Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:- Je, ni nini umuhimu wa kurasimisha ardhi kwenye maeneo ambayo hayajapimwa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.
Mheshimiwa Spika, japo nia ya Serikali ni njema kurasimisha ardhi kwenye maeneo ambayo hayajapimwa,
lakini kuna concern kwamba tunakuwa tunaendeleza squatters, maeneo ya wazi ambapo miundombinu inakuja
kuwa challenge. Sasa badaye mnapotaka ku-implement mambo ya mipango miji au ramani zetu tulizonazo kutakuwa kuna gharama tena husika za kubomolea watu. Je, Serikali nimezingatia hili? Asante.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ni kweli anachozungumza nadhani kama nimejibu vizuri, ulinisikiliza wakati najibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Allan, si nia ya Serikali kuona kwamba miji inaendelea kuharibika kwa kuendeleza squatter na ndiyo maana nimewaomba Waheshimiwa Wabunge kwa sababu wote ni Wajumbe wa Baraza la Madiwani katika Halmashauri zetu, pale ambapo Serikali imeanza kufanya zoezi la urasimishaji katika maeneo ni jukumu la kila Halmashauri kuhakikisha kwamba wanasimamia maeneo yao ili kusiwe na muendelezo wa ujenzi holela. Kwa sababu zoezi hili linapaswa kusimamiwa na Halmashauri zenyewe husika, Wizara sio rahisi kushuka kila maeneo.
Mheshimiwa Spika, ni kweli zoezi tunalifanya na inaonekana ni zuri, lakini tusingependa kuona ujenzi holela
unaendelezwa. Sasa ujenzi huu utasimama pale ambapo kila halmashauri itawajibika katika eneo lake kuhakikisha inakuwa na michoro ya mipango miji kwenye maeneo yao na kusimamia zoezi la ujenzi holela lisiendelee katika maeneo yao. Tukifanya hivyo, miji yetu itakuwa salama na itakuwa inapendeza.

Name

Maulid Said Abdallah Mtulia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:- Je, ni nini umuhimu wa kurasimisha ardhi kwenye maeneo ambayo hayajapimwa?

Supplementary Question 2

MHE. MAULID S. A. MTULIA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kupata fursa hii ya kuuliza swali la nyongeza.
Mimi katika maeneo yangu ya Jimbo langu la Kinondoni, hasa Magomeni Mtaa wa Kwa Suna, Hananasifu
Mtaa wa Mkunguni na mitaa mingine, nyumba za wananchi zilifanyiwa urasimishaji, lakini kwa masikitiko makubwa watu wakatumia fursa ile wengine kwenda kukopa. Nasikitika kwamba Serikali imeenda kuvunja nyumba zile bila kulipa fidia kwa wananchi wale.
Je, kwa nini Serikali inavunja nyumba zilizofanyiwa urasimishaji na kupata leseni za makazi bila kulipa fidia?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, anachokizungumza ni kweli, kuna maeneo yalifanyika hivyo, lakini suala la msingi hapa kupewa leseni ya makazi haina maana ya kwamba pale ambapo utaratibu wa mipango miji umeyapanga vinginevyo yale maeneo hautavunjiwa. Kwa sababu Dar es Salaam yenyewe sasa hivi iko katika mchakato na ninadhani imekamilisha mpango wa master plan ya mji ule.
Sasa pale ambapo inaonekana kabisa kwamba kuna suala zima la kutaka kuweka miundombinu inayofaa katika
eneo lile watu hawa wanaweza kuvunjiwa katika maeneo yao.
Mheshimiwa Spika, lakini Wizara ilishatoa tangazo kwa wale ambao walikuwa na umiliki halali na wana hati
kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na wamevunjiwa kimakosa, tulisema walete orodha yao na watu wa mipango miji watakwenda kuhakiki waone kweli walivunjiwa kimakosa. Lakini kwa wale ambao waliendelea na ujenzi bila kuzingatia mipango miji imepanga nini katika ule mji hao hawatalipwa na itakuwa ni tatizo. Watu wa Hananasifu na Mkunguni kama alivyosema, kama hao wapo kulingana na maelezo niliyoyatoa, basi tupate wakiwa na hati zao kutoka Wizarani kwetu au kutoka kwenye ma nispaa inayohusika, tutawa-consider kulingana na malalamiko watakavyokuwa wameyaleta.

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:- Je, ni nini umuhimu wa kurasimisha ardhi kwenye maeneo ambayo hayajapimwa?

Supplementary Question 3

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuweza kunipatia nafasi ya kuuliza swali.
Kufuatia majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, je, ni lini Wizara itashuka chini kwenye Halmashauri mpya kama
vile Mkalama, ikarasimisha maeneo ya wananchi kwa sababu kuna miji midogo inayochipua ambapo wananchi wanahitaji maeneo yao yarasimishwe ili waweze kupata mikopo na ardhi yao iwe na thamani?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, mimi ningependa kushauri halmashauri mpya zinazoanzishwa, tusikimbilie kwenye suala la urasimishaji, kwa sababu urasimishaji si suluhu ya kupanga miji yetu. Mimi ninachomshauri Mheshimiwa waingie katika maandalizi ya kuwa na mpango kabambe wa kupanga mji wao, ili miji hii yote mipya inayoanza ianze katika mpangilio mzuri wa mipango miji na si kuanza zoezi la kurasimisha. Lakini kwa maeneo ambayo tayari yameshaendelezwa bila kufuata taratibu za mipango miji tutakuwa tayari kushiriki pamoja nao katika kuhakikisha kwamba tunafanya zoezi la urasimishaji, lakini wakati huo huo waingie katika mpango wa maandalisi ya mpango kabambe.

Name

Salma Mohamed Mwassa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA M. MWASSA aliuliza:- Je, ni nini umuhimu wa kurasimisha ardhi kwenye maeneo ambayo hayajapimwa?

Supplementary Question 4

MHE. SALMA M. MWASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza naishukuru Serikali kwa kutambua umuhimu wa urasimishaji, lakini naomba itekeleze kwa vitendo.
Mheshimiwa Spika, ili kupunguza migogoro ya ardhi suluhisho muhimu ni kupima, kupanga na kurasimisha na si
vinginevyo. Kumekuwa na miradi ya urasimishaji, kwa mfano mradi unaondelea sasa hivi katika Jiji la Dar es Salaam Kimara, mradi ule ni kama umetelekezwa. Wafanyakazi wale hawana hela za kwenda site, hawana mafuta na wala hawana vitendea kazi vyovyote katika.
Mheshimiwa Spika, kama hivi ndivyo sasa tuone kwamba kurasimisha inakuwa ni sehemu ya kufanya thamani
za ardhi zile kupanda hasa katika Jiji la Dar es Salaam ambako squatter sasa hivi katika Jiji la hilo ni tatizo kubwa.
Watu wanajenga hovyo, mji unachafuka, haupangwi inavyostahili.
Mheshimiwa Spika, sasa huu mradi uliokuwa pilot area kwa ajili ya Dar es Salaam ambao sasa ungeweza
kufanya huko kwenye mikoa mingine. Sasa ni kwa nini Serikali haipeleki fedha kwenye mradi ule na kutoutelekeza kama ilivyo sasa? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali namba la pili, katika miradi ile ya MKURABITA kwenye urasimishaji huo huo, wananchi
walilipa fedha zao huko huko Kimara, wamelipa kati ya shilingi 400,000 mpaka 800,000. Wananchi wale bado wana zile risiti, sasa je, napenda Wizara inahakikishie ni lini hizo hela zitarudishwa kwa wananchi au kuwarasimishia ili waweze kuondokana na hiyo sintofahamu?
Mheshimiwa Spika, je, ni lini Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari kuongozana na mimi kwenda katika hiyo ofisi ya mradi hapo Kimara tuangalie hayo matatizo na mimi kama mtaalamu nimshauri?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Mwassa kwa kufuatilia, lakini vilevile Mheshimiwa Mwassa ni mmoja wa Wajumbe wa Kamati yetu ya Ardhi, Maliasili na Utalii. Amekuwa ni mstari wa mbele katika shughuli hizi na pia ni mwanataaluma hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba niseme kwamba kwa maswali yake mawili aliyoyauliza habari ya kutopeleka fedha
katika mradi wa Kimara si kweli. Naomba nisema zoezi la urasimishaji linaloendelea Kimara halijakwama kwa ajili ya pesa, limekwama kwa ajili ya wananchi wengine kutotoa ushirikiano; na hii inatakiwa pia Halmashauri zote kule ambako zoezi hili linafanyika tuwasihi wananchi wetu watoe ushirikiano.
Mheshimiwa Spika, kwa sababu suala la urasimishaji si la mtaalamu kwenda pale na kuamua nini kifanyike.
Anapokwenda katika eneo la mradi ni lazima ashirikishe viongozi waliopo lakini pia wale ambao wanapaka katika
yale maeneo yanayofanyiwa urasimishaji. Ikitokea mmojawapo akagoma au akakataa kukubaliana na kile
ambacho kinafanyika zoezi haliwezi kuendelea. Kwa hiyo, mimi niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge tuwasihi
wananchi wetu kwa sababu zoezi hili lina manufaa kwao na kwa nchi pia.
Mheshimiwa Spika, swali la pili amezungumzia habari ya MKURABITA, kuhusu habari ya kurudishiwa pesa.
Mheshimiwa Spika, miradi yote iliyoanzishwa na MKURABITA bado inaendelea kufanyika na hii ni kwa sababu
tu, kumekuwa na miradi mingi ambayo inaendelea katika maeneo ambapo baadaye MKURABITA walisimama
wenyewe, ikiwepo na ile Kusini, walisimama hawakuendelea na hilo zoezi kutokana na tatizo kama hilo hilo la mwanzo ambalo nimelizungumzia.
Mheshimiwa Spika, lakini kwa wale waliolipa pesa zao hakuna atakayedhulumiwa na wote tutawatambua. Kwa
hiyo mimi naomba kama unayo orodha, kwa sababu pale ofisini kwetu hatujawa na orodha, hatujaletewa malalamiko hayo kwa maandishi na kujua kwamba kuna watu wamechangia lakini hawajapewa huduma hiyo. Kwa hiyo mimi nitamwomba Mheshimiwa Mbunge alete orodha hiyo, na Waheshimiwa Wabunge wengine kama kwao kuna watu wenye madai hayo wayalete na ofisi itakuwa tayari kuyashughulikia.