Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Selemani Moshi Kakoso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mpanda Vijijini
Primary Question
MHE. MOSHI S. KAKOSO Aliuliza:- Serikali iliahidi kujenga Barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mpanda hadi Uvinza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi huo?
Supplementary Question 1
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza niishukuru Serikali kwa jitihada ambazo zimefanywa, barabara ile imeanza kujengwa, lakini Serikali iliahidi barabara hiyo inapojengwa ingejengwa sambamba na kilometa 60 za kutoka Uvinza kuja eneo la Mishamo ili ziweze kuendana na kasi ya Mheshimiwa Rais na vile vile Ilani ya Chama cha mapinduzi. Je, ni lini eneo hilo la kipande cha kilometa 60 kutoka Uvinza kuja Mishamo kitaanza kujengwa?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa ujenzi wa barabara ulishaanza, tayari Serikali imetathmini wale ambao wamefuatwa na barabara. Ni lini wale ambao walioathirika kwa kufuatwa na barabara wataanza kulipwa?
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, ni kweli tuliahidi kwamba tungejenga kuanzia Uvinza na vile vile kuanzia huku ambako tumeanzia na nimuahidi tu kwamba, madam tumeanza kupata hizi fedha kwa ajili ya upande mmoja, tumeona tuanze hii wakati tunaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ule upande wa pili. Nimhakikishie mara tu tutakapozipata fedha tutatekeleza ahadi tuliyoitoa.
Mheshimiwa Spika, kuhusu watu ambao wameifuata barabara; nimhakikishie tu Mheshimiwa Selemani Kakoso na wananchi husika kwamba watu wote walioifuata barabara hawatalipwa fidia na wale wote ambao barabara imewafuata watalipwa fidia; na taratibu za kuwatambua zilishafanyika na nimhakikishie kwamba hilo tutalitekeleza.
Name
Sikudhani Yasini Chikambo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MOSHI S. KAKOSO Aliuliza:- Serikali iliahidi kujenga Barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mpanda hadi Uvinza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi huo?
Supplementary Question 2
MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Spika ahsante kwa kunipa nafasi. Tatizo la ujenzi wa barabara lililopo Mpanda hadi Uvinza halina tofauti na tatizo la ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami lililopo Mbinga hadi Nyasa. Barabara ile iliahidiwa na Serikali kwamba itajengwa, napenda kujua ni lini sasa ujenzi ule utaanza? Ahsante.
Name
Eng. Edwin Amandus Ngonyani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Namtumbo
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Chikambo, kama ambavyo nilimweleza alipofika ofisini mbele ya Waziri wangu akifuatilia utekelezaji wa barabara hii akiongozana na Mheshimiwa Stella Manyanya, Mbunge wa Nyasa, kwamba barabara hii inaanza kujengwa mwaka huu wa fedha.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu kwamba tumechelewa katika taratibu za Procurement kwa sababu nafahamu fedha zinazotarajiwa kujengea barabara hii zinatoka African Development Bank na kwamba wao wana utaratibu wao wa Procurement, ni lazima tuufuate. Tumechelewa lakini tutahakikisha mara tutakapokamilisha taratibu za Procurement barabara hiyo itaanza kujengwa.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved