Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. MBARAKA K. DAU aliuliza:- Ujenzi wa barabara ya Kilindoni - Utende (Airport Access Road) yenye urefu wa kilometa 14 umekamilika, lakini mkandarasi CHICO ameijenga barabara hiyo chini ya viwango kwani ina viraka vingi. Je, ni lini Serikali itaitaka kampuni hiyo kufanya marekebisho makubwa?

Supplementary Question 1

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwanza Naibu Waziri anakiri kwamba barabara ile imejengwa chini ya kiwango;
lakini Naibu Waziri atakubaliana na mimi, alipotembelea Mafia tuliikagua barabara hii mimi na yeye. Barabara hii si ya kufanyiwa matengenezo makubwa, ni ya kurudiwa upya.(Makofi)
Mheshimiwa Spika, ng’ombe akikatisha kwenye barabara anaacha mashimo, barabara ya lami! Gari likipata
puncture ukipiga jeki, jeki inakwenda chini kama unapiga jeki kwenye tope, kule Mafia wanaiita barabara ya big G
(chewing gum).
Mheshimiwa Spika, sasa nina maswali mawili. Swali la kwanza; kwa kuwa Serikali inakiri kwamba mkandarasi
huyu ameijenga chini ya kiwango, ni hatua gani za kimkataba na za kisheria zimechukuliwa dhidi ya huyu
mkandarasi aliyeisababishia Serikali hasara? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, wananchi wa maeneo ya Kilindoni, Kiegeyani na Utende ambao wahanga wa kubomolewa nyumba zao, wengine walikuwa ni wahanga wa kubomolewa nyumba zao, wengine wamekatiwa minazi yao na mikorosho yao na mazao yao mbalimbali, mpaka leo wengi wao hawajalipwa fidia kutokana na ujenzi wa barabara ile, ningependa nisikie kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri, nini hatma ya waathirika hawa wa fidia? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri kwamba
nilikuwa Mafia na Mheshimiwa Dau na tuliikagua hiyo barabara. Lakini namuomba tu asiongeze utani sana ndani
ya Bunge, maeneo machafu ni machache ambayo yameshaainishwa na kwa mujibu wa mkataba tumeshachukua hatua ya kumlazimisha mkandarasi kurudia maeneo hayo kwa gharama zake.
Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu fidia; nimuombe Mheshimiwa Kitwana Dau, kwamba yale tuliyoongea Mafia
ayazingatie. Nikuhakikishie yeyote mwenye haki ya kulipwa fidia atalipwa. Sehemu ya wengi tunaowaongelea pale ni
wale ambao waliifuata barabara.

Name

Suleiman Ahmed Saddiq

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. MBARAKA K. DAU aliuliza:- Ujenzi wa barabara ya Kilindoni - Utende (Airport Access Road) yenye urefu wa kilometa 14 umekamilika, lakini mkandarasi CHICO ameijenga barabara hiyo chini ya viwango kwani ina viraka vingi. Je, ni lini Serikali itaitaka kampuni hiyo kufanya marekebisho makubwa?

Supplementary Question 2

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona, lakini vilevile niipongeze sana
Wizara hii.
Katika Serikali ya Awamu ya Nne kupitia Ilani yetu ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi iliweka ahadi kwamba
itaweka lami barabara ya kutoka Korogwe - Kwa Shemshi - Dindila - Bumbuli hadi Soni, lakini mpaka leo hii hakuna ufafanuzi wowote wa kujengwa kwa lami. Nataka Serikali iwahakikishie wananchi kule kwamba barabara ile ni lini sasa itajengwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, hii barabara anayoizungumzia ya kuanzia Korogwe kuelekea Bumbuli – Dindila mpaka kule mwisho ni barabara ambayo amekuwa akiiongelea mara nyingi kuanzia kipindi cha bajeti ya mwaka jana. Nimhakikishie tu yale ambayo tulimueleza, kwamba barabara hii kwanza itaanza kujengwa kutokea Korogwe, kama ambavyo usanifu ulionesha.
Mheshimiwa Spika, lakini la pili, nimhakikishie kwamba haya anayoyasikia kuhusu hii barabara sio kweli. Serikali ina dhamira ya dhati ya kutekeleza ahadi yake ya kuijenga hii barabara kwa lami. Kama nilivyomueleza mara nyingi tu ofisini na maeneo mengine na hata alipomuona Waziri wangu, nikupongeze sana kwa namna unavyofuatilia kwamba barabara hii tutaijenga baada ya kukamilisha hizi barabara ambazo sasa hivi zinatuletea madeni mengi, tunataka tuziondoe kwanza hizo ili tuzianze hizi nyingine, lakini kimsingi katika miaka hii mitano ahadi hiyo tutaitekeleza.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MBARAKA K. DAU aliuliza:- Ujenzi wa barabara ya Kilindoni - Utende (Airport Access Road) yenye urefu wa kilometa 14 umekamilika, lakini mkandarasi CHICO ameijenga barabara hiyo chini ya viwango kwani ina viraka vingi. Je, ni lini Serikali itaitaka kampuni hiyo kufanya marekebisho makubwa?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na wakandarasi kujenga barabara chini ya kiwango au kukarabati barabara
chini ya kiwango si jambo geni na Mheshimiwa Spika, na wewe ni shahidi barabara ya kutoka Morogoro kuja hapa
Dodoma sasa hivi tayari imeshavimba, Wabunge wote mnajua. Lakini hiyo barabara ninayoitaja pia inapita Jimboni
kwako, nadhani shahidi tayari sasahivi imeshaanza kuvimba, nimeona tu nikuulizie bosi wangu.
Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge pia mashahidi, ukarabati unaofanywa hata kwenye barabara
za hapa Dodoma, Area D, Area C pia uko chini ya kiwango, unaigharimu sana Serikali kuwa tunakarabati barabara mara kwa mara pindi Waheshimiwa Wabunge wanapokuja Dodoma.
Mheshimiwa Spika, kingine, barabara ya kutoka Musoma – Bunda na yenyewe pia, ilishaharibika kabla hata
ya kukabidhiwa.
Swali langu, je, mna mkakati gani katika barabara mpya ya kutoka Kisorya - Bunda Mjini - Nyamswa, ambayo
bado haijajengwa, inajengwa kwa kiwango cha lami, ili barabara hiyo isiigharimu Serikali fedha za kutosha na iwe ya kiwango? Naomba jibu zuri na ujue unamjibu Waziri Kivuli na Mjumbe wa Kamati Kuu.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, nimechanganyikiwa kwa sababu swali ninalotakiwa nilijibu ni moja, sijui ni jibu lile la Mbande, niache lile la Kisorya au nijibu la Kisorya niache haya ya Mbande?
SPIKA: Nimekuachia kama Engineer nikajua tu utapata moja la kujibu hapo.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, barabara ya kutoka
Morogoro hadi Dodoma na viunga vya Dodoma huwa zinajengwa kwa kufuata mikataba. Katika ile mikataba kuna
viwango ambavyo vinawekwa kwa mkataba na kutokana na kiwango cha fedha. Kwa hiyo, mimi nimhakikishie
Mheshimiwa Ester Bulaya kwamba barabara hizi za kutoka Morogoro hadi Dodoma, pamoja na Dodoma Mjini,
tunahakikisha kwamba kile kiwango cha mkataba kinafikiwa. Nichukue nafasi hiyo kuwapongeza watu wa
TANROADS kwa kuhakikisha kwamba wanasimamia kwa kiwango kikubwa na pale inapotokea mkandarasi
aliyetengeneza hajafikia kiwango, hatua bhuwa zinachukuliwa.

Name

Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MBARAKA K. DAU aliuliza:- Ujenzi wa barabara ya Kilindoni - Utende (Airport Access Road) yenye urefu wa kilometa 14 umekamilika, lakini mkandarasi CHICO ameijenga barabara hiyo chini ya viwango kwani ina viraka vingi. Je, ni lini Serikali itaitaka kampuni hiyo kufanya marekebisho makubwa?

Supplementary Question 4

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Spika,
nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, hii barabara ambayo Mheshimiwa Dau ameisema, wenzenu ndiyo ilikuwa lami ya kwanza
tumeiona katika miaka 50 ya uhuru, kwa hiyo, ilipoharibika baada ya siku chache kwa kweli tumeumia. Sasa hii barabara ukitoka pale round about ya Kilindoni kwenda Utende ni kwamba zaidi ya theluthi mbili ya barabara ni mbovu. Sasa
nashangaa Mheshimiwa Naibu Waziri anavyotwambia
kwamba ni sehemu chache.
Sasa swali langu, je, Mheshimiwa Waziri
atatuhakikishia ushirikishwaji uliokamili wa wadau wote wa
Mafia na watumiaji wa barabara ile kabla ya hiyo kazi ya
kuanza ukarabati ili na sisi tujue hilo andiko mlilosema ninyi
mapungufu machache na kazi itafanyika kwa kiasi gani?
Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, nakubali, tutashirikisha wadau na kwa taarifa hii TANROADS Mkoa wa Pwani wawashirikishe wadau wa Mafia kabla CHICO hajaanza kurekebisha yale maeneo ambayo yamegundulika yana matatizo.