Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO Aliuliza:- Serikali iliahidi kujenga Barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mpanda hadi Uvinza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi huo?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza niishukuru Serikali kwa jitihada ambazo zimefanywa, barabara ile imeanza kujengwa, lakini Serikali iliahidi barabara hiyo inapojengwa ingejengwa sambamba na kilometa 60 za kutoka Uvinza kuja eneo la Mishamo ili ziweze kuendana na kasi ya Mheshimiwa Rais na vile vile Ilani ya Chama cha mapinduzi. Je, ni lini eneo hilo la kipande cha kilometa 60 kutoka Uvinza kuja Mishamo kitaanza kujengwa?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa ujenzi wa barabara ulishaanza, tayari Serikali imetathmini wale ambao wamefuatwa na barabara. Ni lini wale ambao walioathirika kwa kufuatwa na barabara wataanza kulipwa?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, ni kweli tuliahidi kwamba tungejenga kuanzia Uvinza na vile vile kuanzia huku ambako tumeanzia na nimuahidi tu kwamba, madam tumeanza kupata hizi fedha kwa ajili ya upande mmoja, tumeona tuanze hii wakati tunaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ule upande wa pili. Nimhakikishie mara tu tutakapozipata fedha tutatekeleza ahadi tuliyoitoa.
Mheshimiwa Spika, kuhusu watu ambao wameifuata barabara; nimhakikishie tu Mheshimiwa Selemani Kakoso na wananchi husika kwamba watu wote walioifuata barabara hawatalipwa fidia na wale wote ambao barabara imewafuata watalipwa fidia; na taratibu za kuwatambua zilishafanyika na nimhakikishie kwamba hilo tutalitekeleza.

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO Aliuliza:- Serikali iliahidi kujenga Barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mpanda hadi Uvinza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi huo?

Supplementary Question 2

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Spika ahsante kwa kunipa nafasi. Tatizo la ujenzi wa barabara lililopo Mpanda hadi Uvinza halina tofauti na tatizo la ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami lililopo Mbinga hadi Nyasa. Barabara ile iliahidiwa na Serikali kwamba itajengwa, napenda kujua ni lini sasa ujenzi ule utaanza? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Chikambo, kama ambavyo nilimweleza alipofika ofisini mbele ya Waziri wangu akifuatilia utekelezaji wa barabara hii akiongozana na Mheshimiwa Stella Manyanya, Mbunge wa Nyasa, kwamba barabara hii inaanza kujengwa mwaka huu wa fedha.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu kwamba tumechelewa katika taratibu za Procurement kwa sababu nafahamu fedha zinazotarajiwa kujengea barabara hii zinatoka African Development Bank na kwamba wao wana utaratibu wao wa Procurement, ni lazima tuufuate. Tumechelewa lakini tutahakikisha mara tutakapokamilisha taratibu za Procurement barabara hiyo itaanza kujengwa.