Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED (K.n.y. MHE. KABWE Z. R. ZITTO) aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa kuzalisha umeme wa Malagarasi utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimwia Spika, kwa kuwa Mkoa wa Kigoma pamoja na Wilaya zake zinaingiza gharama kubwa sana katika Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kutumia majenereta, zaidi ya bilioni 160 kwa mwezi, kwa nini Serikali pamoja na Wizara ya Nishati na Madini isifanye haraka mradi huu ili kuokoa pesa kwa Mkoa wa Kigoma?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa shughuli za ugawaji wa umeme katika Mji wa Kigoma ni gharama kubwa na gharama alizozitaja Mheshimiwa Keissy kwa kweli ni kidogo siyo shilingi milioni 160 isipokuwa ni shilingi milioni 600 kila siku za mafuta tunatumia.
Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia uzito huo huo, ndiyo maana Serikali imesema itaanza ujenzi wa mradi huo wa Malagarasi ndani ya miezi sita kuanzia sasa, kuanzia mwezi Februari mwakani shughuli za ujenzi kwa ajili ya kuwapatia umeme wa uhakika wananchi wa Kigoma zitaanza. Kama nilivyosema shughuli hizi zitachukua miaka mitatu hivyo mwaka 2020 shughuli za ugawaji wa umeme katika Mji wa Kigoma zitakamilika na umeme utakuwa ni wa uhakika ambao haukatiki.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED (K.n.y. MHE. KABWE Z. R. ZITTO) aliuliza:- Je, ni lini Mradi wa kuzalisha umeme wa Malagarasi utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mchakato mzima wa uzalishaji umeme katika Mto Malagarasi umetumia vilevile fedha za Mfuko wa Changamoto za Milenia (MCC I). Ninataka nifahamu kwamba watu wa MCC wamekuwa wakipeleka fedha zao nyingi kwenye mradi wa umeme, na sasa hivi wamejitoa.
Je, sasa Serikali itupe commitment ya miradi yote ya umeme ambayo fedha zake zilikuwa za MCC, sasa Serikali itatumia vyanzo gani kuhakikisha kwamba miradi iliyopangwa inakamilika kwa wakati.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge kwamba MCC wamejitoa kwenye mradi wa Awamu ya Pili, lakini kazi ya MCC iliyofanyika awamu ya kwanza ilifanyika vizuri, na pesa zote zilitumika. Sasa Serikali inafanyaje.
Mheshimiwa Spika, katika awamu ya mradi huu wa 2016/2017, nichukue mfano kwa Mto Malagarasi shilingi bilioni moja ilikuwa ni fedha za ndani, lakini dola za Marekani bilioni moja pamoja na zingine dola za Marekani bilioni tatu zitafadhiliwa na World Bank pamoja na Benki ya Dunia ya Maendeleo.
Mheshimiwa Spika, pamoja na MCC kujitoa halijaharibika jambo. Ahsante sana.