Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamaliza kujenga mradi wa maji wa Sawala, Mtwango, Rufuna na Kibao?

Supplementary Question 1

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu WazirI ninaomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza kutangaza na kutafuta mkandarasi sasa hivi imeanza muda mrefu toka mwezi wa pili na imechukua karibu miezi sita sasa, ukisema mpaka Juni itachukua miezi sita. Swali langu, je, kutafuta
mkandarasi kisheria inatakiwa miezi mingapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Jimbo langu la Mufindi Kusini tuna tatizo kubwa sana la maji, ukizingatia Serikali ilijenga matenki ya maji katika kijiji cha Igowole, Nyororo, Idunda, Itandula, Kiyowela matenki haya yote yameharibika sasa hivi yana miaka karibu sita, je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha watu wa Igowole na Nyororo na
vijiji nilivyotaja vinaweza kupata maji na kukarabati mitandao ambayo imeharibika?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja anasema muda au mchakato wa kumpata Mkandarasi unakuwa mrefu sana unatumia muda gani; upo kwa mujibu wa sheria. Muda wa manunuzi upo kwa mujibu wa sheria ambayo ilipitishwa katika Bunge hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ni kuna matenki 11 yaliyojengwa na sasa hayana maji, ni kweli tatizo hili nilikuta pia Nanyamba, kuna matenki zaidi ya saba ambayo yalijengwa na AMREF na yalikuwa hayana maji. Matenki yale
yalikuwa yamejengwa pamoja na visima. Sasa jumuiya za watumiaji maji ambazo tuliziunda tumekuta changamoto ziko nyingi unakuta kulikuwa na pump, pump imekufa, kuna jenereta, jeneretaimekufa. Wakati mwingine kisima kinakuwa kimekosa maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa sasa nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunachokifanya sasa hivi tumefanya uchunguzi tukakuta kwamba hzi jumuiya zinaelekea kushindwa kufanya hii kazi; lakini sio kwamba ni
kwa sababu yao tu, hapana; ila ni kwa sababu ya
miundombinu iliyowekwa hawana uwezo wa kuiendesha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tumechukua
utaratibu wa kuweka solar na visima vilivyopo tutavisafisha maeneo yaliyokuwa na mtiririko tutayaweka vizuri kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma na yele matanki yanafanya kazi iliyotarajiwa.