Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO Aliuliza:- Jimbo la Njombe lina Mahakama ya Mwanzo moja tu iliyopo Njombe Mjini. Je, Serikali ipo tayari kukarabati Mahakama za Mwanzo za Mahenye na Igominyi ili wananchi waweze kupata huduma hiyo jirani?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Spika ahsante kwa kunipa nafasi. Nashukuru kwa majibu mazuri
ya Serikali, nina maswali madogo mawili ya nyongeza:-
Pamoja na Mahakama hiyo lakini liko tatizo kubwa sana la Mabaraza ya Kata. Mabaraza ya Kata yamekuwa ni
mwiba mchungu sana kwa wananchi katika maeneo mbalimbali na hasa hasa katika Jimbo la Njombe. Kinachosababisha, moja; ni kukosa weledi. Je, Serikali sasa ipo tayari kuajiri mtaalam mmoja mmoja katika Mabaraza ya Kata ili asaidiane na wale wananchi wanaokuwa wajumbe wa Mabaraza haya ili kupunguza matatizo
yanayojitokeza kwa kukosa utaalam?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, Serikali ipo tayari kutoa mafunzo kwa wajumbe wa Mabaraza haya ya Kata ili
kusudi wanapofanya kazi zao za kusuluhisha migogoro mbalimbali kwa wananchi wawe na uelewa? Ahsante.

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa kuhusiana na kuongeza idadi ya watumishi katika mabaraza ya kata. Nimhakikishie tu kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI imekuwa ikifanya kazi nzuri katika kuyasimamia mabaraza haya na lengo kubwa ni kuhakikisha kwamba Mabaraza haya ya Kata pamoja na Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya pamoja na mahakama zetu zote zinasogeza huduma karibu zaidi na wananchi kwa kuwa na miundombinu, vitendea kazi, lakini pia kuwa na watumishi wa kutosha kwa hiyo, nimhakikishie tu kwamba tunalipokea, tutalifanyia kazi na Ofisi ya Rais, TAMISEMI.
Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili, kwamba, endapo Serikali tupo tayari kutoa mafunzo kwa watendaji
hawa katika Mabaraza ya Kata; nimhakikishie ndiyo na Ofisi ya Rais TAMISEMI imekuwa ikifanya hivyo kila mara ili
kuhakikisha kwamba wanaenda na wakati, wanafahamu sheria na masuala mengine wanayosimamia.
Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. EDWARD F. MWALONGO Aliuliza:- Jimbo la Njombe lina Mahakama ya Mwanzo moja tu iliyopo Njombe Mjini. Je, Serikali ipo tayari kukarabati Mahakama za Mwanzo za Mahenye na Igominyi ili wananchi waweze kupata huduma hiyo jirani?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa tatizo lililopo Njombe linafanana kabisa na tatizo lililopo katika Kata ya Mtae Jimbo la Mlalo Wilayani Lushoto. Je, ni lini Serikali itayakarabati majengo yale machakavu ya Mahakama ile ya mwanzo Mtae?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwanza kabisa nimhakikishie tu kwamba, azma ya Serikali kupitia Mahakama ni kuhakikisha kwamba tunasogeza huduma za mahakama karibu zaidi na wananchi. Ukiangalia tu katika mwaka huu wa fedha ambao tunaumaliza Serikali ilitenga zaidi ya Shilingi bilioni 46.5 na hata katika mwaka huu wa fedha ambayo bajeti yake tunaanza nayo zaidi ya Shilingi bilioni 18.1 pia zimetengwa kwa ajili ya kujenga mahakama mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaliona suala hili, tutakwenda kuliangalia; lakini katika mahakama ambazo ziko katika utaratibu kwa mwaka huu tunaomalizana nao ni ujenzi wa Mahakama Kuu, Tanga ambako na yeye pia anatoka, tunakamilisha ukarabati huo. Vile vile tunakamilisha ukarabati katika
Mahakama Kuu, Dar es Salaam lakini pia tunaanza ujenzi katika Mahakama Kuu, Mara pamoja na Kigoma na vile vile tunakamilisha ujenzi wa Mahakama za Wilaya Bagamoyo, Kigamboni na Mkuranga.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Mahakama za Mwanzo tunakamilisha ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo
Kawe pamoja na Kinyerezi, vile vile katika mwaka huu wa fedha, zaidi ya Mahakama za Mwanzo 10 zitaweza kujengwa na kukarabatiwa.