Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Koryo kwa kushirikiana na Mbunge wao na wananchi wa Rorya wanaoishi Mwanza, Arusha na Dar es Salaam wamejenga wodi ya akina mama na watoto pamoja na kununua jokofu lakini mapungufu yaliyopo sasa ni Jengo la upasuaji. Je, Serikali sasa haioni ipo haja ya kusaidia jengo hilo pamoja na vifaa vyake?

Supplementary Question 1

MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, je, Serikali ina mpango gani wa kuzielekeza Halmashauri kutumia force account ili miradi midogo midogo kama hii iweze kutengenezwa kwa fedha ndogo na iweze kuleta impact?
Swali la pili, kwa kuwa jambo hili linafanana kabisa
na vituo vya afya vilivyoko Jimbo la Magu katika kituo cha afya Lugeye pamoja na Nyanguge. Serikali ina mpango gani wa kuvijengea majengo ya upasuaji ili wananchi waweze kupata huduma karibu? Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali hivi sasa si kutoa maelekezo, tayari tumeshatoa maelekezo hivi sasa na Halmashauri mbalimbali zinaendelea kutumia force account na tumepata mafanikio makubwa sana, kwa sababu maeneo mbalimbali unapopita hivi sasa mradi ambao zamani ulikuwa saa nyingine ulikuwa unagharimu shilingi milioni 150 utakuta sasa hivi milioni 70 mradi umekamilika tena upo katika ubora unaokusudiwa.
Kwahiyo Mheshimiwa Kiswaga ni kwamba sasa hivi jambo hilo linaendelea na linaendelea kwa ufanisi mkubwa, na nipende kuwashukuru sana Wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi ambao wanasimamia jambo hili kwa uzuri zaidi
na hasa Waheshimiwa Wabunge katika Majimbo yenu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, katika suala zima la Jimbo la Magu ambalo Mheshimiwa Mbunge umesema na ni kweli, katika harakati za Serikali tuna mpango ambao si muda mrefu sana tutakuja kuuanza katika kituo chako kimoja cha afya tutakuja kujenga jengo la upasuaji na kuweka vifaa tiba vyote. Kwa hiyo, naomba nikushauri
Mheshimiwa Mbunge kwamba usiwe na wasiwasi Serikali yako kama kila siku inavyopiga kelele hapa Bungeni itaendelea kushirikiana nanyi na ujenzi huo Mungu akijaalia utaanza hata kabla ya mwezi wa sita.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Koryo kwa kushirikiana na Mbunge wao na wananchi wa Rorya wanaoishi Mwanza, Arusha na Dar es Salaam wamejenga wodi ya akina mama na watoto pamoja na kununua jokofu lakini mapungufu yaliyopo sasa ni Jengo la upasuaji. Je, Serikali sasa haioni ipo haja ya kusaidia jengo hilo pamoja na vifaa vyake?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Katika Mkoa wa Arusha kuna majimbo saba na katika majimbo hayo majimbo mawili yana jiografia ngumu sana
ikiwemo Jimbo la Longido na Jimbo la Ngorongoro. Je, Serikali iko tayari sasa katika bajeti tunayoiendea kutazama majimbo haya kwa mujibu wa jiografia yao ili wananchi wanaoishi
katika maeneo hayo waweze kupata huduma za afya kwa urahisi na kwa wakati?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba Serikali inapeleka nguvu kubwa sana katika eneo hilo, na ndiyo maana juzi juzi nilikuwa katika Wilaya hizo zote mbili;
Wilaya ya Longido pamoja na Wilaya ya Ngorongoro, katika Wilaya ya Ngorongoro siyo muda mrefu sana Mungu akijaalia katika kipindi hiki cha katikati tutakwenda kuwekeza nguvu
kubwa sana kwa kupeleka takribani milioni 700. Lengo kubwa ni kwamba maeneo yale yana jiografia tata sana wananchi waweze kupata huduma kujua kwamba Serikali yao ipo
vitani katika kuhakikisha kwamba wananchi wanapata huduma hiyo inayokusudiwa.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Koryo kwa kushirikiana na Mbunge wao na wananchi wa Rorya wanaoishi Mwanza, Arusha na Dar es Salaam wamejenga wodi ya akina mama na watoto pamoja na kununua jokofu lakini mapungufu yaliyopo sasa ni Jengo la upasuaji. Je, Serikali sasa haioni ipo haja ya kusaidia jengo hilo pamoja na vifaa vyake?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kuna wilaya nyingi mpya ambazo zina matatizo sana ya hata kutokuwa na Hospitali za Wilaya. Na kwa kuwa majibu yake anasema kwamba kuna fedha ambazo zimetengwa, je, Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza kunihakikishia kwamba katika Wilaya ya Busega kituo cha Nasa hizo fedha zitapatikana lini?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Dkt. Chegeni unafahamu na wewe kule kwako umenikaribisha, nakushukuru sana. Hicho kituo cha afya ulichokisema
miongoni mwa maeneo ambayo yana changamoto, na akina mama wanapata shida kubwa sana kupata huduma za upasuaji. Nilikueleza wazi kwamba katika kipindi cha huu
mwaka tutafanya kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba tunajenga jengo la upasuaji kama nilivyosema katika maeneo mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kuwa na imani,
kwamba Serikali kwa kupitia Wizara ya afya tuna mkakati mpana sana kuhakikisha kwamba tunapelekea huduma katika maeneo hayo na Mungu akijaalia kabla ya mwezi wa sita tunaweza tukaenda kuweka jiwe la msingi sawa sawa
na kituo cha afya cha Malya kule kwa ndugu yangu Ndassa.

Name

Grace Sindato Kiwelu

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:- Wananchi wa Kata ya Koryo kwa kushirikiana na Mbunge wao na wananchi wa Rorya wanaoishi Mwanza, Arusha na Dar es Salaam wamejenga wodi ya akina mama na watoto pamoja na kununua jokofu lakini mapungufu yaliyopo sasa ni Jengo la upasuaji. Je, Serikali sasa haioni ipo haja ya kusaidia jengo hilo pamoja na vifaa vyake?

Supplementary Question 4

MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti katika hospitali yetu ya Wilaya ya Siha hatuna hatuna jokofu na imekuwa inaleta usumbufu sana kwenye kuhifadhi miili ya marehemu wetu.
Je, ni lini Serikali itatuletea jokofu kupunguza upungufu huo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Hospitali ya Siha takribani wiki sita zilizopita nilikuwa pale Siha na namshukuru sana Mbunge tulikuwepo pamoja na
tulitembelea hospitali ile na kipindi kilichopita hapa nilitoa maelekezo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilivyofika pale Siha,
kutokana na changamoto tuliyobaini pale, kwamba tumepeleka fedha lakini matumizi yale ya fedha tumeona hayaelekezwi sawa sawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kabla ya jokofu kuanza kuna suala zima la fedha tulizozipeleka pale lazima zitumike vizuri na tumeshatoa maelekezo hayo. Lengo letu ni kwamba lile jengo, floor ya juu iweze kukamilika vizuri lakini hatuachi hapo kwa sababu changamoto kubwa ya pale lazima tuhakikishe hospitali ile inafanya kazi vizuri na Serikali
itaweka nguvu za kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulishapeleka zaidi ya milioni 250, inafanya kazi lakini suala la jokofu litakuwa ni kipaumbele chetu ili kuhakikisha, lengo kubwa hospitali ile inafanya vizuri kwa wananchi wa Siha.