Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:- Serikali imeweka mpango wa umeme vijijini ambapo kwa Jimbo la Magu ni asilimia 20 tu ya vijiji ndivyo vimepata umeme ambalo ni hitaji muhimu kwa kila Mtanzania:- (a) Je, asilimia 80 ya vijiji vilivyobaki vitapata lini umeme? (b) Je, Serikali imejipangaje kukabiliana na tatizo la kukatikakatika kwa umeme nchini?

Supplementary Question 1

MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pia nashukuru majibu ya Serikali na kuwapongeza Wizara hii kwa jinsi wanavyoshughulikia masuala haya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Wizara inatambua kwamba Magu bado vijiji 85 na 34 vitaingizwa kwenye mpango wa REA III, je, Wizara inaonaje kuviingiza vijiji vyote vilivyobaki kwenye mpango huu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa REA II inaendelea na miradi kule Magu na kwa sababu baadhi ya vijiiji mkandarasi ameondoa nguzo ambazo zilikuwa zinategemewa na wananchi na wananchi wengine hawajawekewa, je, Mheshimiwa Waziri anaweza kuambatana nami kwenda Jimboni kwangu kutembelea vijiji hivyo pamoja na Vijiji vya Mahaha, Nobola, Bungilya, Mwamabanza na Matale? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakubaliana na Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wengine na naamini kila Mbunge angependa sana vijiji vyake vyote viingie kwenye REA III. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tunaendelea kufanya tathmini kama itaonekana ipo haja ya vijiji vyote kuingia basi vitaingia lakini kutegemeana na bajeti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la pili la kuondoa nguzo kwenye maeneo mengine na kupeleka maeneo mengine, hili nimelichukua. Sambamba na hilo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi tuko tayari kutembelea maeneo yote yenye kero za umeme na kuhakikisha kwamba zinatoweka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ridhaa yako niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge, usambazaji na upatikanaji wa umeme nchini ulianza mwaka 1908 enzi za ukoloni wa Mjerumani. Kwa hiyo, miundombinu mingi sana imeharibika kama transfoma na mingine, kwa hiyo, tunaendelea na ukarabati. Kwa hiyo, maeneo mengine ambayo Waheshimiwa Wabunge mtapenda tutembelee, tutaendelea kutembelea na tutaendelea kuboresha lengo ni kuhakikisha wananchi wote wanapata umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba lengo letu ni wananchi wote wapate umeme. Nimwombe sana Mheshimiwa Lukuvi kwa sababu anaimarisha nyumba za wananchi, sisi hatutajali kumwekea mtu umeme eti mpaka awe na nyumba nzuri, tutamtundikia umeme hata kwenye mkaratusi karibu na nyumba yake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:- Serikali imeweka mpango wa umeme vijijini ambapo kwa Jimbo la Magu ni asilimia 20 tu ya vijiji ndivyo vimepata umeme ambalo ni hitaji muhimu kwa kila Mtanzania:- (a) Je, asilimia 80 ya vijiji vilivyobaki vitapata lini umeme? (b) Je, Serikali imejipangaje kukabiliana na tatizo la kukatikakatika kwa umeme nchini?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa matatizo ya Jimbo la Kavuu yanafanana kabisa na matatizo ya Jimbo la Magu na hivi karibuni kupitia mpango wa REA wameweza kuweka umeme katika Kata yangu ya Usevya katika Jimbo la Kavuu. Hivi karibuni umeme umeanza kuwaka takribani wiki tatu baada ya REA kukamilisha ujenzi wake pale lakini mpaka sasa hivi wananchi hao hawana umeme ikiwemo pamoja na mimi. Je, kwa kuwa wananchi wale walikuwa na hamu na umeme huo ambao haupatikani, Serikali inasema nini kuhakikisha kuanzia sasa umeme unapatikana?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge kwamba yapo maeneo ambayo hayana umeme hadi sasa. Kwa ridhaa yako niombe kusema kwamba nitakaa na Mheshimiwa Mbunge ili tuyatambue kwa kina maeneo ambayo hayana umeme na tuyafanyie kazi ili wananchi wapate umeme.