Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. JASSON S. RWEIKIZA Aliuliza:- Kampuni ya Chai ya Maruku imekuwa sugu kwa kutowalipa wakulima wanaoiuzia chai pamoja na kutowalipa wafanyakazi wake wenyewe. Je, ni kwa nini Serikali haichukui hatua ya kuwasaidia wakulima na wafanyakazi hao ili kupata haki yao?

Supplementary Question 1

MHE. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza siyo kweli kwamba amelipa madeni hadi Oktoba mwaka jana. Madai ninayo bado yapo mengi yana zaidi ya mwaka mmoja, miaka miwili sasa nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, inakuaje Serikali inampa mtu kiwanda kwa mikataba na kwa utaratibu unaokubalika anashindwa kutimiza wajibu wake ambao ni pamoja na kulipa bei za wakulima na mishahara ya watumishi Serikali
inamuangalia tu mwekezaji huyo, anasema hapa ameahidi ambapo siyo kweli kama nilivyosema na Serikali inamuangalia tu huyu inasema ameahidi halafu inamuachia?
Swali la pili, wakulima hawa ambao hawalipwi hela yao ya chai ndiyo wakulima hawa ambao wanalima kahawa. Tumesema humu mara nyingi kahawa ina bei hafifu. Wizara ni hiyo hiyo ya kilimo imeagizwa na Mheshimiwa Rais iondoe kodi kwenye zao la kahawa, kodi ziko nyingi karibu
30. Kwa nini mpaka leo kodi hazijaondolewa na wakulima hawa wanazidi kuumia, kwenye chai wanaumia na kwenye kahawa wanaumia? Ahsante sana.

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI:
Mheshimiwa Spika, kuhusu kama ni kweli au siyo kweli kwamba tayari haya malipo yamefanyika, mimi nipo tayari kukaa na Mheshimiwa Mbunge ili tufananishe taarifa tulizonazo, kwa sababu kwa ripoti ambayo ninayo na ambayo ni ya Serikali inaonesha kwamba kuna malipo yamefanyika lakini niko tayari kukutana nae, tujadili tuone
taarifa sahihi ni ipi.
Mheshimiwa Spika, vilevile mazingira ya kampuni
ambayo anazungumzia ni magumu kidogo kwa sababu wakulima wenyewe ni wamiliki vilevile wa hisa kwenye kampuni ile kwa hiyo ilipobinafsishwa na Serikali wakulima wa chai vilevile nao waliweza kupata asilimia fulani. Pamoja na changamoto ambazo zimekuwepo bado wakulima nao vilevile ni wamiliki wa kiwanda kwa kiasi kikubwa, lakini kama nilivyosema Serikali imekuwa ikiendelea kuwasiliana na kiwanda ili kuondoa hizo changamoto ambazo zimetokea.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala la pili, ni kweli kama Mheshimiwa Mbunge alivyosema kwamba kumekuwepo na manung’uniko ya haki kabisa kuhusu tozo na kodi nyingi ambazo zimepitiliza katika zao la kahawa na mazao mengine. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge
kwamba siku tutakaposoma hotuba yetu kwa ajili ya mwaka ujao wa fedha awepo maana yake tutaziondoa tozo mwaka huu mpaka nyingine mtatuomba tuzirudishe.

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JASSON S. RWEIKIZA Aliuliza:- Kampuni ya Chai ya Maruku imekuwa sugu kwa kutowalipa wakulima wanaoiuzia chai pamoja na kutowalipa wafanyakazi wake wenyewe. Je, ni kwa nini Serikali haichukui hatua ya kuwasaidia wakulima na wafanyakazi hao ili kupata haki yao?

Supplementary Question 2

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Spika, ni jambo la kushangaza na
kusikitisha kwa sababu wafanyakazi mimi nina malalamiko yao, nina document nitaweza kumletea Mheshimiwa Waziri hawajalipwa wale wafanyakazi na wengine wamefikia mahali pa kustaafu hawajapata hata pesa zao. Kile kiwanda
kimebaki kubadilishwa na wasimamizi mara kwa mara kwa ajili ya kutaka kuwadhulumu wafanyakazi pamoja na wakulima. Ni lini Waziri utakwenda pale kuhakikisha wewe mwenyewe kwamba wafanyakazi wameshalipwa? Mheshimiwa Spika, nina uhakika hawajalipwa hata senti tano.

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI:
Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwishasema kwa
Mheshimiwa Rweikiza, niko tayari kukutana na Waheshimiwa Wabunge ili tufananishe taarifa tulizonazo. Taarifa sisi tuliyonayo ni kwamba tayari kuna malipo ambayo yamefanyika siyo yote sawa, lakini niko tayari kama nilivyosema kukutana nae ili tuangalie kwamba nani ana taarifa sahihi na vilevile Wizarani au Serikalini kama kuna Afisa
ambaye ameniletea mimi taarifa za uongo atachukuliwa hatua.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. JASSON S. RWEIKIZA Aliuliza:- Kampuni ya Chai ya Maruku imekuwa sugu kwa kutowalipa wakulima wanaoiuzia chai pamoja na kutowalipa wafanyakazi wake wenyewe. Je, ni kwa nini Serikali haichukui hatua ya kuwasaidia wakulima na wafanyakazi hao ili kupata haki yao?

Supplementary Question 3

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nianze kwa
kupongeza Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa ushirikiano wanaonipa kuhakikisha kwamba tunapata zao jipya Tanzania, zao linaloitwa stevia kupitia Jimbo langu la Ngara.
Mheshimiwa Spika, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi tayari wameshatoa kibali cha kuingiza mbegu ya zao la stevier zao ambalo ni sukari ambayo ni anti-diabetes, antipressure lakini zao ambalo ni zao la kuinua kipato cha Watanzania. Pamoja na kutoa kibali hicho kwa sababu ni
zao geni tunahitaji kufanya utafiti kwanza na tayari Wizara imeelekeza Kituo cha Utafiti Maruku ambacho kiko Mkoa wa Kagera kushirikiana na Kampuni ya East African Stevier and Agro-Investment kufanya utafiti wa zao hilo lakini tatizo ni fedha za kufanyia utafiti. Je, Wizara ya kilimo, Mifugo na Uvuvi wako tayari kutenga pesa ili kuwezesha kituo cha utafiti Maruku kushirikiana na Kampuni ya East Africa Stevier kutoa pesa ili kuweza kufanya utafiti huu na hatimae zao hilo liweze kuanzishwa katika nchi yetu ya Tanzania na kuleta mabadiliko ya uchumi?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI:
Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Gashaza kwa jitihada na ubunifu ambao ameufanya Jimboni kwake katika kutafuta mazao ambayo yana tija kwa wakulima. Kimsingi tumekuwa tukishirikiana naye kama Wizara ili kuangalia namna ya kuleta nchini zao la stevier
ambalo huko maeneo mengine linakolimwa lina tija kubwa sana. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kama ambavyo tayari tumeshashirikiana naye katika hatua za kusajili hilo zao, Wizara iko tayari vilevile kushirikiana naye na wananchi wake katika kufanya utafiti katika kituo chetu cha Maruku ili zao hilo liweze kuanza kulimwa nchini na Wizara iko tayari kutenga bajeti ya kawaida ya utafiti kwa kituo hicho ili utafiti huo uweze kufanyika.