangalia huenda population imeongezeka, lakini vilevile hata ukiangalia suala zima la tarafa, vigezo lazima angalao kuwe na tarafa tatu pale ukiangalia ni tarafa moja. Ninafahamu kwamba mlikuwa na juhudi ya kuitenga ile Tarafa moja mpate tarafa nyingine tatu, hii nilidhani kwa sababu Mbunge mnafahamu kama ulivyosema mna kata zipatazo 40, mnaweza mkakaa kwa pamoja sasa na RCC
yenu kuangalia mnaweza kuishauri vizuri nini cha kufanya. Baadae ikionekana vigezo hivi sasa vimekaa vizuri basi Serikali itaona nini cha kufanya na jinsi gani ya kupata eneo hili kuwa eneo la kiutawala la Kiwilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala kwamba Mkuu wa Wilaya ya Busokelo anahudumia eneo kubwa sana, kwa hiyo kuna haja ya kuona hili jambo sasa ikiwezekana Wilaya ile sasa Busokelo iwe Wilaya kamili. Kama nilivyosema pale awali ni kwamba hivi sasa ninyi angalieni jinsi ya kufanya. Nafahamu kwamba ni kweli Mkuu wa Wilaya ya Rungwe anafanya kazi kubwa sana, nilikuwa nae pale site siku ile tulipopata lile tatizo, kweli ni miongoni mwa Wakuu wa Wilaya ambao wanajituma sana katika kazi yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile wote kama Viongozi Wakubwa na Mheshimiwa Naibu Spika uko hapa, nadhani mtaliangalia kwa uzito wenu kwa jinsi gani mtafanya, kama Busokelo, kama Rungwe kwa wakati mmoja ni jinsi gani hata mtafanya mipaka yenu na kila kitu. Lengo kubwa ni kupeleka huduma kwa wananchi na Serikali mkiona kwamba mmekidhi vigezo hivyo, haitasita kufanya maamuzi sahihi.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itayakubali maombi ya wananchi wa Halmashauri ya Busokelo ya kuifanya Halmashauri hiyo iwe Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Matatizo yaliyopo huko Busokelo yapo pia katika
Halmashauri ya Wilaya ya Itigi. Katika Wilaya ya Manyoni kuna Halmashauri ya Manyoni na Hamashauri ya Itigi; Halmashauri ya Itigi square kilometer zinakidhi na maombi yamekuwa yakipelekwa kila mara na toka mwaka 1980 Serikali imekuwa ikiwaahidi wananchi wa Itigi kwamba watapatiwa Wilaya kamili.
Je, sasa ni lini Serikali itaipa Halmashauri ya Itigi kuwa Wilaya kamili?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ukiangalia Manyoni, lazima tufahamu juhudi kubwa ya Serikali iliyofanya pale, mwanzo ile yote ilikuwa inaitwa Wilaya na Halmashauri ya Manyoni. Hapa katikati ndiyo tukapata Halmashauri mpya ya Itigi na wewe Mheshimiwa Mbunge unafahamu hata suala zima la upelekaji wa fedha ndiyo kwanza tumepeleka kwa ajili ya kujenga miundombinu ya Halmashauri ile.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili ninafahamu
kwamba, siku ile nilikuwa na Mkuu wa Wilaya pale na alisikitika katika hilo alisema kwamba mafuta anayoyatumia ni kwamba, akiamua kuzunguka eneo lake matufa yanaisha kwa sababu Manyoni ukijumlisha na Itigi ni eneo kubwa sana.
Naomba niseme japokuwa maombi hayo inawezekana mwanzo yalikuja yalidondoka kwa sababu yalishindwa kupata sifa, hizo sifa sasa hivi zikikamilika basi naomba mfanye ile michakato ya kisheria kama inavyokusudiwa kuanzia katika ngazi za Ward DC, Baraza la Madiwani, DCC, RCC na ikifika katika Ofisi ya Rais – TAMISEMI
na Waziri wangu yuko hapa, hawezi kushindwa kufanya maamuzi sahihi kwa kadri anavyoona jambo hilo linafaa kwa maslahi mapana ya wananchi wa Itigi.

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itayakubali maombi ya wananchi wa Halmashauri ya Busokelo ya kuifanya Halmashauri hiyo iwe Wilaya?

Supplementary Question 3

MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda yenye majimbo ya Mwibara na Bunda ni majimbo mawili ambayo hayapakani. Jimbo la Bunda liko kwingine na Jimbo la Mwibara liko kwingine, lakini ndiyo yanaunda Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa jambo hili
tulishampelekea Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI, na kwa kuwa Mwibara iliwahi kuwa Jimbo tangu mwaka 1974, lakini tulishapeleka TAMISEMI iwe Wilaya mpaka leo vigezo ilishatimiza lakini hatupatiwi.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anawaambia nini wana - Mwibara juu ya jambo hili ambalo ni changamoto ya miaka mingi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, wasiofahamu hili Jimbo la Mheshimiwa Kangi Lugola ni sawasawa kama unazungumza kama lile bakuli halafu katikati kuna kile kisahani. Katikati ya kisahani pale unapata Jimbo la Dada yangu Mheshimiwa Ester Bulaya, Jimbo la Bunda Mjini. Ukienda huku utakuta Jimbo la ndugu yangu Mheshimiwa Boniphace Getere na huku unakuta Jimbo la Mwibara, kwa
hiyo anachozungumza ni kweli.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaambie
Waheshimiwa Wabunge, wakati mwingine tunapoenda kufanya maamuzi ya mgawanyo wa haya maeneo wakati mwingine hatuweki mipaka sahihi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, pale hata
ukiangalia ni kama yai, katikati kiini cha yai ndiyo Jimbo la Mheshimiwa Ester Bulaya hata ninaamini inawezekana ukatokea ugomvi mkubwa wa wapi Halmashauri ya Jimbo hilo itajengwa inawezekana ni kutokana na huko mwanzo maamuzi yetu hayakuwa sahihi. Inawezekana ilikuwa ni mihemko ya kisiasa ya kugawanya, jinsi gani tugawanye, hatukufanya maamuzi sahihi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba hili kweli ni changamoto kubwa. Kama Mheshimiwa Kangi Lugola nafahamu kweli changamoto yako ni kubwa na nimefika mpaka kule ziwani siku ile nilivyofika, nimechanginyikiwa kweli Jimbo lako lilivyo. Basi mtajadiliana kwa pamoja kule katika vikao vyenu kuangalia nini cha
kufanya. Jukumu letu kubwa Serikali ni kuona jinsi gani tutafanya ili wananchi waweze kupata huduma. Hivi sasa ninaamini wewe na Mbunge mwenzako ni lazima mkae vizuri la sivyo inawezekana mkapishana wapi Makao Makuu yenu itaenda kujengwa kwa maslahi mapana ya maeneo yenu. Ahsante sana.

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. FREDY A. MWAKIBETE Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itayakubali maombi ya wananchi wa Halmashauri ya Busokelo ya kuifanya Halmashauri hiyo iwe Wilaya?

Supplementary Question 4

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Vilevile katika Wilaya ya Serengeti ni moja ya Wilaya kongwe ambayo kimsingi ni Wilaya ambayo iliizaa Bunda; na ni Wilaya ambayo ina changamoto kubwa sana kijiografia, ni Wilaya ambayo ni kubwa kwa eneo, pia, ni Wilaya ambayo ina kata nyingi kweli.
Je, ni lini Wilaya hii itagawanywa kuwa Wilaya mbili?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba tuweke kumbukumbu sawa, hapa ukiwa unajibu maswali haya lazima kidogo akili yako ikae vizuri. Kwa sababu Wabunge wengine wanasema maeneo yasigawanywe, wengine
wanasema maeneo yagawanywe.
Mheshimiwa Mbunge, nadhani unakumbuka siku ile tulienda wote mpaka usiku tumetoka kule tukiwa Serengeti kwako. Ni kweli Kata zako zimekuwa scattered sana, ndiyo maana nalifananisha Jimbo lako na lile Jimbo la Ngorongoro, ukiingalia jiografia yake ni jiografia yenye changamoto kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutaangalia jinsi gani tutafanya kwa sababu Serikali hii hatuwezi kugawanya kila maeneo tu, ni lazima kuangalia jinsi gani kuweza kuyahudumia yale maeneo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pale kwenye haja na michakato halali na vikao vyetu huko ambako mamlaka tulizopita mamlaka za Wilaya na mamlaka za Mikoa, zikifanya maamuzi hayo basi jambo hilo litakuja katika Ofisi ya Rais TAMISEMI na Waziri wangu ataliangalia, atalipima, pale atakapoona linakidhi basi atafanya maamuzi sahihi, kutokana na uhalisia wa eneo hilo.