Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. PAULINE P. GEKUL (K.n.y. MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliluiza:- Mkao Makuu ya Wilaya ya Kyerwa yamewekwa katika Kata ya Kyerwa. Je, ni mchakato gani ulifanyika mpaka Kata ya Kyerwa kuwa Makao Makuu ya Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti
nikushukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.
Kwanza, kwa kuwa michakato hii inachukua muda mrefu sana ambayo inaanzia kwenye ngazi za vijiji mpaka juu kama Naibu Waziri alivyosema.
Je, endapo michakato hii katika ngazi za chini
itakamilika mapema, nini kauli ya Serikali Kuu ili na wao waharakishe na wananachi hawa wapate haki zao?
Swali la pili, kwa kuwa tunapokaribia wakati wa
Uchaguzi Mkuu, Serikali imekuwa na hali ya kugawa kata zetu na vijiji ili kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma kwa karibu. Naomba nifahamu Serikali ina mpango gani
kuanza mchakato huo mapema kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili kuondoa usumbufu na maandalizi pia ya muhimu kwa wananchi hawa ambao maeneo yao ni makubwa na Kata zao ni kubwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA
SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti kwanza katia
sehemu ya kwanza ni kwamba mchakato umekamilika na
Makao Makuu ya Halmashauri imeshathibitishwa ndiyo ile
ambayo imetajwa pale isipokuwa Mheshimiwa Mbunge
alikuwa na utata katika hayo Makao Makuu mapya, kwa
hiyo mchakato huo ulishakamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala zima la kugawa
wakati wa kuelekea kwenye uchaguzi nadhani hii sasa ni
mamlaka zetu katika Ward Council zetu, vikao vyetu vile vya
kisheria kama nilivyovisema, ambapo inaonesha baadaye
jambo hili litaenda katika Tume ya Uchaguzi kupita Ofisi ya
Waziri Mkuu.
Kwa hiyo, hakuna shaka naamini kwamba kila mtu
katika maeneo yake anabaini changamoto zinazokabili eneo
hilo na tutafaya maandalizi ya awali ilimradi kuepusha
ukakasi kwamba maeneo yanagawiwa muda mfupi kabla
ya uchaguzi.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PAULINE P. GEKUL (K.n.y. MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliluiza:- Mkao Makuu ya Wilaya ya Kyerwa yamewekwa katika Kata ya Kyerwa. Je, ni mchakato gani ulifanyika mpaka Kata ya Kyerwa kuwa Makao Makuu ya Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Kwa kuwa Wilaya ya Ngorongoro ni kubwa kuliko
Mkoa wa Kilimanjaro, hali inayopelekea jiografia ya Wilaya hiyo kuwa ngumu. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kugawa Wilaya hii ya Ngorongoro au kuweka Halmashauri mbili ili kuwasogezea wananchi wa Ngorongoro huduma kwa karibu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli na Mheshimiwa Mbunge pale wa Jimbo hio la Ngorongoro ambalo Naibu Waziri wa Kilimo na yeye alinialika niweze kufika kule jimboni kwake juzi juzi hapa nilikuwepo kule. Kwa
umbali kweli jiografia ya Ngorongoro ina changamoto kubwa sana kwa sababu ukianzia hapa getini ukitoka hapa Karatu mpaka unafika Makao Makuu kule Loliondo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nilipata fursa ya
kutembelea mpaka Ziwa Natron kwenda shule ya sekondari ya Ziwa Natron. Jiografia ya Ngorongoro kweli ni kubwa zaidi, lakini mara nyingi sana maeneo haya yanagawanywa kutokana na population.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia eneo kubwa la Ngorongoro ni hifadhi, lakini kama kutakuwa na haja ya kuweza kugawanya basi kwa mchako ule ule wa kisheria wananchi wa aeneo hilo watafanya hivyo na Serikali itaangalia kama kuna umuhimu wa kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini inawezekana
tunaweza tukaangalia mbali kwa sababu Ngorongoro na Serengeti ukiangalia jiografia yao ina changamoto kubwa sana. Hili sasa tuwaachie wenye maeneo hayo mkaweza kufanya maamuzi sahihi kama ulivyo Mheshimiwa Catherine Magige unavyokuwa na wazo hilo, basi na Serikali itaangalia nini cha kufanya kwa maamuzi sahihi kwa maslahi mapana kwa wananchi wa Ngorongoro.