Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) walipewa kandarasi ya kujenga Ofisi na Makazi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe lakini ujenzi huo umesimama. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza tena ujenzi huo na kuukamilisha kupitia TBA?

Supplementary Question 1

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali hata hivyo nina maswali
mawili kama ifuatavyo:-
(a) Serikali kupitia kwa Naibu Waziri imekiri kwamba ni asilimia 23 tu ya zoezi zima la ujenzi wa nyumba za Wakuu
wa Wilaya na Mikoa ndizo zilizokuwa zimetekelezwa. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuhakikisha kwamba hizi nyumba zinakamilika kwa wakati katika mwaka wa fedha ujao?
(b) Je, Serikali imepanga kiasi gani cha fedha kwa Wilaya ya Mbogwe katika mwaka ujao wa fedha? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika
jibu la swali la msingi kwamba kuna kiwango cha fedha ambazo TBA wanahitaji kuzipata ili waweze kukamilisha zoezi hili la ujenzi. Naomba tu kama nilivyosema kwamba fedha zimetengwa katika mwaka huu wa 2017/2018 na niombe radhi sina kile kiwango kamili kilichotengwa chini ya TAMISEMI tutaweza kukupa hizo taarifa baadaye baada ya kuwasiliana na watu wa TAMISEMI kujua kiasi gani kimetengwa. Lakini nina uhakika na nimepata taarifa kutoka TBA kwamba mwaka huu wa fedha unaokuja wanaanza kujenga nyumba hizo hadi kuzikamilisha kwa sababu wameahidiwa kupata fedha zilizobakia zote.

Name

Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) walipewa kandarasi ya kujenga Ofisi na Makazi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe lakini ujenzi huo umesimama. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza tena ujenzi huo na kuukamilisha kupitia TBA?

Supplementary Question 2

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tatizo linaloikabili Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe linafanana na linaloikabili
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, lakini tofauti iliyoko kati ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe na ile ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga imekwishakujengwa takribani zaidi ya miaka mitano iliyopita, imekwisha kuezekwa, isipokuwa mpaka sasa haijamalizika kwa kutopakwa rangi, haijawekwa madirisha, haijawekwa mfumo wa wiring pamoja na milango na madirisha ambapo thamani ya umaliziaji huo inakadiriwa kuwa 300,000,000. Waziri anawahakikishiaje wananchi wa Wilaya ya Mbinga kwamba mwaka huu hautaisha mpaka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga inakamilika? Kwa sababu inapozidi kukaa zaidi ya miaka mitano inazidi kupoteza ubora, inakuwa ni nyumba ya popo, bundi na kadhalika ambayo siyo malengo ya ujenzi wa ile ofisi?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nilijibu swali la msingi, na bahati nzuri nyumba anayoongelea ina uhusiano wa moja kwa moja na swali la msingi, kwamba
mwaka ujao wa fedha 2017/2018 TBA imeahidiwa kupata fedha kutosha na itakamilisha majengo ambayo imeyaanza.
Aidha, nikupongeze, maana sikutengemea utarudia tena kuliuliza hapa wakati ulishakuja ofisini na tukaongea kwa
kirefu.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) walipewa kandarasi ya kujenga Ofisi na Makazi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe lakini ujenzi huo umesimama. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza tena ujenzi huo na kuukamilisha kupitia TBA?

Supplementary Question 3

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, hivi karibuni TBA walikabidhiwa maeneo ambayo yalikuwa ya National Housing ambayo
yalikuwa katika Halmashauri zetu ili waweze kufanya ujenzi mbalimbali. Lakini kwa bahati mbaya maeneo haya ambayo TBA wamekabidhiwa yaliyokuwa tayari yanatumika na Halmashauri zetu, mfano ni eneo la National Housing lililoko pale Mji wa Babati ambalo linatumika na vijana wetu wa Machinga. Ombi hilo tulishapeleka Waziri ya Ardhi, lakini sasa maeneo yale yamekabidhiwa TBA ambayo iko Wizara ya Ujenzi.
Naomba nifahamu Serikali au Wizara ya Ujenzi iko tayari na TBA kupokesa maombi yetu tena ili eneo hilo la
National Housing libaki kwa vijana wetu wa Machinga wasisumbuliwe kama ambavyo kauli ya Rais imesema?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, Wizara yangu iko tayari
kupokea hayo maombi kama ambavyo umesema na tutayaangalia kwa maslahi mapana ya nchi.