Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI Aliuliza:- Serikali iliahidi kujenga madaraja ya Shaurimoyo, Nakalolo na Miesi. Je, ni lini madaraja hayo yatajengwa?

Supplementary Question 1

MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Kwa kuwa Naibu Waziri anayeshughulika na barabara yupo, je, anaweza akalithibitishia Bunge hili kwamba fedha hizi TANROADS
wameshazitenga kweli kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii? Swali langu la pili, je, ni lini madaraja haya yatajengwa, kwa sababu wananchi hawa wa maeneo ya Miesi, Kata za Mkundi na Mpindimbi kwa miaka minne sasa wanapata tatizo kubwa sana baada ya madaraja haya yaliyokuwepo kuzolewa na mafuriko, je, ni lini baada ya bajeti
kazi itaanza?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge sana kwa harakati zake kubwa na kazi kubwa anayofanya katika Jimbo lake kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za maendeleo. Kama tulivyosema, kutokana na kazi hiyo nzuri
ambayo ameifanya ndiyo maana sasa, kwa sababu barabara ile ilikuwa chini ya barabara ya Halmashauri lakini kutokana na msukumo mkubwa ndiyo maana TANROADS imeamua kufanya assessment ya barabara ile na kukubali
kwamba madaraja haya yataweza kujengwa.
Nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge hilo ondoa hofu kwa sababu kwanza imeshafanyika hiyo tathmini na kuona kwamba shilingi bilioni tatu na ofisi ya ujenzi naamini katika harakati za hii bajeti ambayo itakuja hapa tutaona katika jedwali hilo ambalo linaeleza kwa sababu tathmini wameshaifanya tayari.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, suala la ni lini barabara hii itajengwa. Barabara hii itajengwa mara baada ya kutengwa kwa bajeti, kwa hiyo, naomba nikuondoe hofu Mheshimiwa Dismas kwa sababu wananchi wa eneo lile wana umuhimu mkubwa wa barabara hii ambayo ni barabara ya kimkakati kwa suala zima la uchumi wa korosho katika maeneo haya, naomba ondoa hofu. Serikali iko tayari kuhakikisha kwamba itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha wananchi wa Lulindi wanapata huduma ya ujenzi wa barabara.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI Aliuliza:- Serikali iliahidi kujenga madaraja ya Shaurimoyo, Nakalolo na Miesi. Je, ni lini madaraja hayo yatajengwa?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika,
ahsante kwa kunipa nafasi hii na mimi niulize swali dogo la nyongeza. Matatizo yaliyoko huko Lulindi yapo katika Jimbo la Manyoni Magharibi, kuna barabara kutoka Idodyandole kwenda Ipangamasasi, kuna tawi la Mto Kizigo imekuwa ni
korofi sana na kwa nguvu ya Halmashauri hatuwezi kujenga;
Je, Mheshimiwa Waziri anaweza akatuahidi angalau kwa maneno kwamba Serikali kupitia TANROADS itatusaidia katika kipande hicho kidogo cha daraja?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba tupewe muda mfupi tu, hatutahitaji muda mrefu tutakuja kutoa taarifa ya barabara ambazo tunapendekeza zipandishwe hadhi na nyingine zikasimishwe kwa TANROADS.
Naomba tu nitoe tahadhari, inaonekana maombi ni mengi sana na tukipeleka barabara nyingi sana TANROADS uwezo wao kwa sababu kifedha haiongezeki sana kulinganisha na mzigo tunaowapa, tusije tukaishia nazo zikawa za sub standard kwa sababu kazi ni kubwa na uwezo
ni mdogo.
Kwa hiyo, nilitaka tu nitoe tahadhari hiyo lakini tutakuja kutoa taarifa hivi karibuni ni zipi zitapandishwa hadhi na zipi zitakasimiwa kwa TANROADS.
Mheshimiwa Spika, naomba tupewe muda kidogo.