Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa uwanja wa ndege katika eneo lililotengwa katika Kijiji cha Manga kwa msaada wa Benki ya Dunia?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti,
nishukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, kwa kuwa Singida Mjini ni mji ambao unakua kwa kasi sana kwa sababu Serikali imehamia Dodoma, Serikali haioni haja
sasa ya kutenga fedha kwenye bajeti ya mwaka huu ili uweze kuwalipa fidia wananchi wa kwenye hilo eneo la Manga na Uhamaka ilitoe hilo eneo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa
Serikali imeanza ukarabati kwenye uwanja wa ndege wa sasa, je, Serikali itamaliza ukarabati huo lini ili na sisi tuweze kuutumia uwanja huo kwa kupanda ndege? Ahsante sana.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Sima na wananchi wa Mji wa Singida wawe na subira, tupate taarifa ya mwisho ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili hatua ya pili ifuate. Si rahisi tukaanza
kutenga fedha kwa mwaka huu na hasa vipaumbele ambavyo tulipitisha mwaka huu, mtakumbuka ambavyo tulipitisha katika mpango wa mwaka huu wa fedha, vinahitaji rasilimali fedha nyingi na hivyo hii kazi tutaifanya mara badaa
ya kazi hii ya upembuzi yakinifu kukamilika. Itakuwa sio rahisi kwa mwaka huu, mnafahamu kwamba bajeti ya mwaka huu tumeshaipitisha katika ngazi ya Kamati na hivi sasa tunaanza kuingiza katika hatua za Bunge Zima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kuhusu ukarabati;
nimhakikishie Mheshimiwa Sima kwamba kazi hii ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina itakapokamilika suala la ukarabati litafuata.

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa uwanja wa ndege katika eneo lililotengwa katika Kijiji cha Manga kwa msaada wa Benki ya Dunia?

Supplementary Question 2

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nishukuru kwamba uwanja wa ndege wa Lindi upo kwenye mapendekezo ya Serikali ya kutaka kuufanyia
ukarabati lakini kwa sasa wananchi wa Lindi tunakosa huduma ya ndege mpaka twende Mtwara kwa kuwa uwanja ule sasa hivi umekuwa ni chakavu sana. Nataka commitment ya Serikali, ni lini itakamilisha ukarabati wa uwanja wa ndege
wa Lindi ili ndege zianze kutua kama kawaida?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli uwanja wa Lindi ni kati ya viwanja 11 vinavyofanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa kutumia fedha za mkopo kutoka Benki ya Dunia. Kimsingi kazi hii itakapokamilika ndipo
tutapata ratiba kamili ya tuanze wapi na tumalizie wapi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda tu nimkakishie
Mheshimiwa Bobali, kwamba kutokana na umuhimu wa kuhakikisha wananchi wa Lindi nao wanakuwa na kiwanja cha ndege, tutahakikisha katika kuangalia priority, na lindi tutaiangalia kwa macho matatu.

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa uwanja wa ndege katika eneo lililotengwa katika Kijiji cha Manga kwa msaada wa Benki ya Dunia?

Supplementary Question 3

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaishukuru sana Serikali kwa kupanua uwanja wa ndege wa Dodoma, lakini upanuzi huo umeathiri sana barabara ya Area D round about ya Shabiby, na wananchi wanaotoka Area D na Majengo Mapya
hurudi mpaka Kisasa kuja mjini kilometa nyingi.
Je, Serikali iko tayari kujenga barabara nyingine ya
lami kuwapunguzia safari ndefu wananchi wanaokaa maeneo ya Area D na Majengo Mapya?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba tunahitaji kuangalia upya namna Area C na Area D inavyoweza kufikika ukitokea Dar es Salaam bila mzunguko huo mkubwa kwa kuhakikisha tutapata barabara nyingine badala ya ile ambayo sasa hivi imefungwa kwa ajili ya kiwanja cha ndege. Kwa hiyo, namhakikishia Serikali nayo inalifikiria na tutalifanyia kazi kwa haraka hilo.

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa uwanja wa ndege katika eneo lililotengwa katika Kijiji cha Manga kwa msaada wa Benki ya Dunia?

Supplementary Question 4

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa sababu pia uwanja wa Musoma upo kwenye ajenda hiyo na kwamba upembuzi yakinifu umeshafanywa. Kwa sababu kutengwa fedha ni kitu kingine na ujenzi ni kitu kingine, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi katika uwanja wa Musoma?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Sokombi na wananchi wote wa Mji wa Musoma na viunga vyake ambao kwa kawaida wamezoea kutumia uwanja wa ndege wa Musoma kwa safari zao kwamba Serikali iko makini na katika muda wa
hivi karibuni kama mtakumbuka tuliwaambia katika viwanja vitatu vya mwanzo tutakavyohakikisha kwamba ujenzi wake unaanza haraka ni pamoja na Musoma, Nduli na Mtwara.
Naomba nimhakikishie Serikali ipo mbioni kuhakikisha viwanja hivi vitatu vinapata fedha na uzuri wake fedha za viwanja hivi vitatu vinatarajia ataketupa fedha maana sio mfadhili ni mkopehsaji hivi karibuni.

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa uwanja wa ndege katika eneo lililotengwa katika Kijiji cha Manga kwa msaada wa Benki ya Dunia?

Supplementary Question 5

MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipa fursa niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mheshimiwa
Naibu Waziri katika majibu yake ya msingi ametamka neno fidia, kuhusiana na kuwafidia wale watakaoathirika na ujenzi wa kiwanja cha ndege Singida. Kwa kuwa neno hilo fidia
amewatonesha na kuwakumbusha wananchi wa Mwibara ambao barabara ya Bunda, Kisoria na Nasio kwa miaka mingi hawajafidiwa. Je, wananchi hao wanataka kumsikia Mheshimiwa Naibu Waziri, ni lini watafidiwa au kwenye mwelekeo wa bajeti fidia ya Mwibara ipo? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Lugola amekuwa akifatilia sana suala la fidia katika eneo lake, na naomba nitumie fursa hii kumdhihirishia yale ambayo tumekuwa tukimwambia ofisini na maeneo mengine ambako amekuwa akituuliza swali hili ni sahihi, kwamba tunatafuta fedha kwa ajili ya kulipa fidia na kwa kweli nimhakikishie mara tutakapopata hizo fedha suala la fidia hilo tutalishughulikia kwa kazi sana.

Name

Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa uwanja wa ndege katika eneo lililotengwa katika Kijiji cha Manga kwa msaada wa Benki ya Dunia?

Supplementary Question 6

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa Manispaa ya Iringa na kiwanja cha ndege cha Nduli kimekaa kimkakati, ukizingatia kwamba Wizara ya Maliasili na Utalii inaboresha Southen Sackett kwa ajili ya kuimarisha utalii Kusini mwa Tanzania. Ni lini sasa Serikali ilikuwa imeahidi kwamba kiwanja hiki kitaboreshwa kama ambavyo Waziri amesema kwamba ni miongoni mwa viwanja 11 ili Manispaa ya Iringa iweze kukua kiuchumi na kimkakati kwa ajili ya ku-boost uchumi wa Taifa ambao kimsingi uchumi unaenda chini?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nilijibu swali la Mheshimiwa Sokombi, kwamba katika viwanja ambavyo tunatarajia kupata mkopo hivi karibuni ni kiwanja cha Musoma, Nduli na Mtwara. Kwa hiyo, naomba
nimhakikishie Mheshimiwa Msigwa kwamba kiwanja cha Nduli nacho kipo katika mtazamo wa mbele sana ili kuhakikisha kwamba utalii unaongezeka katika mbuga yetu ile ya Ruaha na kuleta mapato makubwa kwa Serikali.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa uwanja wa ndege katika eneo lililotengwa katika Kijiji cha Manga kwa msaada wa Benki ya Dunia?

Supplementary Question 7

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti,
ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niko kwenye Kamati ya Miundombinu; kwa kuwa uwanja huo huo wa Nduli tayari kuna pesa zimetengwa kwa ajili ya ukarabati huo lakini pia mradi huu umeshakubaliwa na wananchi kwa sababu
Serikali tayari ilishakaa na wananchi waliopo katika eneo lile. Sasa naomba jibu kutoka kwa Serikali, kwa sababu kuna wananchi ambao wamekuwa wakiendeleza maeneo ambayo yataguswa sasa ni lini itaweka alama na ili
wasiyaendeleze maeneo yale ili wakati wa kulipa fidia pesa iwe kidogo?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Ritta Kabati amekuwa akihoji haya masuala ndani ya Kamati ya Miundombimu na mimi niendelee kumpongeza kwa namna anavyochukua hatua kuwatetea wananchi na kuhakikisha kwamba maslahi yao yanazingatiwa na Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu kama
ambavyo nimekuwa nikimhakikishia mara nyingi katika Vikao vya Kamati, kwamba kazi hii ya kuweka alama tutaifanya hivi karibuni. Naongelea si zaidi ya miezi mitatu, minne ijayo kazi hii itakuwa imekamilika ili kuhakikisha kwamba wananchi wa pale wanajua mipaka ya maeneo tutakayotumia katika kukarabati na kupanua ule uwanja wa Nduli.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa uwanja wa ndege katika eneo lililotengwa katika Kijiji cha Manga kwa msaada wa Benki ya Dunia?

Supplementary Question 8

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Tunaunga mkono juhudi ambayo inafanyika ya kuboresha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam. Lakini kuna malalamiko ya muda mrefu ya wananchi wa Kata ya Kipawa, Ukonga - Kipunguni, Kigiragira kule Buyuni, wanadai fidia Serikali mpaka leo na
wameshindwa kufanya shughuli za kimaendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kujua ni lini
mgogoro huo utamalizwa na Serikali ili uwanja ukamilike na wananchi wakaendelea kuwa na amani na kuishi maisha ambayo na wenyewe wanapaswa kuishi kama binadamu wa kawaida hapa Tanzania? Ahsante.

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tena kumthibitishia Mheshimiwa Waitara pamoja na jirani yake Mheshimiwa Bonnah Kaluwa, Mbunge wa Segerea kwamba kazi mlioifanya, mtakumbuka mimi ndio Mbunge wa Segerea alinileta kukutana na wale wananchi wa Kipunguni, kuhusiana na suala hili. Niwaombe kwamba tulidhamiria suala hili tutalimaliza katika miaka hii mitano. Mnafahamu baadhi ya maeneo tumeshaanza kulipa fidia, Mheshimiwa Bonnah
Kaluwa unalifahamu hilo na umelifuatilia kwa kasi sana na ninakuhakikishia pamoja na Mheshimiwa Waitara kwamba wananchi wale watalipwa fidia katika miaka hii mitano. Kuna matatizo ambayo yapo katika suala hili la fidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tunashughulikia matatizo yaliyoingiliwa katika suala hili la fidia, kuna wajanja wachache walitumia fursa wakatumia fedha vibaya na tumepelekea PCCB wanafanya kazi, tutakapopata taarifa PCCB tutakuja kulimaliza hili suala la fidia katika wale ambao wamebakia kulipa.