Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Serikali ilipata mkopo kutoka Benki ya Dunia na kujenga miundombinu ya mradi wa mabasi yaendayo kasi Jijini Dar es Salaam. Baada ya ujenzi wa mradi huo kukamilika Serikali ilitoa msamaha wa baadhi ya kodi wakati wa uingizaji nchini mabasi yanayotumika kusafirisha abiria katika mradi huo. Serikali inamiliki asilimia 49 ya hisa za mradi huo na mwekezaji asilimia 51. (a) Wakati wa kukokotoa hisa kati ya Serikali na mwekezaji, je, sehemu ya msamaha imejumlishwa katika ukokotoaji wa hisa? (b) Je, ni nini faida na hasara za msamaha huo wa kodi upande wa Serikali? (c) Wakati wa kulipa mkopo huo, je, ni nini wajibu wa mwekezaji katika mkopo?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniruhusu kuuliza maswali mawili ya
nyongeza.
Mheshimiwa Spika, wakati naandika swali hili, nilitaka lijibiwe na Wizara ya Fedha na si kwamba nilikuwa nimekosea kwa kuitaka Wizara ya Fedha ijibu swali hilo.
Mheshimiwa Spika, ni ukweli usiopingika na Serikali wanakiri pale ambapo mwekezaji unampunguzia badala
ya kulipa asilimia 25 akalipa asilimia 10 maana yake hiyo ni pesa ambayo ingeweza kwenda kwa Watanzania, ni tax ambayo ilitakiwa kuwa imekusanywa, haikukusanywa.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, je, isingekuwa busara nafasi hiyo inekuwa imetolewa kwa Mtanzania awae
yeyote ambaye ananunua mabasi ya aina hiyo either anapeleka Mwanza, anapeleka Sumbawanga akaweza
kupata fursa kama hiyo?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, katika utaratibu wa Serikali kujenga barabara hizi kwa awamu ya kwanza
ambayo imeshakamilika sasa tunaenda awamu ya pili na mpak aya tatu, ni wazi kwamba Serikali itaendelea kuwekeza na katika hali ya kawaida ili muweze kugawana lazima kila mmoja aoneshe rasilimali ambayo amewekeza. Je, ni busara kwamba pamoja na uwekezaji ambao utaendelea kuwekwa na Serikali, bado mwekezaji huyu aendelee kumiliki asilimia 51 na Serikali ibaki na asilimia 49?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri yaliyotolewa na Naibu Waziri Mheshimiwa Jafo, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kandege kama ifuatavyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tufahamu kwamba mradi huu kwa nature yake ni PPP ni Public Private Partnership na kwa sababu ni PPP na kusema ukweli sisi hatuna uzoefu mkubwa sana wa miradi ya PPP hapa nchini, lakini PPP hii ni PPP ambayo kusema ukweli inagusa the public direct, kwa maana ya usafiri wa wananchi wa Dar es Salaam lakini PPP hii ni PPP ambayo inawahusisha kampuni ya Kitanzania na Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala la misamaha ni kweli jambo limekuwa likipigiwa kelele kuhusu misamaha.
Ipo misamaha mingi imetolewa na Bunge limekuwa likisema juu ya suala la misamaha. Lakini huu ni msamaha wa aina yake, tena ni kwa eneo ambalo linaleta unafuu kwa wananchi hao hao. Sasa mimi nimuombe tu Mheshimiwa
Kandege aje tumpe details zaidi za suala hili. Pengine swali hili aliliuliza muda mrefu uliopita kwa hiyo limeshabadilika sana na tumekwenda mbali zaidi.
Mheshimiwa Spika, lakini la pili ameuliza je, katika mwendelezo wa hatua zingine zinazofuata za uendelezaji wa mradi huu, umiliki wa kampuni hii binafsi na Serikali utabakia asilimia ile ile?
Mheshimiwa Spika, ninachotaka kusema tu kwamba katika hiyo asilimia 51 na asilimia 49 ni katika mradi huu wa
awamu hii kwa sababu ni kampuni inayoundwa na Serikali kwa maana ya Simon Group na Serikali wameunda kampuni inayo-operate mabasi haya ya UDART ambayo yanafanya usafiri Dar es Salaam.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo unaona Serikali katika kila hatua imo na ndiyo maana tusipokuwa makini na jambo
hili sio watu wote wanalipenda na hasa wenzetu. Kwa hiyo, ninaposema wenzetu sina maana upande wowote wa Bunge hapana, nina maana nje kwasababu wangependa PPP ya aina fulani. Nadhani mmenielewa.
Kwa hiyo, niwasihi sana Waheshimiwa Wabunge, hii ni PPP nzuri ambayo kila kitu kinabaki hapa hapa ingelikuwa
ni kampni imetoka Bogota imetoka wapi, hapo ndio lakini hii ni PPP nzuri na ninaomba sana kama Jiji waliuza hizi asilimia 51 na Serikali tumeweza ku-acquire, kwanza ilikuwa zaidi ya hapo; tumeweza ku-acquire back karibu hizi 49%. Tuendelee lakini ni kwa hatua ya awamu hii tu ndiyo wameshinda hii tender ya kuendesha hii na awamu zinazofuata na zenyewe zitakuwa procured kwa utaratibu mwingine.

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Serikali ilipata mkopo kutoka Benki ya Dunia na kujenga miundombinu ya mradi wa mabasi yaendayo kasi Jijini Dar es Salaam. Baada ya ujenzi wa mradi huo kukamilika Serikali ilitoa msamaha wa baadhi ya kodi wakati wa uingizaji nchini mabasi yanayotumika kusafirisha abiria katika mradi huo. Serikali inamiliki asilimia 49 ya hisa za mradi huo na mwekezaji asilimia 51. (a) Wakati wa kukokotoa hisa kati ya Serikali na mwekezaji, je, sehemu ya msamaha imejumlishwa katika ukokotoaji wa hisa? (b) Je, ni nini faida na hasara za msamaha huo wa kodi upande wa Serikali? (c) Wakati wa kulipa mkopo huo, je, ni nini wajibu wa mwekezaji katika mkopo?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa suala la usafiri Jijini Dar
es Salaam hasa public transport ni jambo nyeti na linawagusa wananchi wote kwa ujumla wao; kwa mazoea katika Majiji ya wenzetu Ofisi za Mameya zinahusika sana katika kusimamia usafiri katika Majiji yao. Kwa mfano katika Jiji la London Ofisi ya Meya wa Jiji la London inahusika mpaka kupanga ratiba za treni, ratiba za mabasi na route zenyewe.
Mheshimiwa Spika, nilitaka kujua kwanini katika Jiji la Dar es Salaam Ofisi ya Meya haihusishwi kwa namna yoyote
katika upangaji wa route au kusimamia usafiri katika Jiji la Dae es Salaam?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TA WALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimwa Spika, ni kweli huo ndiyo utaratibu wa Majiji mengi, lakini tatizo letu hapa ni historia ya UDA na Jiji la Dar es Salaam. Jiji la Dar es Salaam waliziuza hizi hisa kwa Kampuni ya Simon Group. Tumejaribu kutafuta namna ya kusaidia, ni Serikali Kuu ndio tuliojitahidi kurudisha asilimia 49 za kwetu maana za zenyewe zilitaka kupotolea huko. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, na kusema ukweli nimpongeze sana Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika jambo hili
tumeshirikiana vizuri. Pia nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa guidance zake mpaka tumeweza hata hizo asilimia 49 zenyewe zilikuwa ni kiini macho. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini Waheshimiwa Wabunge tukumbuke pia historia ya UDA ilivyokuwa, kilikuwa ni kitu
ambacho kimetupwa, kimeachwa huko lakini baadaye kimerudi na kuwa kitu chenye thamani leo ndiyo tunasema.
Waulize wao Jiji la Dar es Salaam wapo, wamewahi kwenda hata Mahakamani kudai kwamba uuzaji huu sio halali? Na kama walikwenda je, ilikuwaje? Na matokeo ya kesi yalikuwaje, mbona sasa hawasemi kwamba tunataka kuappeal?
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niwaombe sana, Jiji la Dar es Salaam is a legal entity. Wao wanaweza kushtaki na
kushtakiwa, wasije hapa Bungeni, maana walipouziana hawakuleta hapa Bungeni tukapitisha. Waende wakatafute
kama hawakuuza sawasawa waone wanavyoweza kufanya, lakini kwa sasa sisi kama Serikali Kuu tumeweza kurejesha asilimia 49 ya hisa zetu na zinaendeshwa kwenye mikono ya Serikali na tume-win tender ya ku-operate mabasi ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na huyo mwekezaji binafsi.

Name

Saed Ahmed Kubenea

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Ubungo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza:- Serikali ilipata mkopo kutoka Benki ya Dunia na kujenga miundombinu ya mradi wa mabasi yaendayo kasi Jijini Dar es Salaam. Baada ya ujenzi wa mradi huo kukamilika Serikali ilitoa msamaha wa baadhi ya kodi wakati wa uingizaji nchini mabasi yanayotumika kusafirisha abiria katika mradi huo. Serikali inamiliki asilimia 49 ya hisa za mradi huo na mwekezaji asilimia 51. (a) Wakati wa kukokotoa hisa kati ya Serikali na mwekezaji, je, sehemu ya msamaha imejumlishwa katika ukokotoaji wa hisa? (b) Je, ni nini faida na hasara za msamaha huo wa kodi upande wa Serikali? (c) Wakati wa kulipa mkopo huo, je, ni nini wajibu wa mwekezaji katika mkopo?

Supplementary Question 3

MHE. SAED A. KUBENEA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kabla ya kuuliza swali langu la nyongeza kwa ruhusa yako naomba niweke rekodi
sawasawa, kwamba hisa za Jiji la Dar es Salaam hazikuuzwa jana, ziliuzwa toka mwaka 2009 wakati sisi hatujawa katika uongozi wa Jiji la Dar es Salaam.
Kwa kuwa Waziri ameliambia Bunge kwamba ule mkataba wa uendeshaji wa usafirishaji wa Jiji la Dar es Salaam ni wa muda na kwamba wao Simon Group ndio wameshinda hiyo zabuni, lakini kwa kuwa mkopo uliojenga
miundombinu ya barabara za Jiji za Dar es Salaam umetolewa na Benki ya Dunia, na kwa kuwa mkopo ulionunua magari yaendayo kasi Dar es Salaam umetolewa na Benki ya NMB, na Serikali ndiyo dhamana wa Benki hiyo haoni kwamba sio halali kwa mtu mmoja kumiliki uendeshaji wa mabasi yaendayo kasi Dar es Salaam na kuacha wananchi wengine ambao wana mabasi madogo madogo kuachwa nje ya utaratibu?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza NMB ni ya nani? Serikali tuna hisa kwenye NMB. Kwa hiyo hakuna hata dhambi yoyote kwa NMB ku-facilitate, maendeleo ya usafiri wa Dar es Salaam. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini zile arrangement za NMB na huyu mwekezaji ambaye anaendesha mradi wa mabasi
yaendayo kasi Dar es Salaam ambaye ni Serikali na mwekezaji binafsi it is a PPP, ni mradi ambao una-arrangements zake.
Arrangements zile ni za kati ya UDART ambayo Serikali imo na Simon Group na benki na ujenzi wa miundombinu ni makubaliano ya Serikali na World Bank wala utaratibu wa uendeshaji haukuwa ni jambo muhimu sana, hapa ilikuwa ni kuboresha usafiri katika Jiji la Dar es Salaam.
Mheshimiwa Spika, Watanzania wanafahamu adha ya foleni ya Dar es Salaam, Watanzania wanafahamu namna
tunavyopoteza uchumi katika Jiji la Dar es Salaam, hivi kwa nini sisi Watanzani tuna-tend kuchukua PPP. Hatuwezi kujenga hii nchi kwa kutegemea Serikali peke yake. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, napenda sana fikra za baadhi ya Wabunge, fikra za kuamini kwamba private sector ni muhimu
katika ujenzi wa uchumi, na siogopi mimi kum-quote Mheshimiwa Zitto Kabwe kwamba ni mtu anayejua sana
eneo hilo la uchumi. Lakini Waziri wa Fedha amekuwa akieleza hapa eneo hilo, lakini bado sisi Watanzania
anaposhiriki mswahili katika shughuli yoyote ya PPP ni nongwa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nchi yetu haiwezi kuendelea kwa msingi huu, ila angekuja mgeni kutoka nje angeshangiliwa
kweli kweli, kwani hamjui kwamba kuna hisa nyingi zinachukuliwa kwenye makampuni ambayo Serikali ilitakiwa
kushiriki lakini tumeshindwa.
Mheshimiwa Spika, hatuwezi kuendelea na msingi huu wa kuendesha uchumi na uchumi ukaenda kama mawazo
yenyewe ndiyo haya.
Mheshimiwa Spika, Serikali inafahamu, imelinda maslahi yake na inafahamu mradi huu umuhimu zaidi si faida
bali huduma kwa wananchi wa Dar es Salaam.