Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS Aliuliza:- Biashara ya vyuma chakavu imeshamiri sana Tanzania Bara na Visiwani na imesababisha madhara ya kuharibiwa na kuibiwa kwa miundombinu yakiwemo mifuniko ya chemba na majitaka. (a) Je, Serikali imejipangaje kupambana na wizi na uharibifu huo wa mali za Serikali na wakati walinzi wa maeneo husika wanashuhudia hayo? (b) Je, Serikali haioni kwamba hata usalama wa raia na mali zao uko mashakani?

Supplementary Question 1

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nashukuru Mheshimiwa Waziri alivyonijibu vizuri na kwa ufasaha swali langu, lakini nitakuwa na maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Waziri, je, kwa nini Serikali haioni
umuhimu wa kuwepo vyombo vya awali vya kuhakiki aina au bidhaa mbalimbali ya vyuma chakavu kabla havijafika sokoni?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kwa nini usiwepo
utaratibu wa kutofautisha biashara ya vyuma chakavu kabla ya kuharibu miundombinu ya Serikali ambayo sasa hivi imeenea nchi nzima kila mahali vinang’olewa? Kungekuwa na uhakiki kabla ya hivyo vyuma chakavu kuweza kufika
sokoni na kuweza kuuzwa? Ahsante.

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ile dhana ya kutumia vyuma chakavu ambavyo kimsingi vinakuwa havitakiwi kwenda kuviyeyusha na kutengeneza chuma ni wazo zuri. Tatizo lililopo ni kwamba watu wenye tamaa, wahalifu ndiyo wanaharibu ile dhana nzuri, hawa ni wahalifu kama wahalifu
wengine. Sasa chombo cha awali cha kuweza kuzuia watu hawa ni wananchi, kama inavyosema Katiba ya nchi yetu, ulinzi wan chi hii ni jukumu la wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwenye ile
miundombinu mikubwa kama ile ya TANESCO nilivyosema, TANESCO anaweka ulinzi akisaidiana na wananchi walio wema. Nina imani huo ndio mfumo mzuri wa kuweza kulinda miundombinu yetu Tanzania nzima, Wizara yangu au Serikali
haiwezi kutengeneza polisi wa kulinda vyuma kuanzia vile vya taasisi mpaka vyetu binafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu wa kutofautisha, kama ilivyo kwa wale wanaoharibu miundombinu kwenda kujipatia pesa wapo hata wenye viwanda ambao wanapokea vyuma ambavyo wazi kabisa vinaonekana vimetoka kwenye miundombinu ya Serikali au ya watu, hao
mimi ndio nakula nao sahani moja. Ma-inspector wangu wanatembelea viwanda hivyo na ni vichache vinajulikana na naendelea kuwapa elimu, atakayebainika atajuta kwanini alifanya hivyo.

Name

Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS Aliuliza:- Biashara ya vyuma chakavu imeshamiri sana Tanzania Bara na Visiwani na imesababisha madhara ya kuharibiwa na kuibiwa kwa miundombinu yakiwemo mifuniko ya chemba na majitaka. (a) Je, Serikali imejipangaje kupambana na wizi na uharibifu huo wa mali za Serikali na wakati walinzi wa maeneo husika wanashuhudia hayo? (b) Je, Serikali haioni kwamba hata usalama wa raia na mali zao uko mashakani?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Suala la biashara ya vyuma chakavu inaonesha ni wazi kuna soko zuri la chuma nchini na nje ya nchi. Sasa kifupi tu, sijui mradi wa chuma Liganga na Mchuchuma umefikia wapi ili nchi ifaidike na soko hilo? Ahsante.

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa Mchuchuma na Liganga; katika mpango wa Serikali wa miaka mitano wa ujenzi wa uchumi wa viwanda, mchuma na Liganga ipo. Nilipofikia mimi; hili suala liko mezani kwangu. Nimepitia vivutio vyote vya mwekezaji alivyoweka, nimevikamilisha, vinakwenda kwenye mamlaka kusudi waweke sahihi, mwekezaji yuko tayari kuweka fidia na kuweza kuanza. Nikipata sahihi ya mamlaka tunaanza kazi.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS Aliuliza:- Biashara ya vyuma chakavu imeshamiri sana Tanzania Bara na Visiwani na imesababisha madhara ya kuharibiwa na kuibiwa kwa miundombinu yakiwemo mifuniko ya chemba na majitaka. (a) Je, Serikali imejipangaje kupambana na wizi na uharibifu huo wa mali za Serikali na wakati walinzi wa maeneo husika wanashuhudia hayo? (b) Je, Serikali haioni kwamba hata usalama wa raia na mali zao uko mashakani?

Supplementary Question 3

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa
Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa hii biashara ya vyuma chakavu inavikumba pia viwanda vilivyobinafsishwa kwa muda mrefu sasa kikiwemo Kiwanda cha Nyuzi Tabora, na kwa kuwa kuna taarifa kwamba mashine nyingi mle ndani zimeuzwa kama chuma chakavu na kimefungwa kile kiwanda, je, Mheshimiwa Waziri, kwa sababu nimewahi kulalamika hapa Bungeni na kutoa taarifa kuhusu kufanyika kwa vyuma
chakavu, ni lini tunaweza tukaenda tukakagua kile kiwanda kwa sababu sasa hivi umetoka kusema utakula nao sahani moja, tuweze kujua kama vile zile mashine hazijauzwa kama vyuma chakavu?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kiwanda cha Nyuzi cha Tabora kina mwenye nacho (owner) kwa hiyo, mwenye mali anapoibiwa mimi siwezi kwenda kuangalia mali yake yule, lakini taarifa nilizonazo kutoka kwa mwenye kiwanda ameniambia amepata soko la nyuzi na kiwanda hicho kitaanza kazi. Kwa hiyo, mimi naweza kumbana yule kwa kupitia msajili wa hazina kwamba aanze kazi na ndio wajibu wangu. Sasa kama alizembea, mali ikaibiwa mle hilo nadhani ni suala la kila abiria achunge mzigo wake.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS Aliuliza:- Biashara ya vyuma chakavu imeshamiri sana Tanzania Bara na Visiwani na imesababisha madhara ya kuharibiwa na kuibiwa kwa miundombinu yakiwemo mifuniko ya chemba na majitaka. (a) Je, Serikali imejipangaje kupambana na wizi na uharibifu huo wa mali za Serikali na wakati walinzi wa maeneo husika wanashuhudia hayo? (b) Je, Serikali haioni kwamba hata usalama wa raia na mali zao uko mashakani?

Supplementary Question 4

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa fursa hii. Ni takribani miaka kumi sasa toka hili swali linaulizwa. Nakumbuka lile Bunge la Tisa niliuliza hili swali
mwaka 2007 na Bunge la Kumi aliuliza Mheshimiwa Maida.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jibu la Serikali siku zote ni kwamba muswada unaandaliwa. Ni lini sasa muswada huo utaletwa hapa Bungeni ili uweze kupitishwa kama sheria?

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Answer

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mbunge najua una imani na mimi. Sasa upele umepata mkunaji, safari hii unaletwa chini ya uongozi wangu.