Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Primary Question

MHE. JUMAA H. AWESO Aliuliza:- Zao la nazi ni kitega uchumi na chanzo cha mapato kwa wananchi wa Halmashauri ya Pangani lakini zao hili linashambuliwa sana na ugonjwa wa mnyauko ambao umeliathiri zao hilo kwa kiwango kikubwa:- Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kufanya tafiti kuhusu ugonjwa huo ili kupata dawa inayofaa ili kuwawezesha wakulima waweze kuendeleza kilimo hicho?

Supplementary Question 1

MHE. JUMAA H. AWESO: Mheshimiwa Spika, tunapozungumzia suala la minazi ndiyo uchumi na ndiyo maisha ya wananchi wa Pangani. Ukisoma majibu ya sasa wamefanya tafiti lakini hawajajua mdudu ambaye anaeneza ugonjwa huo na wala hakuna tiba kama UKIMWI. Kwa kuwa, mnazi ndiyo uchumi, je, Serikali haioni haja sasa ya kuangalia nchi ambazo zinalima zao hili la mnazi kwa wingi ili kupata ushauri kujua namna gani tunaweza kuokoa zao hili la mnazi. (Makofi) Swali la pili; naomba sasa nipate commitment ya Waziri kwa kuwa tunaona jitihada zinazofanyika mpaka sasa hakuna majibu sahihi yaliyoweza kupatikana. Je, ili kuweza kuwaokoa wananchi wa Pangani kuondokana na umaskini kwa nini wasitupe zao mbadala ili kuhakikisha kwamba badala la mnazi tuwe na zao ambalo linakimu maisha ya wananchi wa Pangani? Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI:
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba imechukua muda mrefu sasa mdudu anayeambukiza ugonjwa huo kuweza
kufahamika, lakini zaidi tiba kuweza kupatikana. Wizara na Serikali inaendelea kushirikiana na Taasisi za Kitaifa na
Kimataifa ili kuangalia namna ya kutafuta tiba ya ugonjwa huu.
Mheshimiwa Spika, tunashirikiana na Taasisi za nchi zinazoongoza kwa kuzalisha minazi kama nchi za Indonesia,
Ufilipino, India na Brazil ili kuangalia namna gani ya kuhakikisha kwamba ugonjwa huu tunautokomeza kama nilivyosema. Kwa sasa tunaangalia namna ya kudhibiti ili usiweze kuleta madhara makubwa zaidi wakati tunaendelea kutafuta tiba.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu Serikali kutafuta zao mbadala; nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali na Wizara inafahamu jitihada ambayo yeye pamoja na Mheshimiwa DC Zainab Abdallah wa Pangani wanafanya katika kuleta zao la korosho Pangani. Nilipotembelea Pangani miezi michache iliyopita niliona
jitihada kubwa zinazofanywa na Mheshimiwa Mbunge pamoja na DC na Halmashauri ili kujaribu kuwashawishi na
kuwahimiza wananchi wapande mikorosho kama zao mbadala wakati Serikali inaendelea kutafuta tiba ya ugonjwa
wa minazi.
Mheshimiwa Spika, vilevile Serikali inaendelea kuangalia namna gani tunaweza tukahimiza matumizi ya mazao mbalimbali yanayozalishwa na mnazi. Kwa sababu mnazi ndiyo zao la pekee duniani ambalo hakuna chochote
ambacho hakitumiki, kuanzia mizizi mpaka matunda yote inatumika. Kwa hiyo, tunajaribu kuhimiza kwa mfano
uchakataji wa mbata ili kuweza kutengeneza mafuta ya kupikia na kujipaka. Waheshimiwa Wabunge mnafahamu kwamba mafuta ya nazi hayana lehemu katika maana ya cholesterol wala hayana mzio katika maana ya allergy. Kwa hiyo, tunaangalia uwezekano wa kuendelea kutumia products za mnazi kama njia mojawapo ya kuwasaidia wakulima wa minazi.

Name

Yosepher Ferdinand Komba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMAA H. AWESO Aliuliza:- Zao la nazi ni kitega uchumi na chanzo cha mapato kwa wananchi wa Halmashauri ya Pangani lakini zao hili linashambuliwa sana na ugonjwa wa mnyauko ambao umeliathiri zao hilo kwa kiwango kikubwa:- Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kufanya tafiti kuhusu ugonjwa huo ili kupata dawa inayofaa ili kuwawezesha wakulima waweze kuendeleza kilimo hicho?

Supplementary Question 2

MHE. YOSEPHER F. KOMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Katika majibu ya msingi ya Waziri amesema ugonjwa unaotokana na minazi haujapatiwa ufumbuzi. Katika Mkoa wa Tanga, tuna Chuo cha MATI Mlingano, Chuo cha Utafiti. Je, Serikali ina mpango gani wa kukifufua kile chuo ili wakulima wa mazao mengine kama korosho, mkonge, michungwa waweze kupata uhakika wa mazao yao?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI:
Mheshimiwa Spika, tunafahamu umuhimu wa Chuo na Kituo cha Utafiti cha Mlingano. Mimi mwenyewe katika ziara yangu ya Mkoa wa Tanga nilipata fursa ya kutembelea pale, kuangalia changamoto zilizopo na tayari Wizara iko kwenye mkakati wa kutatua changamoto mbalimbali ambazo tuligundua katika kituo hicho ili iweze kuwasaidia wakulima wa Mkoa wa Tanga na maeneo mengine ya Tanzania katika kuboresha kilimo.